MKE wa Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), amehojiwa na Taasisi ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za ufisadi.
Wakati mama huyo, Tina Chenge, akinaswa na kuhojiwa na TAKUKURU kwa rushwa, Chenge mwenyewe ambaye kwa muda mrefu amekuwa akitajwa ndani na nje ya chama chake kuhusika na kashfa ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE-System, alisafishwa na Rais Jakaya Kikwete kwamba hakuna rushwa katika ununuzi wa kifaa hicho.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata, zilisema kuwa Tina alihojiwa juzi na TAKUKURU na kisha kuachiwa huru wakati uchunguzi dhidi yake ukiendelea.
Haikuweza kujulikana mara moja endapo amehojiwa kuhusiana na vitendo vya rushwa vinavyoendelea kwenye uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo Chenge anawania au la.
Kukamatwa kwa mke wa kigogo huyo na hatimaye kuhojiwa na TAKUKURU, kulithibitishwa jana na Mkurugenzi wa taasisi hiyo nchini, Dk. Edward Hosea.
SOURCE: Tanzania Daima
Wakati mama huyo, Tina Chenge, akinaswa na kuhojiwa na TAKUKURU kwa rushwa, Chenge mwenyewe ambaye kwa muda mrefu amekuwa akitajwa ndani na nje ya chama chake kuhusika na kashfa ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE-System, alisafishwa na Rais Jakaya Kikwete kwamba hakuna rushwa katika ununuzi wa kifaa hicho.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata, zilisema kuwa Tina alihojiwa juzi na TAKUKURU na kisha kuachiwa huru wakati uchunguzi dhidi yake ukiendelea.
Haikuweza kujulikana mara moja endapo amehojiwa kuhusiana na vitendo vya rushwa vinavyoendelea kwenye uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo Chenge anawania au la.
Kukamatwa kwa mke wa kigogo huyo na hatimaye kuhojiwa na TAKUKURU, kulithibitishwa jana na Mkurugenzi wa taasisi hiyo nchini, Dk. Edward Hosea.
SOURCE: Tanzania Daima