sifi leo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2012
- 5,013
- 8,369
Ni sikitiko na masikitiko makubwa askari ambaye ana nyota moja yupo hapo barabarani akiwa amevalia kiraia na trafiki mmoja aliyevalia sare za kitrafiki, wanakamata magari yote yanayotoka Marangu Mwika, pamoja njia panda. Trafiki anasimamisha gari, hakagui gari, anachukua namba na leseni za madreva na kuwaagiza washushe abilia na kuwafata.
Kwa wenye cash wanatoa rushwa kesho kwa askari polisi mwenye nyota na kijana mmoja ambae nina imani nae ni askari polisi. Wasio na pesa wanaambiwa warudi hapo hapo walisha shusha abilia Ili wajisalimishe.
Hakuna gari inayokaguliwa, kila dreva anakaguliwa leseni basi, baada ya hapo unapewa kibano. Ni jambo la aibu askri polisi, afisa kabisa mwenye nyota moja kutongoza kundi la askari wasio na vyeo kwenda kufanya uhalifu.
Yote haya ni kwa sababu TAKUKURU mkoa wa Kilimanjaro, na hasa wilaya ya Moshi Vijijini hawatimizi wajibu wao ipasavyo. Hivi vitendo vya huyu askari sio leo wala jana walipunguza speed alipo wasema Kinana ila ni mwezi umeisha sasa upuuzi umerudi tena barabarani.
Angalizo mkuu wa kituo cha Himo, nina kusihi mkuu, Kilimanjaro hasa hapo. Sisi hatuwezi endelea kuona vijana wetu wanaonewa na askari wageni hao, wambie waache rushwa wafanye kazi kwa mujibu wa sheria. La sivyo tutalaumiana, hatuwezi ishi na mijizi inayo lipwa mshahara na tunao lipa mijizi iliyovaa gwanda ni sisi hapa.
Mimi dereva haice Mwika-Moshi, nimeandika kwa hasira sana.
Mkuu wa kituo ukitaka ushahidi nipo tayari maana hata picha nimepiga.
Kwa wenye cash wanatoa rushwa kesho kwa askari polisi mwenye nyota na kijana mmoja ambae nina imani nae ni askari polisi. Wasio na pesa wanaambiwa warudi hapo hapo walisha shusha abilia Ili wajisalimishe.
Hakuna gari inayokaguliwa, kila dreva anakaguliwa leseni basi, baada ya hapo unapewa kibano. Ni jambo la aibu askri polisi, afisa kabisa mwenye nyota moja kutongoza kundi la askari wasio na vyeo kwenda kufanya uhalifu.
Yote haya ni kwa sababu TAKUKURU mkoa wa Kilimanjaro, na hasa wilaya ya Moshi Vijijini hawatimizi wajibu wao ipasavyo. Hivi vitendo vya huyu askari sio leo wala jana walipunguza speed alipo wasema Kinana ila ni mwezi umeisha sasa upuuzi umerudi tena barabarani.
Angalizo mkuu wa kituo cha Himo, nina kusihi mkuu, Kilimanjaro hasa hapo. Sisi hatuwezi endelea kuona vijana wetu wanaonewa na askari wageni hao, wambie waache rushwa wafanye kazi kwa mujibu wa sheria. La sivyo tutalaumiana, hatuwezi ishi na mijizi inayo lipwa mshahara na tunao lipa mijizi iliyovaa gwanda ni sisi hapa.
Mimi dereva haice Mwika-Moshi, nimeandika kwa hasira sana.
Mkuu wa kituo ukitaka ushahidi nipo tayari maana hata picha nimepiga.