Mkakati mzito umesukwa na CCM wa kumchonganisha Prof Lipumba na waislam. Kwa mujibu habari zilizonifikia mpango huo una lengo la kusambaratisha UKAWA wasisimamishe mgombea mmoja nafasi ya urais. Mtoa habari anasema kuwa CCM wameiona hatari ya muungano wa CUF na CHADEMA. Wanasema ni hatari hasa watakapofanikisha lengo la kumtosa Lowasa rasmi. Mtoa habari anasema kunakanda zimekusanywa za kuonyesha unafiki wa Lipumba kwa Waislam.Naambiwa mkakati huo unaandaliwa na wanaojiita Mashekh kutoka Morogoro wakiongozwa na mhariri gazeti moja linalondika habari za waislam likijifanya ni la waislamu