Mke wa Chenge ahojiwa na TAKUKURU

TATOO

Senior Member
Jul 1, 2012
113
21
MKE wa Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), amehojiwa na Taasisi ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za ufisadi.

Wakati mama huyo, Tina Chenge, akinaswa na kuhojiwa na TAKUKURU kwa rushwa, Chenge mwenyewe ambaye kwa muda mrefu amekuwa akitajwa ndani na nje ya chama chake kuhusika na kashfa ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE-System, alisafishwa na Rais Jakaya Kikwete kwamba hakuna rushwa katika ununuzi wa kifaa hicho.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata, zilisema kuwa Tina alihojiwa juzi na TAKUKURU na kisha kuachiwa huru wakati uchunguzi dhidi yake ukiendelea.

Haikuweza kujulikana mara moja endapo amehojiwa kuhusiana na vitendo vya rushwa vinavyoendelea kwenye uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo Chenge anawania au la.

Kukamatwa kwa mke wa kigogo huyo na hatimaye kuhojiwa na TAKUKURU, kulithibitishwa jana na Mkurugenzi wa taasisi hiyo nchini, Dk. Edward Hosea.

SOURCE: Tanzania Daima
 
MKE wa Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM), amehojiwa na Taasisi ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za ufisadi.

Wakati mama huyo, Tina Chenge, akinaswa na kuhojiwa na TAKUKURU kwa rushwa, Chenge mwenyewe ambaye kwa muda mrefu amekuwa akitajwa ndani na nje ya chama chake kuhusika na kashfa ya ununuzi wa rada kutoka Kampuni ya BAE-System, alisafishwa na Rais Jakaya Kikwete kwamba hakuna rushwa katika ununuzi wa kifaa hicho.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata, zilisema kuwa Tina alihojiwa juzi na TAKUKURU na kisha kuachiwa huru wakati uchunguzi dhidi yake ukiendelea.

Haikuweza kujulikana mara moja endapo amehojiwa kuhusiana na vitendo vya rushwa vinavyoendelea kwenye uchaguzi wa ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo Chenge anawania au la.

Kukamatwa kwa mke wa kigogo huyo na hatimaye kuhojiwa na TAKUKURU, kulithibitishwa jana na Mkurugenzi wa taasisi hiyo nchini, Dk. Edward Hosea.

SOURCE: Tanzania Daima

Je siyo kwamba naye "alihusika" na mauaji ya wale "Madenti" wawili wa KIBAJAJ? Mumewe akaibeba kesi ili "KUPOTEZEA"
 
Kila siku wanahojiwa tu. Mbona hawahukumiwi na kutupwa gerezani!? Hii nchi ya ajabu sana, waiba kuku na vyupi kwenye Kamba ndio wanaotumikia vifungo huku hawa wahujumu uchumi na wauaji wanapeta ushuani. Muda utafika.
 
Baba na mama wala/watoa rushwa kwa mikono yao wanajenga familia ya rushwa. Si watoto tu hadi wajukuu na vitukuu wanarithishwa rushwa.
 
Maigizo yanaendelea, pigeni chini huu upuuzi unaitwa ccm tujue mbivu na mbichi, sasa hivi hamwezi kufanya lolote chama lao litawalinda km kawaida
 
nadhani sis watanzania ndo watu wa ajabu sana

Hapo umenena mkuu. Yote yanayotokea nchi hii-ubabe, dhuluma, uonevu, unyanyasaji n.k ni kwasababu watanzania tuko kama tulivyo. Wasingefanya ujinga wote huo tungeonekana si watu wa kuchezea
 
amehojiwa tu..kawaida..'anaisaidia polisi' si unajua..hana ksi, bongo ukiwa mkuu unahojiwa unaachiwa gazeti linauza basi
 
VWamemuhoji ili kama ilivyokuwa kwa "mchawi" chenge iwe na kwa mkewe, asafishwe!!!!!!

Hansad za bunge zilionyesha akifanya ulozi kwa kumwaga unga unga bungeni, ikatafsiriwa alikuwa anaweka ndumba!!!!!!
 
Back
Top Bottom