bhageshi
JF-Expert Member
- Jul 24, 2010
- 264
- 101
Katika kushughurikia maswala yangu katika ofisi za umma na katika mabenki nimebaini kuwa baadhi ya wafanyakazi nilio wasikia wanatumia neno "MAMA" wakimaanisha mkuu wao wa kazi, awali ilinipa shida kuelewa ana maana gani katika ofisi fulani lakini baada ya kwenda ofisi nyingine nikakutana tena na msemo huo, nimefika mapokezi nikakutana na mfanyakazi wa kiume nakueleza shida yangu, naye akamuuliza mfanyakazi mwenzake wa kike eti "mama" yupo kuna mteja hapa anashida naye. sasa nikaanza kujiuliza kulikoni mbona mkuu wa ofisi akiwa mwanamme sijasikia akiitwa "BABA" badala yake wanatumia zaidi neno Boss au MKUU. Binafsi imenikera sana tena sana kwani kwangu mie mama ni mama tu na wala mtu mwingine hawezi vaa wasifu huo tena kwa mtu asiye hata na udamu na mama yangu. Au ndio ni aina fulani ya Rushwa ya unyenyekevu maofsini ili mtu kunufaika malupulupu kwa haraka. Nawaulizeni nanyi wanaJF kuitwa "mama" kwa kiongozi mwanamke maofsini je ni sawa kwenu?