Tumaini Makene
JF-Expert Member
- Jan 6, 2012
- 2,642
- 6,071
Wakuu
Labda leo naweza kuendelea kuandika tena kama namna yangu ya kumuenzi Daudi Mwangosi. Maana kama ni kumuaga, kwa kweli nimekataa kumuaga. Nikimuaga, nitakuwa namumwaga. Sina sababu ya kumumwaga Mwangosi. Si mtu wa kumwagwa. Nimekataa kama ambavyo nimekuwa nikikataa kuwaaga wapiganaji wengi wa namna yake.
Kwani maisha ni nini? Maisha si mwili pekee. Wala maisha si kiwiliwili hiki kinachotembea. Ni zaidi ya hayo. Wapiganaji wa namna ya Mwangosi niliyekuwa nikimfahamu, huendelea kuishi hata baada ya miili yao kutoweka duniani. Ukisoma kale kakitabu kadogo lakini kazuri, Intellectual Versatility, hii inaelezwa kama moja ya sifa za wanazuoni. Kuishi baada ya mwili kufa. Natumaini wengi mnajua hili.
Leo nitaweza kuendelea kuandika kumuenzi, kwa sababu moja ya vitu vilivyokuwa vikinisumbua kabisa kichwani tangu siku ile baada ya mauaji ya mpiganaji Daudi, ilikuwa ni namna ambavyo waandishi wa habari na UMMA WA WATANZANIA, 'tulipuuza' moja ya masuala ya muhimu kabisa ambayo tulipaswa kuwa tumewa-task Jeshi la Polisi na serikali kwa ujumla, kutekeleza. Ni kuhusu vitendea kazi vya Daudi. Silaha zake muhimu, kamera na kompyuta. Viko wapi vitu hivi?
Mapema sana nikingali Iringa, nikichangia hapa jukwaani, niliuliza swali hili hili nikitumia maneno ya Kiingereza. Niliuliza wamevichukua kwa sababu gani? Viko wapi? Wanavifanyia nini? Naona wengi tulipitwa. Bado hatukuona umuhimu wake.
Nashukuru sana leo swali hili limepata nafasi ya kusikika dunia nzima kupitia maandamano ya wanahabari. Limehojiwa pale Jangwani (ingawa kwa kuchelewa, maana ni dhahiri halikuwa likikumbukwa).
Nimemsikia mpiganaji Malembeka katika maandamano makubwa pale Iringa, akipaza sauti kubwa sana kuifahamisha dunia juu ya vifaa hivyo kuwa mikononi mwa Jeshi la Polisi, huku akihoji kwa nini hawataki kuvitoa! Tunawataka polisi watoe vifaa hivyo vya Daudi, kamera na kompyuta. Namshukuru sana Malemebka kuwa amekumbuka kile ambacho tulikuwa tukijadili naye, siku moja ama mbili, baada ya mauaji yale yaliyofanywa na Jeshi la Polisi.
Labda watu hawaelewei kwa nini. Si ajabu ndiyo maana hata katika press conferences mbili ambazo nimehudhuria, hasa katika presentations za still pictures and moving pictures za matukio ya siku hiyo ya mauaji pale Nyololo, (Iringa na Dar es Salaam), pamoja na suala hilo la kamera na kompyuta kusisitizwa sana kuwa viko wapi, wanahabari waliohudhuria hawakuona kama ni suala muhimu.
Wakati akikutwa na mauaji yale ya kikatili, Daudi alikuwa yuko kazini. Alikuwa akichukua habari. Ukiangalia picha kama tatu hivi, zipo mbili zinamuonesha akiwa katika mapambano yake ya mwisho hapa duniani. Akipigania uhai. Amemkumbatia yule askari Mwampamba amuokoe kwenye mikono ya israili.
Unaweza kuona kamera iko mikononi mwake. Upande wa kuchukulia ukiwa umefunguliwa. Ameishikilia imara. Ndiyo maana alilalama kwa ujasiri "msiniue msiniue...niko kazini." Ima fa ima na kamera yake mikononi. Israili hawakumsikiliza. Mmoja akafanya kazi aliyoagizwa kufanya. Akamlipua Daudi. Akamsambaratisha na kukatisha uhai wa mpiganaji yule!
Sasa waweza kuona namna ambavyo Daudi alikufa akiwa kazini. Kamera yake ilikuwa kazini. Ilikuwa ikiendelea kuchukua habari. Ilikuwa ikirekodi. Hata kama katika hatua za mwisho sana za uhai wa Daudi hakuweza kurekodi kwa uzuri picha kadri alivyotaka, lakini kamera yake iliendelea kuwa kazini, ikimfanyia kazi ya kurekodi sauti yeye kutaka. Wakati yeye anapigania uhai, kamera yake ilikuwa ikimpigania 'apate' ushahidi. Iko wapi hiyo kamera?
Katika moja ya zile picha ambazo inahitaji ujasiri mkubwa kuziangalia mara mbili ili uweze kutambua kuwa ule ni mwili wa binadamu, pembeni kabisa mwa mkono wa kushoto wa Daudi (kulia kwako mtazamaji), unaweza kuona kitu fulani kikubwa, cheusi. Hilo ni begi la kompyuta (Laptop) ya Daudi! Nayo iko wapi?
Ukiendelea mbele kidogo, hapa utahitajika kuhoji mpaka notebook na kalamu za Daudi ziko wapi. Hizi ni silaha za mwandishi. Ziko wapi silaha za mpiganaji yule. Kama askari wanavyohoji silaha za wenzao wakiuwawa vitani, nasi tunahoji silaha za mwenzetu! Wamezichukua za nini? Wamezifanyia nini? Wameziweka wapi? Kwa nini...kwa nini...kwa nini!
Kwa ujasiri wake, uwezo wake na kuipenda kazi yake, kamera ile ilikuwa imechukua matukio ya muhimu sana kwa siku ile. Hasa baada ya polisi kuwa wameanzisha vurugu, wakaharibu mali za raia, wakapiga na kukamata watu waliokuwa wakifanya shughuli za chama chao pale kwenye Ofisi ya Kata ya CHADEMA, Nyololo.
Daudi alikuwa akichukua matukio kwa ukaribu sana. Maana tangu mapema, alikuwa ameikamia kweli kweli ile stori. Haki yake na wajibu wake.
Kama havina chochote cha maana, kwa nini waendelee kubaki navyo.
Sasa tunahoji, ziko wapi hizo silaha za Daudi?
Labda leo naweza kuendelea kuandika tena kama namna yangu ya kumuenzi Daudi Mwangosi. Maana kama ni kumuaga, kwa kweli nimekataa kumuaga. Nikimuaga, nitakuwa namumwaga. Sina sababu ya kumumwaga Mwangosi. Si mtu wa kumwagwa. Nimekataa kama ambavyo nimekuwa nikikataa kuwaaga wapiganaji wengi wa namna yake.
Kwani maisha ni nini? Maisha si mwili pekee. Wala maisha si kiwiliwili hiki kinachotembea. Ni zaidi ya hayo. Wapiganaji wa namna ya Mwangosi niliyekuwa nikimfahamu, huendelea kuishi hata baada ya miili yao kutoweka duniani. Ukisoma kale kakitabu kadogo lakini kazuri, Intellectual Versatility, hii inaelezwa kama moja ya sifa za wanazuoni. Kuishi baada ya mwili kufa. Natumaini wengi mnajua hili.
Leo nitaweza kuendelea kuandika kumuenzi, kwa sababu moja ya vitu vilivyokuwa vikinisumbua kabisa kichwani tangu siku ile baada ya mauaji ya mpiganaji Daudi, ilikuwa ni namna ambavyo waandishi wa habari na UMMA WA WATANZANIA, 'tulipuuza' moja ya masuala ya muhimu kabisa ambayo tulipaswa kuwa tumewa-task Jeshi la Polisi na serikali kwa ujumla, kutekeleza. Ni kuhusu vitendea kazi vya Daudi. Silaha zake muhimu, kamera na kompyuta. Viko wapi vitu hivi?
Mapema sana nikingali Iringa, nikichangia hapa jukwaani, niliuliza swali hili hili nikitumia maneno ya Kiingereza. Niliuliza wamevichukua kwa sababu gani? Viko wapi? Wanavifanyia nini? Naona wengi tulipitwa. Bado hatukuona umuhimu wake.
Nashukuru sana leo swali hili limepata nafasi ya kusikika dunia nzima kupitia maandamano ya wanahabari. Limehojiwa pale Jangwani (ingawa kwa kuchelewa, maana ni dhahiri halikuwa likikumbukwa).
Nimemsikia mpiganaji Malembeka katika maandamano makubwa pale Iringa, akipaza sauti kubwa sana kuifahamisha dunia juu ya vifaa hivyo kuwa mikononi mwa Jeshi la Polisi, huku akihoji kwa nini hawataki kuvitoa! Tunawataka polisi watoe vifaa hivyo vya Daudi, kamera na kompyuta. Namshukuru sana Malemebka kuwa amekumbuka kile ambacho tulikuwa tukijadili naye, siku moja ama mbili, baada ya mauaji yale yaliyofanywa na Jeshi la Polisi.
Labda watu hawaelewei kwa nini. Si ajabu ndiyo maana hata katika press conferences mbili ambazo nimehudhuria, hasa katika presentations za still pictures and moving pictures za matukio ya siku hiyo ya mauaji pale Nyololo, (Iringa na Dar es Salaam), pamoja na suala hilo la kamera na kompyuta kusisitizwa sana kuwa viko wapi, wanahabari waliohudhuria hawakuona kama ni suala muhimu.
Wakati akikutwa na mauaji yale ya kikatili, Daudi alikuwa yuko kazini. Alikuwa akichukua habari. Ukiangalia picha kama tatu hivi, zipo mbili zinamuonesha akiwa katika mapambano yake ya mwisho hapa duniani. Akipigania uhai. Amemkumbatia yule askari Mwampamba amuokoe kwenye mikono ya israili.
Unaweza kuona kamera iko mikononi mwake. Upande wa kuchukulia ukiwa umefunguliwa. Ameishikilia imara. Ndiyo maana alilalama kwa ujasiri "msiniue msiniue...niko kazini." Ima fa ima na kamera yake mikononi. Israili hawakumsikiliza. Mmoja akafanya kazi aliyoagizwa kufanya. Akamlipua Daudi. Akamsambaratisha na kukatisha uhai wa mpiganaji yule!
Sasa waweza kuona namna ambavyo Daudi alikufa akiwa kazini. Kamera yake ilikuwa kazini. Ilikuwa ikiendelea kuchukua habari. Ilikuwa ikirekodi. Hata kama katika hatua za mwisho sana za uhai wa Daudi hakuweza kurekodi kwa uzuri picha kadri alivyotaka, lakini kamera yake iliendelea kuwa kazini, ikimfanyia kazi ya kurekodi sauti yeye kutaka. Wakati yeye anapigania uhai, kamera yake ilikuwa ikimpigania 'apate' ushahidi. Iko wapi hiyo kamera?
Katika moja ya zile picha ambazo inahitaji ujasiri mkubwa kuziangalia mara mbili ili uweze kutambua kuwa ule ni mwili wa binadamu, pembeni kabisa mwa mkono wa kushoto wa Daudi (kulia kwako mtazamaji), unaweza kuona kitu fulani kikubwa, cheusi. Hilo ni begi la kompyuta (Laptop) ya Daudi! Nayo iko wapi?
Ukiendelea mbele kidogo, hapa utahitajika kuhoji mpaka notebook na kalamu za Daudi ziko wapi. Hizi ni silaha za mwandishi. Ziko wapi silaha za mpiganaji yule. Kama askari wanavyohoji silaha za wenzao wakiuwawa vitani, nasi tunahoji silaha za mwenzetu! Wamezichukua za nini? Wamezifanyia nini? Wameziweka wapi? Kwa nini...kwa nini...kwa nini!
Kwa ujasiri wake, uwezo wake na kuipenda kazi yake, kamera ile ilikuwa imechukua matukio ya muhimu sana kwa siku ile. Hasa baada ya polisi kuwa wameanzisha vurugu, wakaharibu mali za raia, wakapiga na kukamata watu waliokuwa wakifanya shughuli za chama chao pale kwenye Ofisi ya Kata ya CHADEMA, Nyololo.
Daudi alikuwa akichukua matukio kwa ukaribu sana. Maana tangu mapema, alikuwa ameikamia kweli kweli ile stori. Haki yake na wajibu wake.
Kama havina chochote cha maana, kwa nini waendelee kubaki navyo.
Sasa tunahoji, ziko wapi hizo silaha za Daudi?