Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,808
- 218,460
Katika mkutano wake mkubwa wa hadhara wa Morogoro mjini leo hii, ambao bila shaka umevunja rekodi ya mahudhurio, pamoja na mambo mengine, Tundu Lissu anahoji anayebandika mabango nchi nzima yakiwa na picha yake na ya watu wengine kwamba eti wamepatanishwa. Amehojiwa kama wamepatanishwa, wamepatanishwa na nani? Anadai kwamba hizo ni propaganda za kichovu, na kwamba anawezaje kupatanishwa huku kukiwa na watu waliouawa, kutekwa na kuumizwa na hatima yao wala habari zao hadi leo hazijulikani?
Akiongea kwa uchungu, Lissu anadai yeye mwenyewe alitandikwa risasi na hadi leo hakuna yeyote aliyekamatwa. Anawezaje kupatanishwa na watu wa aina hiyo? Anadai sasa hivi anaitwa CHIBA kutokana na majeraha ya wauaji wake (kwa wasiolewa Chiba ni lugha ya mjini ikimaanisha mlemavu wa mguu).
Amezungumzia kupotezwa kwa watu wengi sana, akiwemo Ben Saanane, ambao hawajulikani walipo hadi leo, huku wenye madaraka au vyombo vya dola vikinyamaza. Anasema katika hali hii anawezaje kupatanishwa na waliokuwa madarakani, unyama huu ukitendwa? Na kwamba ambaye hayupo miongoni mwa watenda unyama huo ni mmoja tu, lakini wengine wote bado wapo. Hapa unapatanishwaje?
Lissu anadai Arusha ndio mkoa unaoongoza kwa mabango ya uongo yaliyopachikwa upatanishi, huku sisi wengine tukidhani lengo lao ni kudanganya watalii ili waone nchi sasa iko shwari.
Akiongea kwa uchungu, Lissu anadai yeye mwenyewe alitandikwa risasi na hadi leo hakuna yeyote aliyekamatwa. Anawezaje kupatanishwa na watu wa aina hiyo? Anadai sasa hivi anaitwa CHIBA kutokana na majeraha ya wauaji wake (kwa wasiolewa Chiba ni lugha ya mjini ikimaanisha mlemavu wa mguu).
Amezungumzia kupotezwa kwa watu wengi sana, akiwemo Ben Saanane, ambao hawajulikani walipo hadi leo, huku wenye madaraka au vyombo vya dola vikinyamaza. Anasema katika hali hii anawezaje kupatanishwa na waliokuwa madarakani, unyama huu ukitendwa? Na kwamba ambaye hayupo miongoni mwa watenda unyama huo ni mmoja tu, lakini wengine wote bado wapo. Hapa unapatanishwaje?
Lissu anadai Arusha ndio mkoa unaoongoza kwa mabango ya uongo yaliyopachikwa upatanishi, huku sisi wengine tukidhani lengo lao ni kudanganya watalii ili waone nchi sasa iko shwari.