Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Mlimani wapinga JK kuunda Tume ya Katiba
na Tutindaga Mwakalonge
VUGUVUGU la madai ya Katiba mpya limechukua sura mpya baada ya uongozi wa serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani (DARUSO) kumpa siku saba Rais Jakaya Kikwete awe amebadili msimamo wake wa kuunda Tume ya Katiba na atangaze kuliacha suala hilo mikononi mwa wananchi.
Mwenyekiti wa wanaharakati wa serikali ya wanafunzi chuoni hapo, Rich Mwita, alisema wanamtaka Rais Kikwete atangaze kuliacha suala la kuandikwa kwa Katiba mpya mikononi mwa wananchi ambao kupitia mwongozo utakaotolewa na Bunge ndio waamue aina ya Katiba inayotakiwa.
Tunataka rais achomoe wazo lake la kuunda tume. Hatutaki yeye atuundie tume ya Katiba, tunatoa siku saba atangaze kuliacha suala la Katiba mikononi mwa Bunge maana ndicho chombo cha wananchi. Tunataka mchakato mzima wa kuandikwa Katiba mpya ushirikishe jamii na si wanasheria au kamati itakayoundwa na Rais. Asipofanya hivyo tutashinikiza kwa maandamano na mgomo. Suala la Katiba linatugusa sana, alisema Mwita.
Sanjari na shinikizo hilo kwa rais, dai la pili la wanaharakati hao wa Daruso ni kutaka Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani, pamoja na Mwanasheria Mkuu, Frederick Werema, kujiuzulu haraka iwezekanavyo kwani walitoa misimamo inayohujumu matakwa ya umma kuhusu Katiba huku kauli zao zikidaiwa kukinzana na kile alichokisema Rais Kikwete mwenyewe.
Daruso pia imempa siku saba Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, kuonana na wanafunzi chuoni hapo vinginevyo watafanya mgomo kushinikiza kupatiwa ufumbuzi wa matatizo yanayowakabili.
Waziri Mkuu wa Daruso, Makuli Paul, alisema wanataka Dk. Kawambwa afike chuoni hapo ili kutambua matatizo yanayowakabili wanafunzi hao ikiwa na kuendelea kupewa fedha kidogo ya kujikimu (boom) isiyolingana na gharama za maisha ambazo zimepanda.
Alisema ukosefu wa madarasa pamoja na viti huwalazimu baadhi ya wanafunzi chuoni hapo kusimama nje ya madarasa wakati wa vipindi hali inayowafanya wazagae nje badala ya kupata mafunzo.
Kumekuwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya kulala (mabweni) chuoni hapo hivyo kusababisha baadhi ya wanafunzi kulala katika korido za vyumba. Hii inahatarisha afya zetu na hakuna jitihada zozote zilizofanywa na uongozi wa chuo na yote haya yanatokana na idadi kubwa ya wanafunzi waliodahiliwa, alisema Paul.
Daruso imemtaka waziri huyo kwa mamlaka aliyopewa kuwarudishia miradi mbalimbali iliyofutwa hapo awali wakati wa uongozi wa serikali iliyopita ambayo ilijulikana kama DUSO na kuifufua tena.
Aliitaja miradi hiyo kuwa ni mgahawa ambao ulikuwa chini ya serikali ya wanafunzi, baa pamoja na steshenari, miradi ambayo iliwasaidia wanafunzi chuoni hapo.
Aidha, alisema Daruso imemwandikia barua rasmi mbunge wa jimbo la Ubungo John Mnyika pamoja na mkuu wa wilaya ili walipatie ufumbuzi tatizo la kutokea ajali katika barabara ya Mandela eneo la Mabibo Hostel kwani wanafunzi wamekuwa wakipoteza maisha yao mara kwa mara.
na Tutindaga Mwakalonge
Mwenyekiti wa wanaharakati wa serikali ya wanafunzi chuoni hapo, Rich Mwita, alisema wanamtaka Rais Kikwete atangaze kuliacha suala la kuandikwa kwa Katiba mpya mikononi mwa wananchi ambao kupitia mwongozo utakaotolewa na Bunge ndio waamue aina ya Katiba inayotakiwa.
Tunataka rais achomoe wazo lake la kuunda tume. Hatutaki yeye atuundie tume ya Katiba, tunatoa siku saba atangaze kuliacha suala la Katiba mikononi mwa Bunge maana ndicho chombo cha wananchi. Tunataka mchakato mzima wa kuandikwa Katiba mpya ushirikishe jamii na si wanasheria au kamati itakayoundwa na Rais. Asipofanya hivyo tutashinikiza kwa maandamano na mgomo. Suala la Katiba linatugusa sana, alisema Mwita.
Sanjari na shinikizo hilo kwa rais, dai la pili la wanaharakati hao wa Daruso ni kutaka Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani, pamoja na Mwanasheria Mkuu, Frederick Werema, kujiuzulu haraka iwezekanavyo kwani walitoa misimamo inayohujumu matakwa ya umma kuhusu Katiba huku kauli zao zikidaiwa kukinzana na kile alichokisema Rais Kikwete mwenyewe.
Daruso pia imempa siku saba Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, kuonana na wanafunzi chuoni hapo vinginevyo watafanya mgomo kushinikiza kupatiwa ufumbuzi wa matatizo yanayowakabili.
Waziri Mkuu wa Daruso, Makuli Paul, alisema wanataka Dk. Kawambwa afike chuoni hapo ili kutambua matatizo yanayowakabili wanafunzi hao ikiwa na kuendelea kupewa fedha kidogo ya kujikimu (boom) isiyolingana na gharama za maisha ambazo zimepanda.
Alisema ukosefu wa madarasa pamoja na viti huwalazimu baadhi ya wanafunzi chuoni hapo kusimama nje ya madarasa wakati wa vipindi hali inayowafanya wazagae nje badala ya kupata mafunzo.
Kumekuwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya kulala (mabweni) chuoni hapo hivyo kusababisha baadhi ya wanafunzi kulala katika korido za vyumba. Hii inahatarisha afya zetu na hakuna jitihada zozote zilizofanywa na uongozi wa chuo na yote haya yanatokana na idadi kubwa ya wanafunzi waliodahiliwa, alisema Paul.
Daruso imemtaka waziri huyo kwa mamlaka aliyopewa kuwarudishia miradi mbalimbali iliyofutwa hapo awali wakati wa uongozi wa serikali iliyopita ambayo ilijulikana kama DUSO na kuifufua tena.
Aliitaja miradi hiyo kuwa ni mgahawa ambao ulikuwa chini ya serikali ya wanafunzi, baa pamoja na steshenari, miradi ambayo iliwasaidia wanafunzi chuoni hapo.
Aidha, alisema Daruso imemwandikia barua rasmi mbunge wa jimbo la Ubungo John Mnyika pamoja na mkuu wa wilaya ili walipatie ufumbuzi tatizo la kutokea ajali katika barabara ya Mandela eneo la Mabibo Hostel kwani wanafunzi wamekuwa wakipoteza maisha yao mara kwa mara.