Mkakati wa Team Lowassa huu hapa

Kama hii habari ni ya kweli basi kuna watu wana raha jamani?Milioni 5 kwa siku?
Unashangaa hizo, mbona hushangai Zali all white party imeingiza sh. Ngapi kwa siku moja.
Hata hivyo pesa za wizi hazina idadi halafu haziumi.
Wana CCM wananunuliwa kama mafungu ya nyanya.
Hovyo kabisa.
 
Wakati vuguvugu la kuwasafirisha,kuwaandalia matamko ya kumsifu na kuwalipa baadhi ya makundi mbalimbali ya kijamii likijadiliwa ndani ya chama kwa hatua za kinidhamu,hali ya marafiki wa EL imekuja na mbinu mpya za kutafuta ushawishi wa nguvu ya pesa ndani ya chama.

Wajumbe wa NEC kutoka mikoa yote ya kanda ya Ziwa wamemiminika Dsm,kwa udhamini na ufadhili wa EL ili kutafuta uungwaji mkono kuelekea Octoba.Wajumbe hao wa NEC walianza kuwasili Dsm toka juzi usiku,wakipokewa na kuwekwa ktk hotel tofautitofauti ndani ya jiji..huku gharama za malazi,chakula,nauli na posho zikiwa chini ya EL.

Wajumbe hao kutoka ktk mikoa ya Mwanza,Geita,Simiyu,Shinyanga,Musoma na Kagera ujio wao umechagizwa na posho ya milioni tano kwa kila mtu,Na kikao kinaendelea na EL ili kutafuta ushawishi kwa wajumbe wa kanda ya ziwa.

Hali hii ya kuanza kuwasafirisha wajumbe kimyakimya na kwa makundi inakuja baada ya ile mbinu ya kuwatafuta watu wa makundi mbalimbali ndani ya nchi kuzuiwa na chama.Lafu hii ya kukiuka kanuni za chama kwa kuwasafirisha na kuwalipa kiasi kikubwa cha pesa wajumbe ni aina mpya ya mbinu ya Team EL baada ya ile ya kwanza kushitukiwa.

Kuelekea uchaguzi Mkuu,EL ameonekana kutumia kiasi kikubwa sana cha pesa ktk kulazimisha ushindi wa kuteuliwa na chama chake kuipeperusha bendera katikati ya vyama vingine vya upinzani hususani UKAWA.

Matumizi haya ya kiasi kikubwa cha pesa si tu ni tishio ndani ya chama chake na kwa mustakabali wa demokrasia safi,bali ni utamaduni unaotaka kupandikizwa ktk siasa za nchi hii kuwapata viongozi nje ya misingi ya uadilifu,nidhamu na uzalendo wa kweli.

Chanzo cha Taarifa hii ni mmoja kati ya wajumbe wa NEC walio ndani ya kikao hicho kinachoendelea sasa Kati ya EL,wapambe wake na wajumbe hao
Ora Et Labora

We ni ji joka una roho mbaya halafu unasema eti kikao na lowasa wakati lowasa mwenyewe yupo nje ya nchi.jinga sana wewe
 
Ulitakaamwage uppupu mpwaaa??kajipangaq nanyie jipangeni. Bilalowasaa nchi aitawaliki 2015

Nyie ndio kikundi cha wahuni wachache mnaonufaika na viongozi wa namna hii, ili wakiingia madarakani mzidi kujinufaisha, wa tz wa sasa wameshajua janja yenu, Endeleeni kula pesa zake tu lakini uraisi hawezi upata, Chonde chonde watanzania maskini tuungane dhidi ya hawa manyang'au wachache ambao wanataka kuhakikisha kuwa jambazi huyu anaingia madarakani. na endapo akifanikiwa tumekwishaaaa... Kwa ccm wote ni wale wale tu, na mwaka huu mnalo. KULA CCM, KULALA UKAWA,
 
Chabruma tupe siri za Zito na Lowasa.wewe ni mwenyekiti wa kamati ya usalama,tupe vitu vya ndani mkuu
 
We ni ji joka una roho mbaya halafu unasema eti kikao na lowasa wakati lowasa mwenyewe yupo nje ya nchi.jinga sana wewe
Kama hayupo Bashe yupo, Abubakar Lyongo, Mgeja,Mwenyekiti wa Arusha,Msindai na Mathayo wa Musoma.
Yeye anaugulia dripu kliniki wakati wapambe wanafanya fitina.
Mbona jana hakuwepo na bado wakatoa Mil.50 Zanzibar.
 
Huyu Fisadi anamwaga noti bila kuchoka, Nchi i Rushwa tupu.

Haya ndiyo maadili, utamaduni na maagizo ya ccm.
Hivi unasahau jinsi viongozi wa ccm walivyoingia madarakani. 2005 na 2010?
NI rushwa,rushwa.....
 
Wana-CCM na Watanzania kwa ujumla, wana haki na sababu ya kuhoji. Yako wapi matunda ya CCM makini ya Azimio la Arusha? Viwanda vya kila aina vidogo, vya kati na vikubwa (Machine Tools)!
Miundombinu lukuki ya maendeleo, dira sahihi ya maendeleo, usawa, umoja wa kitaifa na mshikamano? Hadhi, heshima na kutambuliwa kwa Mtanzania kimataifa kama mtu wa Taifa makini?Makatazo ya rushwa,uzembe na ubadhilifu?ziko wapi nguvu za mwenyekiti wa chama dhidi ya hujuma ndani ya chama chake?wakowapi viongozi wa juu wa ccm wakikodolea macho hadi mti umekuwa namna hii....Lowasa anafanya atakayo ndani na nje ya chama amevuruga kila jambo kwa masikitiko sana namkumbuka baba wa Taifa hili...Lazima niseme.

 
Wana-CCM na Watanzania kwa ujumla, wana haki na sababu ya kuhoji. Yako wapi matunda ya CCM makini ya Azimio la Arusha? Viwanda vya kila aina vidogo, vya kati na vikubwa (Machine Tools)!
Miundombinu lukuki ya maendeleo, dira sahihi ya maendeleo, usawa, umoja wa kitaifa na mshikamano? Hadhi, heshima na kutambuliwa kwa Mtanzania kimataifa kama mtu wa Taifa makini?Makatazo ya rushwa,uzembe na ubadhilifu?ziko wapi nguvu za mwenyekiti wa chama dhidi ya hujuma ndani ya chama chake?wakowapi viongozi wa juu wa ccm wakikodolea macho hadi mti umekuwa namna hii....Lowasa anafanya atakayo ndani na nje ya chama amevuruga kila jambo kwa masikitiko sana namkumbuka baba wa Taifa hili...Lazima niseme.

Wanamuogopa halafu wana mtii.
Si unaona jana amealikwa Zanzibar, na amewapa Mihela ya kutosha. Sasa nani atajaribu kumkosoa??
Tangu lini Mashetani yakafukuza Shetani mwenzao.
Chama hakitishi tena. Anaweza hata akagawa hadharani na bado wakamuita Jembe.
Poor CCM Leadership.
 
Lowassa anaonewa kwa kufungwa mdomo hata kuongea tu kwake ni dhambi. Hivi yaliyotokea zanzibar kwenye harambee haiwezi kuhesabika ni kampeni? Maana watangaza nia wameshindana kutoa day waziwazi. Aliyetoa nyingi atakuwa ameshinda. Wangepata haki wangewapagia wote kiasi cha kutoa kilicho sawa. Bora zaidi wasingewaomba kabisa kuchangia maana hii inaonekana kama kuwa omba 'ransom'.
 
Kama hayupo Bashe yupo, Abubakar Lyongo, Mgeja,Mwenyekiti wa Arusha,Msindai na Mathayo wa Musoma.
Yeye anaugulia dripu kliniki wakati wapambe wanafanya fitina.
Mbona jana hakuwepo na bado wakatoa Mil.50 Zanzibar.

Hivi humu kuna mijitu isojua kusomaee.hili jitu ni mojawapo pumbavu kabisa.mleta mada aya ya mwisho kasema kikao kinaendelea kati y EDO na wajumbe.ndipo nilipojua mleta mada muflisi wa fikra na wewe kumbe zezeta mwenzake.lo nenda kajifunze tena kusoma na kuandika
 
Tangu mwanzo wa sentensi hadi mwaisho, inaonyesha mwandishi ni muongo na hii hi habari ya kupikwa. Hakika mti wenye matunda ndio unaopigwa mawe. Hii ni dalili ya wazi kabisa kuwa huyu EL ndo rais mwenya matunda tamu kwa ajili ya taiafa hili. Huyu ndio pekee, ambae jina lake linawatisha wasioitakia maendeleo tanzania ndani ya ccm and ne yake.

hii tabia ya kutumia misemo ya maana kwenye mambo ya kipuuzi ni upumbavu.huu mti wenye matunda ndio lowasa? Hata chenge mlisema ni mti wenye matunda.wajinga nyie.
 
Kiwewe cha nini na ngoma bado?Mnaweweseka nini na mnadai mtashinda? Ushindi wa kwenye maforums ndio zenu sio uchaguzi halisi.
 
Shida nini sasa,watu tusikutane kisa nyie kambi zenu hamwezi kukutana?
 
Teteeteeeee....mleta uzi umewastukiza team EL...sina mbavu hapa! Yanavyochangia utazani wamefumaniwa.
 
Mi nawashanga Bashe na, Abubakar Lyongo . Bashe waandishi vibarua wanakaa zaidi ya miezi 3 pale mtanzania halafu na lyongo nae kule kwa bos wake subhash ambae yeye ni meneja mahusiano kuna vibarua mwaka wa 20 huu hawana mikataba. Hebu kwanza lekebisheni hayo ya chini yenu kabla ya kumnadi jamaa yenu.
 
Back
Top Bottom