Mkakati wa 'kuua' Red Brigade, huku Green Guard wakitamba huu hapa...

Crashwise

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
22,227
8,735
Hatimaye Serikali ya CCM imeamua kutumia wanasheria wa Serikali kushughulikia vijana wa CHADEMA wanaofanya mafunzo ya uzalendo na ukakamavu Kwa kutumia Sheria ya kikoloni iitwayo The Public Order Act ya Mwaka 1951 kuanzia leo.

Hatua ya kwanza ya kuhakikisha Red Brigade ya CHADEMA inashughulikiwa kisha kuwapatia mwanya vijana wa CCM kupitia Green Guard wafanye wanavyotaka, inaanzia rasmi leo mkoani Simiyu ambako vijana takriban 13 wa CHADEMA wanafikishwa mahakamani leo eti kushtakiwa kwa kosa la kufanya kazi au majukumu yanayofanana na polisi baada ya kukutwa uwanjani wakifanya mazoezi ya ukakamavu.

Hatua hiyo inafuatia maelekezo ya kikao kilichofanyika mkoani Morogoro ambapo maofisa wa serikali walipewa maagizo maalum ya kuhakikisha Red Brigade haiendelei na ifikapo wakati wa uchaguzi iwe 'imekufa' ili kutoa mwanya kwa CCM kupitia Green Guard kufanya wanavyotaka kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, kama ilivyo ada, wakishirikiana na baadhi ya watumishi kwenye Vyombo vya dola.

Katika kikao cha Kamati Kuu ya CCM iliyokutana Zanzibar hivi karibuni suala la mafunzo ya uzalendo na ukakamavu Kwa vijana wa CHADEMA liliibua mjadala ambapo walikubaliana kuwa wakiiacha Red Brigade ikaendelea kuimarika CCM itakuwa kwenye wakati mgumu wa kufanya hujuma wakati wa uchaguzi. Kwa hiyo ikakubaliwa lazima kuwepo mikakati ya kuizuia.

Mkakati wa kwanza ulikuwa ni kutumia ziara za akina Nape na Kinana mikoani kusema maneno majukwaani kuwa Red Brigade eti ni ugaidi na uhaini. Ndiyo maneno aliyoyasema Nape akiwa mkoani Dodoma, Kongwa.

Maneno hayo yalikuwa ni code words kwa ajili ya Vyombo vya dola kuchukia hatua lakini bahati mbaya baadhi ya watu serikalini na katika Vyombo hivyo ambao ni wapenda haki walihoji na kusema iwapo CCM inataka Red Brigade isiwe

wakaenda mbali na kuwaambia CCM kuwa Green Guard ndiyo imekuwa kikundi kinachotishia amani na kusababisha vurugu, utekaji nyara, mateso na mauaji wakati wa uchaguzi na kufanya hujuma zingine mbalimbali hata kwenye vituo vya kupigia kura kwa ajili ya kuiba kura.

Baada ya mkakati huo wa kutumia code words za ugaidi na uhaini kwenye mikutano ya hadhara ili eti vyombo vya dola vichukue hatua za makosa ya ugaidi na uhaini kushindikana, ndiyo sasa imetafutwa njia nyingine...

Maofisa kadhaa wa Serikali wakaitwa Morogoro kwa ajili ya jambo moja tu; Red Brigade ambako ndiyo ikakubaliwa kuwa Sheria ya The Public Order Act itumike 'kuwashughulikia' vijana wa CHADEMA ili kuwatisha wasiendelee na Red Brigade.

Baada ya hapo ndiyo vijana wa CHADEMA wakakamatwa huko Bariadi wakiwa katika mafunzo ya uzalendo ambapo walipofikishwa kituoni walipewa kesi ya tuhuma za Unlawful Assembly...kisha wakapewa dhamana na kuondoka kituoni hapo.

Lakini punde tu baada ya vijana hao kutoka kituoni hapo, wakakamatwa tena na kuwekwa ndani kwa kosa lingine.

Leo ndiyo wanafikishwa Mahakamani wakishtakiwa kufanya kazi zinazofanana na majukumu ya polisi.

Huu sasa ndiyo umeamriwa uwe mkakati wa kuzuia Red Brigade utakaotumika kuhakikisha haiendelei nchi nzima baada ya CCM kuona wazi kuwa haitapata mwanya wa kufanya hujuma dhidi ya CHADEMA, viongozi wake na mali za chama hicho kama ambavyo imekuwa ikifanyika Kwenye kila uchaguzi.

Wakati kesi hiyo ikianza leo, hakuna kesi hata moja ambayo inaendelea mahakama yoyote ya Tanzania kuhusu vitendo vya kihalifu vya kikosi cha ulinzi cha CCM, Green Guard, ambapo ushahidi upo wazi namna ambavyo wamekuwa wakipewa mafunzo Kwenye makambi ya siri, huku pia wakifanya shows za kijeshi mchana hadharani na Mkuu wa Nchi akipita akikagua magwaride yao.

Imetolewa na mkuu wa habari Chadema
Tumaini Makene
 
Hatimaye Serikali ya CCM imeamua kutumia wanasheria wa Serikali kushughulikia vijana wa CHADEMA wanaofanya mafunzo ya uzalendo na ukakamavu Kwa kutumia Sheria ya kikoloni iitwayo The Public Order Act ya Mwaka 1951 kuanzia leo.

Hatua ya kwanza ya kuhakikisha Red Brigade ya CHADEMA inashughulikiwa kisha kuwapatia mwanya vijana wa CCM kupitia Green Guard wafanye wanavyotaka, inaanzia rasmi leo mkoani Simiyu ambako vijana takriban 13 wa CHADEMA wanafikishwa mahakamani leo eti kushtakiwa kwa kosa la kufanya kazi au majukumu yanayofanana na polisi baada ya kukutwa uwanjani wakifanya mazoezi ya ukakamavu.

Hatua hiyo inafuatia maelekezo ya kikao kilichofanyika mkoani Morogoro ambapo maofisa wa serikali walipewa maagizo maalum ya kuhakikisha Red Brigade haiendelei na ifikapo wakati wa uchaguzi iwe 'imekufa' ili kutoa mwanya kwa CCM kupitia Green Guard kufanya wanavyotaka kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, kama ilivyo ada, wakishirikiana na baadhi ya watumishi kwenye Vyombo vya dola.

Katika kikao cha Kamati Kuu ya CCM iliyokutana Zanzibar hivi karibuni suala la mafunzo ya uzalendo na ukakamavu Kwa vijana wa CHADEMA liliibua mjadala ambapo walikubaliana kuwa wakiiacha Red Brigade ikaendelea kuimarika CCM itakuwa kwenye wakati mgumu wa kufanya hujuma wakati wa uchaguzi. Kwa hiyo ikakubaliwa lazima kuwepo mikakati ya kuizuia.

Mkakati wa kwanza ulikuwa ni kutumia ziara za akina Nape na Kinana mikoani kusema maneno majukwaani kuwa Red Brigade eti ni ugaidi na uhaini. Ndiyo maneno aliyoyasema Nape akiwa mkoani Dodoma, Kongwa.

Maneno hayo yalikuwa ni code words kwa ajili ya Vyombo vya dola kuchukia hatua lakini bahati mbaya baadhi ya watu serikalini na katika Vyombo hivyo ambao ni wapenda haki walihoji na kusema iwapo CCM inataka Red Brigade isiwe

wakaenda mbali na kuwaambia CCM kuwa Green Guard ndiyo imekuwa kikundi kinachotishia amani na kusababisha vurugu, utekaji nyara, mateso na mauaji wakati wa uchaguzi na kufanya hujuma zingine mbalimbali hata kwenye vituo vya kupigia kura kwa ajili ya kuiba kura.

Baada ya mkakati huo wa kutumia code words za ugaidi na uhaini kwenye mikutano ya hadhara ili eti vyombo vya dola vichukue hatua za makosa ya ugaidi na uhaini kushindikana, ndiyo sasa imetafutwa njia nyingine...

Maofisa kadhaa wa Serikali wakaitwa Morogoro kwa ajili ya jambo moja tu; Red Brigade ambako ndiyo ikakubaliwa kuwa Sheria ya The Public Order Act itumike 'kuwashughulikia' vijana wa CHADEMA ili kuwatisha wasiendelee na Red Brigade.

Baada ya hapo ndiyo vijana wa CHADEMA wakakamatwa huko Bariadi wakiwa katika mafunzo ya uzalendo ambapo walipofikishwa kituoni walipewa kesi ya tuhuma za Unlawful Assembly...kisha wakapewa dhamana na kuondoka kituoni hapo.

Lakini punde tu baada ya vijana hao kutoka kituoni hapo, wakakamatwa tena na kuwekwa ndani kwa kosa lingine.

Leo ndiyo wanafikishwa Mahakamani wakishtakiwa kufanya kazi zinazofanana na majukumu ya polisi.

Huu sasa ndiyo umeamriwa uwe mkakati wa kuzuia Red Brigade utakaotumika kuhakikisha haiendelei nchi nzima baada ya CCM kuona wazi kuwa haitapata mwanya wa kufanya hujuma dhidi ya CHADEMA, viongozi wake na mali za chama hicho kama ambavyo imekuwa ikifanyika Kwenye kila uchaguzi.

Wakati kesi hiyo ikianza leo, hakuna kesi hata moja ambayo inaendelea mahakama yoyote ya Tanzania kuhusu vitendo vya kihalifu vya kikosi cha ulinzi cha CCM, Green Guard, ambapo ushahidi upo wazi namna ambavyo wamekuwa wakipewa mafunzo Kwenye makambi ya siri, huku pia wakifanya shows za kijeshi mchana hadharani na Mkuu wa Nchi akipita akikagua magwaride yao.
Makamanda hakuna tutakachopewa mkononi,tuko tayari kumshinda adui.Hakuna kesi hapo.Na hiyo kesi tutashinda kwa sababu tunaaza na MUNGU na kumaliza na MUNGU
 
Huu mpango kamwe hawatafanikiwa.Waovwana Ibilisi na Chadema tuna Mungu
 
Hili sasa malizeni tu kimyakimya maana tulisema hapa suluhu ya kudumu ni kukomesha makundi pande zote sababu hayana sababu ya kuwepo wala ulazima wa kuanzishwa. . . . . .

Mkaona njia bora nanyi ni kuanzisha lenu basing on same wrong premises za waliotangulia. . ..

Two wrongs. . . ..
 
Huu mpango kamwe hawatafanikiwa.Waovwana Ibilisi na Chadema tuna Mungu

Watu wanaenda mahakamani we unaleta habari ya Paulo na Sila. . . . . .wasije kufungwa vijana wa watu. . . . .Hivi nyie maarufu wa humu mlishapitia mafunzo haya ya ukakamavu???!??
 
penye changamoto nyingi NDIPO penye mAfanikio makubwa hakika tuashinda. Twatakiwa kujizatiti
 
Ninaona serikali imeingia rasmi vitani:-

1. Vita kati ya serikali na vyama vya upinzani (vikipiganwa kutumia wanasheria wa srikali na majeshi ya ulinzi na usalama huku upande wa pili kukiwa na nguvu ya umma ikiwakilishwa na raia wasio na silaha, raslimali wala uwakilishi serikalini)
a
2. Vita kati ya srikali na wasio waislam (vikipiganwa na kikwete, pinda, kova, membe na waislam wachache huku upande wa pili ukisimamiwa na Mungu anayejulikana kama "Mtu wa Vita na Bwana ndilo jina lake).

3. Vita kati ya srikali ya vyombo vya habari (vikipiganwa kwa kutunga sheria dhibiti ili umma usijue kinachoendelea kusudi mfalme uwongo atamalaki)

4. Vita kati ya srikali ya watafiti (hakuna ku publish findings no matter how realistic and important they are, unless tu ziwe zinai pamba serikali"


5. Vita dhidi ya wasomi (Hakuna kutmia elimu yako kwa lolote mpaka likubalike na wanasiasa kwa maendeleo ya ccm, kama wewe una utaalam wako na ubunifu wako, kama si mwana ccm, kafie mbali".
 
Chadema ina wasemaji wengi kweli kweli naona Tumaini Makene tangia tuanze kuratibu mambo yake mabaya aliyofanyiwa na Shigongo amekuwa kimya sana siku hizi.

Shigongo alimfanyia kitu mbaya sana Makene nikiangalia hizi Picha Lukuki hapa nasikia kulia, ingawa itikadi zetu hazifanani lakini mimi ni kijana, mtanzania kama wewe nimeumia sana.

Sasa Makene kwa Hili pia tumuachie Mungu? Shigongo ni katili sana amekufanyia kitu kibaya sana, najua wajua fika alichokufanyia Shigongo!

Hata Molemo, Crashwise na wengine wanajua fika!
 
Ninachojua ni kwamba CDM imesheheni mafundi wa kisheria. Kama CCM wanataka mashindano ya kisheria na CDM nakaa kwa mkao wa 4 nikiangalia muvi kama ya Rambo hivi. Mahakama ikiamua kwamba chama kisiwe na watu wanaofanya mazoezi kwa jina la vyama, basi hata Green Guards naturally hakitakuwapo. Kwa kuwa mwakani ccm ni chama cha upinzani, wanachokifanya sasa ndicho kitakachofanyika dhidi yao mwakani. Patamu hapo.
 
Hila zao za kijinga awata weza kuzuia mabadiliko ya kweli kwenye nchi hii Mungu ibariki chadema na Tanganyika kwa ujumla wake
 
Chadema ina wasemaji wengi kweli kweli naona Tumaini Makene tangia tuanze kuratibu mambo yake mabaya aliyofanyiwa na Shigongo amekuwa kimya sana siku hizi.

Shigongo alimfanyia kitu mbaya sana Makene nikiangalia hizi Picha Lukuki hapa nasikia kulia, ingawa itikadi zetu hazifanani lakini mimi ni kijana, mtanzania kama wewe nimeumia sana.

Sasa Makene kwa Hili pia tumuachie Mungu? Shigongo ni katili sana amekufanyia kitu kibaya sana, najua wajua fika alichokufanyia Shigongo!

Hata Molemo, Crashwise na wengine wanajua fika!
Maneno ya fisi hayo kitu gani mbaya umeanza kuweweseka?
 
Hakika tutashinda..

Sasa crashwise na Molemo mbona mnapiga gitaa wenyewe na kucheza wenyewe? Siasa mbaya ndugu zangu, kuanzia October tutaanza kuheshimiana maana maneno yatakuwa kwishney kabisa na hapo tukutane 2025 ambapo Babu yetu Dr Slaa atakuwa anatimiza miaka 98.

Halafu tutakuwa tunaimba kwa pamoja "watoto wangu eeh.. Mimi baba yenu ehh.....sina nguvu tena ehh.... Ya kugombea tena eeh.... Kugombea Nini ehh.... Umagogoni ehh.... Watoto wangu ehh nyumba ile pale ehh.... Muigopeni kama ukoma ehhh.... Watoto wangu ehh
 
Makundi hayo ni hatarishi kwa pande zote hebu ondoeni upofu wa kisiasa na muone hatari iliyopo kwa uwepo na muendelezo wa makundi hayo!!!!!
 
Hao mashetani green Guard tena jana wamempga kamanda wetu kwenye mkutano wa mwembetogwa iringa na police wanaangalia
 
Maneno ya fisi hayo kitu gani mbaya umeanza kuweweseka?

Chademakwanza,

Unajua tunaongelea Nini hapa wakubwa? Umeingia juzi JF mbwembwe nyingi hujuwi tuache wakubwa tuongee au ndio umetoka kuamka uende shule?

Umekunywa chai? Chukua 500 mezani uwahi shule sawa mtoto? Msalimie sana Mwl Mussa sawa ehh
 
Ccm wanatapatapa. Hawama lolote. Tutapambana nao kwa kila namnaHao ni wahuni wasio na maana. Safari hii hatutawavumilia nguvu ya umma itatumika sawasawa
 
Back
Top Bottom