Mkapa upo?Supervisor wa ujenzi U/Taifa anyongwa kwa ufisadi Tanzania!!!!!

yule supervisor wa kichina wa ujenzi wa uwanja wa taifa amenyongwa nchini china kwa ufisadi alioufanya tanzania.

Inshu iko hivi.
Huyu kibopa wakati anakuja na jopo lake alidakwa na mkulu mmoja wa wizara usika(jina kapuni)na kumshauli waichakachue ramani ili cheji ibaki waigawane na kwamba tanzania hakutakua na shida yoyote na hakuna atakaye uliza maana hakuna aliyeiona ramani zaidi ya watu wacheche ambao ndio watakao igawana chenji hiyo.huyu mchina baada ya kupewa info hizo akaona hapa ndio pakutokea kimaisha,akakubali kuichakachua ramani na kuipunguza kwa 50%,huku akiwa ameondoa maduka na viwanja vya mazoezi.

Siri yafichuka:
Wakati rais wa china akija kuuzindua uwanja huo alipitia kwenye wizara yake husika huko china ili kuipata ramani hiyo ili atakapo fika ajue anazindua uwanja wa namna gani.
Alipofika nchini siku ya uzinduzi alishangaa kuona uwanja anaokuja kuuzindua ni tofauti na ulio kwenye ramani,hauna maduka yaliyopo kwenye ramani na pia hauna viwanja vya mazoezi vya nje.alitaka kuahirisha uzinduzi lakini maofisa aliokua ameandamana nao walimpa hathali za kuahirisha zoezi ili kwamba wangeingia kwenye kashafa kimataifa na pengine kuhatalisha uchumi wake kupitia nyanja hizo.baada ya uzinduzi kukamilika alitoa amri ya kuondoka na fisadi huyo kurudi home ili akajieleze.

Baada ya mahakama za china kujilidhisha kwa ufisadi wake kwa pamoja zilimuhuku kunyongwa kwa kosa la kuhujumu uchumi!!!!!

weka source pleaseee nikaisome hukohuko ulikoitoa...otherwise hii ni hadithi kama hadithi zingine za alfu lela ulela
 
weka source pleaseee nikaisome hukohuko ulikoitoa...otherwise hii ni hadithi kama hadithi zingine za alfu lela ulela
Mkuu source ya kwanza ni copy ya ramani ya uwanja halisi uliostahili kujengwa ambayo sehemu na nnafuatilia kuipata,kwahiyo just be patient.
 
Hii ishu itakuwa kweli maana nakumbuka kabla uwanja haujajengwa nakumbuka nilisoma kwenye magazeti kuwa uwanja utazungukwa na maduka ya kisasa...! Nilipoona hakuna maduka nikajua ni mabadiliko tu ya ramani. kumbe watu wamepiga....
 
mmh....mbona huyu jamaa kanyongwa zamani sana??..ulikuwa wapi?
Mkuu mbona sasa hukuitupia humu ndani?mie nilizinyaka hizi nyuzi juzi but nikaona nizifanyie kazi kujilidhisha,na baada ya kupata ukweli nikaitupia hapa ndani ili tuidadavue.
 
Si mnaita kila bidhaa feki ni ya kichina wakati nyingine zinatengenezwa hapo kariakoo na wabongo wenyewe tu?haya sasa sijui huu uwanja nao mtasema wa "kichina" wakati umefanyiwa utaalamu "kibongo bongo" huku mchina akipewa darasa na mbongo!crazy Bongo!
 
Habari hii mimi siiamini. Kwanza imesikika muda mrefu sana kama uvumi, lakini hakuna ushahidi na mtiririko wa matukio ya kubumbuluka kwa dili hili yanachanganya sana. Yaani eti Raisi wa China akapitia wizarani. Huko aliikariri hiyo ramani au alikuja nayo huku kujiridhisha?

Inawezekana wizi ulifanyika, lakini tafadhalini hebu leteni habari kamili na vyanzo vyake kabla hatujaibeba.
 
Mojawapo ya ushahidi wa wazi wa uchakachuaji ni paa la uwanja. Kama kuna mvua basi ujue VIP seats ni zile za nauli ya chini kabisa!! Only in bongo.
 
Unless I read the original source of this news, it remains as ridiculous as Mwigulu's tapes !
 
Acha propaganda!
Mradi wa ujenzi wa uwanja wa Taifa wa mpya ulikua uambatane na kituo cha michezo mbali mbali, ambapo katika awamu ya kwanza ilikua ni ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu ambao umekamilika na awamu ya pili ilikua ni ujenzi wa viwanja vingine vya michezo kama indoor ya basketball, volleyball, table tenis, swiming pool, hotel na viwanja vingne vya mazoezi kikiwemo kiwanja cha sasa cha Uhuru.
Mhe Mkapa mpaka anaondoka alikua amekamilisha aslimia 90% hivyo ilipaswa rasi aliyefuata kukamilisha asilimia 10% ya ujenzi ya mradi huo.
cha ajabu mpaka leo mradi haujaendelezwa zaidi ya uwanja wa uhuru tu, kitu kinachopelekea kampuni ya BCCG kuedelea kuwepo eneo la taifa kusubiria kumalizia mradi huo.
 
Acha propaganda!
Mradi wa ujenzi wa uwanja wa Taifa wa mpya ulikua uambatane na kituo cha michezo mbali mbali, ambapo katika awamu ya kwanza ilikua ni ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu ambao umekamilika na awamu ya pili ilikua ni ujenzi wa viwanja vingine vya michezo kama indoor ya basketball, volleyball, table tenis, swiming pool, hotel na viwanja vingne vya mazoezi kikiwemo kiwanja cha sasa cha Uhuru.
Mhe Mkapa mpaka anaondoka alikua amekamilisha aslimia 90% hivyo ilipaswa rasi aliyefuata kukamilisha asilimia 10% ya ujenzi ya mradi huo.
cha ajabu mpaka leo mradi haujaendelezwa zaidi ya uwanja wa uhuru tu, kitu kinachopelekea kampuni ya BCCG kuedelea kuwepo eneo la taifa kusubiria kumalizia mradi huo.

Kujenga vitu vyote ivyo kwa eneo lipi unless kama walikuwa na plan ya kumega eneo la JKT na la DUCE!
Hii kitu wangieshusha CHANIKA UKO nashangaa viwanja viwili sehemu moja awazo ya KIJUHA KWELI HAYA
 
Kuna umuhimu wa kutupa uhakika wa habari hii. Ilivyokaa ni ngumu kuiamini haina facts nyingi. Unless muiweke kama tetesi maana hata jina la aliyenyongwa (kama ni kweli) hakuna. Mtu kama kahukumiwa kunyongwa jina lake sio siri tena, vyombo vya habari vimeshalidaka.
 
Back
Top Bottom