MK 4 ndio gemu la karne ,hakuna Arcade game linalozidi kwa ubora

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Sep 7, 2016
17,496
21,270
Wakuu mimi nimecheza gemu nyiingi sana hizi za PC ingawaje kwa miaka ya hivi karibuni nimesitisha kidogo ila hakuna gemu ambalo nalikubali sana kama Motor Kombat 4 aisee hili gemu haliishi hamu kwa kweli

Tena isitoshe enzi hizo linatoka toka teknolojia ilikuwa haijasambaaa kivile so ulikuwa ukipiga FATALITIES unaonekana bonge la mjanja aisee tena kama sikosei fatality ya kwanza kabisa kuijua ilikuwa ya Raiden ile ya fimbo

Screenshot_2017-02-28-18-49-13_1.jpg


Enzi hizo mtu unacheza kwenye vibanda umiza kwa kuwa ukicheza peke yako nyumbani hainogi sawa na kuangalia mpira peke yako nyumbani


Fatality ya pili kuijua ilikuwa ya reptile kuna sehemu ulikuwa una sett then unabonyeza button ya direction ya juu anafanya yake

Screenshot_2017-02-28-18-53-12_1.jpg


Fatality ya 3 kuijua ilikuwa ya liu kang ,fan fatality


Baadaye ikaja ufundi mwingine wa kumchezesha shinnok kama goro

Screenshot_2017-02-28-18-58-00_1.jpg



Hapa ndio nilizidi kuonekana fundi

Pia mbali na goro other hidden characters ambao ilikuwa ngumu sana kujulikana na watu ni Noob saibot ambaye anasimama badala ya Reiko

Kitana ambaye anasimama badala ya Tanya


Yani kwa kifupi Motor Kombat 4 ni very interesting game ever kwenye hii dunia

Kuna cheat fulani hivi ilikuwa ukiset inakuwa mtu akikupiga damu zinaisha kwake mwenyewe

Yaan daaah kama wewe ni mpenzi wa Arcade game na hujacheza MK4 kajinyonge tuuuu.


Screenshot_2017-02-28-19-05-11_1.jpg
 
me nilikuwa napenda dogo akicheza utasikia a
Wanyannyanyanyaaaaaaa
Mara get out over here ah basi bwana ingawa ni kitambo sana
 
we unaleta game za mwaka 47 tena zilikuwa kwenye 2D sahv kuna motor combat X ndo tunajiburisha nayo humo ndani ni hatari tupu lakini kwa ww ulivyo nyuma nenda kwanza kaanze na mortal combat complete edition hyo itakufaa zaidi alafu ndo uje X ukiwa basis nzuri
 
we unaleta game za mwaka 47 tena zilikuwa kwenye 2D sahv kuna motor combat X ndo tunajiburisha nayo humo ndani ni hatari tupu lakini kwa ww ulivyo nyuma nenda kwanza kaanze na mortal combat complete edition hyo itakufaa zaidi alafu ndo uje X ukiwa basis nzuri

 
Sijafanikiwa kupiga fatalities
hapa kuna njia mbili

Njia ndefu ambayo ina raha yake ukiweza na njia fupi

Tukianza na njia ndefu

Hapa unaenda movie list wanakuelekeza jinsi ya kupiga FATALITIES na styles mbalimbali na kupata weapons

U inamaanisha up (juu)

D inamaanisha Down

B back

F forwad

block (Gadi)

Hp ina maana high punch ngumi ya juu

Lp low punch yani ngumi ya chini

Lk low kick maana yake teke la chini

Hk high kick yani teke la juu

Rn run yani kukimbia

Tuchukulie mfano wa fatality ys raiden ya fimbo ukienda movie list wameandika

D+U+U+U+HP

Hapo inamaanisha unabonyeza button ya direction ya chini mara moja na direction ya juu mara 3 halafu unabonyeza button ya ngumi mara moja

Au tuchukulie fatality ya scorpion ile ya ng'e

Wameandika

B+F+D+U+HP

Yani nyuma mbele chini juu halafu unabonyeza button ya ngumi ila inabidi uwe fasta kidogo


FATALITIES zimegawanyika sehemu mbili zipo ambazo inabidi umsogelee adui yako kwa karibu pia zipo ambazo inabidi uwe na umbali kidogo na adui yako
 
we unaleta game za mwaka 47 tena zilikuwa kwenye 2D sahv kuna motor combat X ndo tunajiburisha nayo humo ndani ni hatari tupu lakini kwa ww ulivyo nyuma nenda kwanza kaanze na mortal combat complete edition hyo itakufaa zaidi alafu ndo uje X ukiwa basis nzuri
Mkuu MKX imezidi uongo mpaka inakera
 
Du...sisi tuliandaa pambano mimi na kaka zangu badaye walipoona miminaweza zile faralities wakaanza kuweka sheria za ajabu ajjabu eti mimi lazima wanichagulie mtu, kumbe mwenzao kila mtu nilikuwa najua style zake
 
Ngoja nikaribu nione
Kajaribu mkuu

Njia fupi ni hii

Nenda kwenye options bonyeza

Baada ya hapo unaenda kwenye continues halafu unabonyeza Run na block kwa pamoja utasikia kicheko halafu utasikia wanasema Outstanding

Baada ya hapo cheats menu itakuwa enabled tayali

Hapo utakuwa unaweka on kama unataka fatality one au two

Baada ya kuset on

Unakuja kucheza kama kawaida ukishasikia finish him unabonyeza direction ya chini na ngumi (Down +HP) hapo utaweza kupiga fatality
 
we unaleta game za mwaka 47 tena zilikuwa kwenye 2D sahv kuna motor combat X ndo tunajiburisha nayo humo ndani ni hatari tupu lakini kwa ww ulivyo nyuma nenda kwanza kaanze na mortal combat complete edition hyo itakufaa zaidi alafu ndo uje X ukiwa basis nzuri
Naomba link ya hilo game
 
hapa kuna njia mbili

Njia ndefu ambayo ina raha yake ukiweza na njia fupi

Tukianza na njia ndefu

Hapa unaenda movie list wanakuelekeza jinsi ya kupiga FATALITIES na styles mbalimbali na kupata weapons

U inamaanisha up (juu)

D inamaanisha Down

B back

F forwad

block (Gadi)

Hp ina maana high punch ngumi ya juu

Lp low punch yani ngumi ya chini

Lk low kick maana yake teke la chini

Hk high kick yani teke la juu

Rn run yani kukimbia

Tuchukulie mfano wa fatality ys raiden ya fimbo ukienda movie list wameandika

D+U+U+U+HP

Hapo inamaanisha unabonyeza button ya direction ya chini mara moja na direction ya juu mara 3 halafu unabonyeza button ya ngumi mara moja

Au tuchukulie fatality ya scorpion ile ya ng'e

Wameandika

B+F+D+U+HP

Yani nyuma mbele chini juu halafu unabonyeza button ya ngumi ila inabidi uwe fasta kidogo


FATALITIES zimegawanyika sehemu mbili zipo ambazo inabidi umsogelee adui yako kwa karibu pia zipo ambazo inabidi uwe na umbali kidogo na adui yako
Naomba kuijua njia fupi
 
Back
Top Bottom