Mnawakumbuka watuma salamu maarufu redioni wa enzi hizo? Tujikumbushe kwa kuwataja...

Nyembo Juma Nyembo
Wesu Mbuzi
Duncan Mwapagata
Nuru Mtoto
Hussein Makabyureta
Hawa Hassan Kilongo
Exaud Annael Nnko
Exaud Makyao
Mbekai Ali Mbekai
Juma ramazan kamage.
Samwaja wa samwaja.
Damas rufinde nyingo.
Ali mbondei.
Romanus ishengoma.
Zamlatha Jongo.
 
Victor Mselabuye huyu hadi bbc utamsikia,kinachonishangaza hawa majamaa wanawezaje kushiriki kwenye vipindi tofauti tena kwenye redio tofauti todauti

Muhiri Obaree hili jina lilikuwa linanifurahisha sana na vituko vyake vya namna ya kuitikia anapoitwa na mtangazaji

Ugali Sokwe aliwahi kutokea kwa kipindi kifupi ila nae alisumbua sana
 
Duu, umenikumbusha mbali,
Enzi hizo miaka ya mwanzo ya 90, nilikuwa na rafiki wa karibu, mtangazaji RTD, alinihadithia mambo mengi.
Siku hizo mshahara wa Mtangazaji RTD akianza kazi ilikuwa ni Shilingi,
3,660.65.
Kikombe cha chai ya maziwa canteen yao pale Pugu Rd. ilikuwa Sh. 20, chapati, 20, andazi 10, mayai mawili ya kukaanga 40. Kipande cha kuku wa kukaanga ni sh.60.

Hao mabingwa wa salamu, walikuwa kila ukisoma kadi yake, kuna mahali unapita, anakupiga na Sh. 100. ukimaliza kipindi cha salaam, ukishuka canteen, hiyo 100, unapata chai, chapati 2 na mayai mawili ya kukaanga, kipande cha kuku na soda juu.

Jioni ukipita maeneo fulani, sio vi offer vinafululuza, akina dada ndio usiseme, enzi hizo redio yenyewe ilikuwa moja.

Hawa mabingwa wa salamu, ndio walikuwa wakiongoza kumwaga hizo 100, wakifuatiwa na wanamuziki wanaotaka nyimbo zao zipigwe, hawa walikata fungu kubwa zaidi,

Enzi hizo, Mghanii wetu akiwa 'Mzee Athumani Khalfani' akilipwa Sh.100 kughani kipindi cha nusu saa.

Jameni watu wametoka mbali!. Wee acha tuu!.
Mungu awarehemu watangazaji wote waliotangulia, na walibakia mpaka sasa, wapewe pongezi nyingi, na hata wazuri waliochipukia na wanaoendelea kuchipukia pia pongezi, ukiondoa wale wachache wana vamia fani.
Hapo kwenye "Mghani" nadhani ni kipindi kile cha mashairi nilikuaa nakipenda saaana mtangazaji alikua Bwana Said Nyoka
Huyooo Mzee wa kughani alikua anajua saaaaaanaaa Enzi za RTD hizoo
 
Enzi za RTD nawakumbuka
Wajadi fundi Wajadi binadam mashaka
Damas Lusinde nyingo
Nuru Msenga au Taaaajiri wa Rohooo
Hapo mtangazaji wa chagua la msikilizaji ni Bwana Malima Ndereeeeeeeeeema
alikua na Mbweembwe saaaaana
 
Kulikuwa na "mabingwa wa salamu" ambao walikuwa hawakosekani aidha kutuma salamu au kutumiwa salamu kwenye vipindi mbalimbali vya radio. Unayakumbuka majina yao?
Chivalavala S. Chivalavala
Aliishi Mwenge Dar.

Chesko mzee wa Matunda alikuwa kona ya Africa Sana....
 
Thobias Mnyani wa uhuru na msimbazi. Rashid nguruwe wa korogwe.Bingwa wa salam tanzania alikuwa Zakaria Ndemfoo,radio zote za kiswahili kuanzia germany,south africa nk lazima utamsikia- Aliwahi kusema asiposikia jina lake redioni hupungua nusu kilo
Alianza kutuma salam anzia late 1960's/1970s...kwenye idhaa za kiswahili ziliokuwepo.Huyu alikua bingwa kweli kweli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom