Mkazi Mtwara atishia gesi kutoonekana

I am not a superstitious, let me sign out for a while!!!
 
bibi nae anamikwala kama mchawi si apeleke maendeleo ya miujiza huko mtwara .?
 
Wana Mtwara wana hoja ya msingi na hakuna haja ya kuwapotoshosha.

Mimi naamini hivyo ni viini macho tu.
 
Katika hatua nyingine Kikongwe Somoe Issa (90) ambaye ni mkuu wa kaya ya Msimbati, kijiji ambachogesi asilia inavunwa ameionya Serikali kutoendelea na mpango wake wakusafirisha gesi kwenda Dar es Salaam na kwamba iwapo itapinga bomba hilo litasafirisha maji badala ya gesi.

Kikongwe huyo ambaye haoni wala kusikia alisema hayupo tayari kuona gesi hiyo ambayo imepatikana katika kijiji hicho ikiondoka mkoani Mtwara.

"Atakayejaribu kuondoa gesi hii kitakacho mkuta atakijua yeye mweyewe…ninasema gesi isiende kokote…iwapo atabisha inawezekana akasafirisha maji tu na isiwe gesi yenyewe"alisema bibi huyo kupitia kwa mkalimani wake Asha Hamis

Aliongeza kuwa,"mwaka walioanza kuchimba(2005) walifika hapa bila kubisha hodi, wanajua kilichowakuta…bomba lilikuwahaliendi chini wala kurudi juu…walinifuata hapa nikaenda kufanya tambiko"

SOURCE: MWANANCHI


Tuna shida ya maji hapa Dar, wacha tu maji yaje tutakunywa!
 
kweli chinga's hawataki gesi ije dar/bagamoyo aisee! mi simlaumu sana huyu mzee coz elimu yake ni ya kimila zaidi, na upeo wake ndipo hapo unaishia na waliomzunguka wengi wao ndo kama yeye. sasa anaposhindwa kujenga hoja gesi isiondoke mtwara unatarajia aseme nini zaidi ili sauti yake isikike kwa nguvu zaidi!
 
Ndio maana kuna Mfalme wa Nyuki, pia kulikuwa na mlinzi wa Rais kwa majeshi yasiyoonekana, na juzi juzi kuna wamejitokeza wasiosaza hata panya.....haya yametokea chini ya miaka 10 iliyopita.

Tanzania leo ina baadhi ya watu waliopaswa kuishi enzi za ujima tena wakiwa ktk minyororo. How pitiable!
 
Kama ni kweli hayo ayasemayo angeanza kujitibu yeye akaweza kuona na kuckia
 
Yale yale, uchawi, ushirikina, matambiko, uganga, ujinga......

Siamini katika hii mambo lakini nilifanya mazungumzo na watu waliokuwepo wakati utafiti umeanza nchi kavu 2005, wanadai kulifanyika tambiko na bibi mmoja kikongwe baada ya tatizo kujitokeza wakati wa utafiti....haya mambo yapo mkuu
 
katika hatua nyingine kikongwe somoe issa (90) ambaye ni mkuu wa kaya ya msimbati, kijiji ambachogesi asilia inavunwa ameionya serikali kutoendelea na mpango wake wakusafirisha gesi kwenda dar es salaam na kwamba iwapo itapinga bomba hilo litasafirisha maji badala ya gesi.

kikongwe huyo ambaye haoni wala kusikia alisema hayupo tayari kuona gesi hiyo ambayo imepatikana katika kijiji hicho ikiondoka mkoani mtwara.

“atakayejaribu kuondoa gesi hii kitakacho mkuta atakijua yeye mweyewe…ninasema gesi isiende kokote…iwapo atabisha inawezekana akasafirisha maji tu na isiwe gesi yenyewe”alisema bibi huyo kupitia kwa mkalimani wake asha hamis

aliongeza kuwa,“mwaka walioanza kuchimba(2005) walifika hapa bila kubisha hodi, wanajua kilichowakuta…bomba lilikuwahaliendi chini wala kurudi juu…walinifuata hapa nikaenda kufanya tambiko”

source: Mwananchi

haoni wala hasiki....sasa kajuaje hayo mambo.........jf siku hizi imekuwa kama sehemu ya udaka na umbeya tu...... Imepoteza sifa kabisa.... Mods topic kama hizi ni kuzitoa tu mana hazina ukweli bali ni umbeya tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom