Mkutano wa CCM wilaya ya Mpanda

mkuu tunashukuru kwa picha. Nappe hakawii kuja humu na IDs mchanganyiko kujitapa kwamba alijaza watu.!

Tuna subiri mkutano uanze, lakini hali ni mbaya, watu wachache sana, sijamuona hata naibu waziri mmoja, tusubiri, labada wao watatokea kwenye mkutano, lakini hapa kwenye mapokezi kwenye ofisi za ccm wilaya, sijawaona!!!!
 
...ndowano ya M4C imewakabaa koo...kheri warudi bungeni wakagonge meza...

kaka meza hazigongeki.....namuona Mwigulu bado yuko na staili yake ya skafu ya bendera ya taifa....sijui ni UZALENDO AU USHAMBA????
 
Watawaeleza nini wana Mpanda?
Au na wao watabaki kulalamika kama wapinzani?
 
Na mjinga mwigulu kaja kushangaa Mpanda na kujipendekeza na wajinga wenzake wakati jimboni kwake kunawaka moto!
 
Watawaeleza nini wana Mpanda?
Au na wao watabaki kulalamika kama wapinzani?

ni malalamiko tu kaka, hakuna jipya, nipo kwenye mkutano hapa...nape anaongea, angalia updates zangu hapo juu!!
 
Nape anafanya trip apate PER-DM, msimuaribie kibarua chake, akitoka hapo anaandika report ya utekelezaji anampelekea Dhaifu afarijike:playball:
 
Nami niko hapa eneo la tukio; ni kituko kama hiki ndio chama tawala; Ama kweli mwisho wa CCM sio 2015 bali ni sasa;
wana JF hapa kuna watu wachache mno tena waliovalishwa sare za kijani. tulivalia kiraia tunahesabika
 
Nami niko hapa eneo la tukio; ni kituko kama hiki ndio chama tawala; Ama kweli mwisho wa CCM sio 2015 bali ni sasa;
wana JF hapa kuna watu wachache mno tena waliovalishwa sare za kijani. tulivalia kiraia tunahesabika

Kumbe small boy upo mpanda....tutafutane bwana....nawajuza wadau ***** ambao unazungumzwa na hawa MAGAMBA.....
 
Ccm ni janga, chama la mabwepande! Hakuna jipya eti nepi anaagiza vyombo vya dola anamuacha muuaji mwigulu na gaidi!
 
Mwigulu Nchemba awe makini anapofunguwa mdomo wake otherwise atailetea serikali yake ya CCM kama ili iliyoletwa na Sophia Simba na Membe. Mwigulu anasema serikali ya Uingereza inaitumua CHADEMA kuleta ushoga nchini! Kama CHADEMA kuwa na urafiki na chama cha conservative ni tatizo, tuseme kuhusu serikali ya CCM inayopewa hela na serikali hiyo hiyo ya Uingereza chini ya chama cha Conservative? Nchemba anaweza kusema 25% ya bajeti ya serikali ya Tanzania inatoka wapi? Na serikali ya CCM wanapokea hela ili kueneza ushoga?
 
Wana wasi wasi gani nao ni wwtawala na wanafanya kazi zao why not just use tv Walibi Dar na kuwaacha Chadema kuingia mitaani huko wana jiamini?
 
Kamanda ahsante sana sana KWA KUSAIDIA SANA KUUTANGAZA MKUTANO WETU WA MPANDA, LAKINI PIA AHSANTE KWA KUHUDHURIA. UMEFANYA UZALENDO MKUBWA KWA CCM KWA KAZI NZURI YA KUUTANGAZA MKUTANO WETU.

ULIPOCHEMKA NI KIDOGO SANA HASA UNAPOJARIBU KUPOTOSHA UKWELI WA KILICHOTOKEA, SINA HAJA YA KUSEMA WALIOHUDHURIA WANAJUA KILICHOTOKEA NA VYOMBO VINGINE VITAROTI UKWELI, NA NDO ITAKUWA AIBU YAKO. KWA KIFUPI NAWASHUKURU SANA WANANCHI WA MPANDA KWA MAPENZI YAO MAKUBWA KWA CHAMA CHA MAPINDUZI.




OTE=STK ONE;4242679]Hadi sasa hakuna ambacho kinaendelea, pamoja na matangazo ya mbwembwe nyingi, lakini hadi hivi sasa hakuna chochote ambacho kinaendelea. Pamoja na madai kuwa kutakuwa na mawaziri watano, lakini tetesi zinasema kuwa hakuna mawaziri isipokuwa waziri magembe tu na manaibu wengine kama Malima, na Agrey Mwanry. Wengine ni makada wa chama kama Nape na Mwigulu.

View attachment 58857View attachment 58859View attachment 58860

Hizi ni baadhi ya picha na hali halisi katika ofisi za makao makuu ya ccm wilaya ya mpanda.

Nitaendelea kuwa UPDATES. ILA PICHA SIYO NZURI SANA KAMCHINA KANGU SIYO KAZURI!!!! TUVUMILIANE WADAU.

UP DATES.....!!!!!


Naona ofisi inaanza kuchangamka, na magari yanaanza kuingia, akina mama wanajiandaa na matarumbeta yanaanza kusikika. Bila shaka wageni watakuwa wanakaribia kuingia. Nitaendelea kuwajuza!!!!


UP DATES.....
naona jamaa ndiyo wanaingia hapa ofisi za ccm wilaya. Ngoja nichukue picha halafu nitawajuza mkutano ukianza....be patient please!!!!!!!


UP DATES....picha za waliofika kwenye mkutano wa ccm mpanda...


View attachment 58868 View attachment 58869
NAPE NA MWIGULU


UP DATES.....

Sikuwa hewani kwa muda kutokana na shamra shamra za maandamano kutoka ofisini kwenda kwenye viwanja vya KASHAULILI Ambako mkutano unafanyika....

sasa hivi NAPE Anaongea na kutoa shukrani. Watu siyo wengi kama ilivyotarajiwa....uwanja umepwaya sana....Nape anasema kidumu chama cha mapinduzi, watu hawamjibu.....anaanza majigambo...kuwa yeye ndiye msemaji wa chama bora cha ccm tz....

UP DATE......

Anaanza matusi ya reja reja....eti waliotoka bungeni wakati jk anahutubia walikuwa wapambe.....anazungumzia wakati cdm wanakwenda kumuona jk ikulu kwa ajili ya katiba mpya....

Ameanzisha nyimbo ya TANZANIA TANZANIA NAKUPENDA KWA MOYO WOTE......NAPE HUYO...

UP DATES.....

Anazungumzia mkutano wa jana wa Ndago na mauaji ya kijana wa ccm.....!!! Ameanza matusi...eti wabunge wa cdm akili zao hazina akili....anasema mkutano wa cdm ulikuwa wa wahuni na waliohutubiwa walikuwa magaidi na wahuni wasioitakia mema tz....ccm inalaani sana mauaji haya...anasema kwa kuwa wao wako madarakanik wanaagiza vyombo vyote vya ulinzi na amani viwashughulikie wote waliohusika......anamwagiza msajili wa vyama vya siasa akiangalie chama ambacho kinaleta fujo....ananukuuu biblian na kurani...habari ya mfalem suleimani na wale wana mama wawili wenye watoto na maamuzi ya mfalme suleima kuhusu maamuzi aliyoyachukua kuhusu yule mtoto ambaye alitaka kugawanywa......

UP DATES.....

Anatoa mfano wa Kenya...na uvunjifu wa amani wakati wa uchaguzi......wameanzisha nambari one ya Komba......




anaanza kuwatambulisha mawaziri na Mwigulu Nchemba.....!!!!

anamdharau dr slaa eti ni babu....kazi kweli leo...watu hawaongezeki....nitawarushia picha baadaye kidogo...!!!

UP DATESS.....
Mwigulu ameanza kuongea....anazungumzia kupanda kwa maisha na hali ngumu ya uchumi....anaanza kuchambua bajeti ya kambi rasmi ya upinzani bungeni.....


UP DATES......!!!
Ameanza matusi...anasema kuna siku wapinzani watakana jinsia zao....siyo matusi haya?????


UP DATES....
Anazungumzia upandaji wa maisha na sababu zake.....
1. anasema ni kupanda kwa gharama za mafuta eti kwa sababu kuna vita mashariki ya kati....
anasema kuwa hakuna mtu ambaye atakuwa kijana milele.....sijui hata anamaanisha nini!!!!!!
Anamtukana mbowe eti....mpigisha disco......!!!!
anazumzia UDOM....Eti asiyeona kuwa jakaya hajafanya chochote, hana akili!!!!

UP DATES....
anazungumzia habari za Mbowe na kuchukua gari la Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni....
anagusia habari za mbowe kumlipia mtoto wake chekechea mil 15.....
anasema kuwa hakuna hata kiongozi mmoja wa upinzania mwenye lengo la kuikomboa nchi hii.....!!!!

UP DATES.....
anazungumzia urafiki wa CDM na chama cha Cameroon...eti kwa kuwa Cameroon anataka ndoa za jinsia moja, anasema CDM wataleta ndoa za jinsia moja......

NAPE AMEZINGUA CAMPAIGN nyingine eti AHADI NI DENI....amempandisha J. Magembe...eti ataeleza utekelezaji wa ilani ya ccm kwenye maji.....anadai vigelegele kwa magembe....

Magembe anabisha hodi Katavi na anawaomba watu wanyooshe mikono juu kuonesha kama kweli wamemkaribisha.....anawasifia akina DHAIFU NA LIWALO NA LIWE.....

UP DATES....
akina mama hapa kando yangu wanasema hata jiwe likisimama kugombea dhidi ya JK katika jimbo la mpanda mjini, jiwe litashinda....nimefurahi sana...huku kwetu akina mama wanatupa raha kweli, wako againsta ccm kabisa....raha kweli....

UP DATES....
Magembe amepunguza bei ya maji kutoka kutoka 25 hadi 30.....anadai amepunguza, lakini akina mama hapa wananiambia bei ya maji ni shilingi 25 kwa ndoo...yeye kadai kuwa amepunguza hadi shilingi 30...jamani...kazi kweli sijui amepunguza au ameongeza....!!!

Up DATES....
Watu wanaanza kuondoka....hakuna cha maana ambacho kinaongelewa....hata mimi wanaanza kuniboa!!!!

UP DATES....
Amenza mzee wa wake za watu na smg...adam Malima....anasema Kikwete atakabidhi km 16000 za bara bara tz nzima....

UP DATES....
Watu wanaondoka.....anaongea sasa naibu waziri wa mifugo....sijui jamaa ni mmasai....kiswahili kigumu kweli kake...jamani watu wanazidi kuisha kwenye mkutano.....

View attachment 58871View attachment 58874 View attachment 58875

Hii ndiyo hali halisi, nape asije akaanza kujisifu...uwanjani watu ndiyo hawa...tena wanazidi kupungua kwa sababu hakuna ambacho wanaongea kikaeleweka.....aibu tupu....

UP DATES.....
Anaongea naibu waziri wa uchukunzi.....hali ni mbaya....jamani watu wanaisha uwanjani na mimi ni miongoni mwao....hakuna cha maana hapa, anasema watu watakuwa na masikio lakini hawataona.....sijui masikio yanaona siku hizi....bange hizi.....!!!!! Me naondoka...asanteni wote ambao mmenifuatilia tangu jana nilipotoa taarifa za mkutano hadi leo ambapo mkutano hauna mvuto wala mashiko...hakuna cha maana hapa TCHAOOOOOOOOOOOOOOO!!!!!!!!!!!!!!!!!!![/QUOTE]
 
Mkuu STK.
Naomba kujuzwa, Mwigulu hajafumaniwa tena huko, maana jamaa ana pepo la kufungua zipu...
 
Ccm hamna hoja mpo mpo tu.mnatumia mbinu za kila aina kujikomboa hamkubaliki au hamuamini...2015 is not much far.
 
Back
Top Bottom