Nothing4good
Senior Member
- Feb 19, 2011
- 180
- 55
Wandugu naomba msaada. Mimi nina mchumba wangu tuko katika mchakato wa harusi. Alishanitambulisha kwao na nikakubalika.
Mimi ninaishi na mamdogo. Mamdogo ndiye aliyenilea so ni kama mamangu kwahiyo nilimpeleka mchumba wangu kwanza kwa mamdogo kumtambulisha kabila ya hatua nyingine na mamdogo ndiye aliyewaambia ndugu zangu wengine na akasema kuwa atagharamia kichen party na send off kwa kuwa mimi ni kama mtoto wake.
Ndugu zangu karibu wote wanamjua huyo kijana, sasa cha ajabu mamdogo ameanza kunikatisha tamaa. Ananiambia mbona huyo mwenzako anaoneka hajatulia? Ni mzuri tu wa sura hana kingine hakufai mwanangu. Tafuta mwingine mbona wanaume wako wengi? Na maneno mengine mengine kibao.
Mimi nikamjibu nampenda hivyo hivyo alivyo mamdogo. Baada ya kuona sielekei kumwacha akaanza kumwaga upupu kwa ndugu zangu wote kwamba yule kaka hanifai. Ndugu zangu wakaanza kumchukia huyu kijana. Cha kushangaza naona mamdogo yuko karibu sana na mchumba wangu nikimuuliza anasema wanashughulikia mambo ya ndoa yetu.
Siku moja mawifi zangu (ukweni) wakaniita na kuniuliza hivi huyo ni mamdogo wako kabisa? Nikawajibu ndio; yeye na mamangu ni wa tumbo moja. Walishangaa na kusema mbona sasa anafanya mambo ya ajabu vile? Nikawauliza mambo gani hayo wakasema nisubiri niolewe kwanza ndo wataniambia sababu wanaogopa kuuvunja uhusiano wetu(mimi na kaka yao).
Katika chunguza yangu nimegundua mamdogo ananichukulia mchumba wangu. Nimuachie mchumba wangu au nifanyeje??
Mimi ninaishi na mamdogo. Mamdogo ndiye aliyenilea so ni kama mamangu kwahiyo nilimpeleka mchumba wangu kwanza kwa mamdogo kumtambulisha kabila ya hatua nyingine na mamdogo ndiye aliyewaambia ndugu zangu wengine na akasema kuwa atagharamia kichen party na send off kwa kuwa mimi ni kama mtoto wake.
Ndugu zangu karibu wote wanamjua huyo kijana, sasa cha ajabu mamdogo ameanza kunikatisha tamaa. Ananiambia mbona huyo mwenzako anaoneka hajatulia? Ni mzuri tu wa sura hana kingine hakufai mwanangu. Tafuta mwingine mbona wanaume wako wengi? Na maneno mengine mengine kibao.
Mimi nikamjibu nampenda hivyo hivyo alivyo mamdogo. Baada ya kuona sielekei kumwacha akaanza kumwaga upupu kwa ndugu zangu wote kwamba yule kaka hanifai. Ndugu zangu wakaanza kumchukia huyu kijana. Cha kushangaza naona mamdogo yuko karibu sana na mchumba wangu nikimuuliza anasema wanashughulikia mambo ya ndoa yetu.
Siku moja mawifi zangu (ukweni) wakaniita na kuniuliza hivi huyo ni mamdogo wako kabisa? Nikawajibu ndio; yeye na mamangu ni wa tumbo moja. Walishangaa na kusema mbona sasa anafanya mambo ya ajabu vile? Nikawauliza mambo gani hayo wakasema nisubiri niolewe kwanza ndo wataniambia sababu wanaogopa kuuvunja uhusiano wetu(mimi na kaka yao).
Katika chunguza yangu nimegundua mamdogo ananichukulia mchumba wangu. Nimuachie mchumba wangu au nifanyeje??