mwakajilae
Member
- Mar 11, 2011
- 58
- 46
Wakati tukiendelea kuhakikisha haya mainteligensia yaliyokuwa na nia ya kumuua Ulimboka yanaanikwa na kuyashughulikia.
Nawaomba wanajamvi tuweze kulitazama na kulitafakali suala hili la Muungano wetu kwa kina na tahadhari kubwa ikiwa si kwa kukomoana, kuoneshana bali kutazama kwa mbele na nyuma.
Mjadala huu unapande mbili za mabishano, upande mmoja ukionesha kutokuridhishwa na upande mmoja ambao ni Tanganyika isiyokuwapo, inayojinufaisha kwa kujificha kwenye sura ya Muungano. Lakini wa upande wa bara wanashutumu juu ya hadhi iliyo nayo Zanzibar kwa maana ya utambulisho wake kama nchi.
Kiufupi matatizo makubwa ya Muungano wetu siyo hayo kimtazamo wangu bali ni uhusiano wa Muungano na Maisha ya Watanzania kama yanaenda sambamba.
Mfano: Wazanzibari na Waliokuwa Watanganyika wanatambuana kwamba ni wamoja? Wananufaika na Muungano? Au ni Muungano wa viongozi tuu kwamba ndiyo wanaofahamiana?
Hoja ya Zanzibar kuwa nchi au siyo nchi, hoja ya Zanzibar kuwa na uwakilishi sawa na bara ninaona haina Mashiko zaidi ya hayo machache niliyoyainisha hapo. Kwani nchi haiwi nchi kutokana na uwingi wa watu au ukubwa wa eneo lake bali ni kutokana na historia yake ya Mapambano ya kuitafta ujitambulisho wa nchi hyo.
Ndo maana japo Afrika ni bara kubwa lakini halina mwakilishi wa kura ya Veto umoja wa Mataifa, ndiyo maana nchi kama Nigeria ni kubwa kuliko Uingereza lakini Nigeria haina kura ya Veto nk.
Nilichotaka kukizungumzia ni Matarajio yetu juu ya Mapambano dhidi ya Muungano na hoja ya Zanzibar kutamani kujitenga.
Kihistoria kabisa hakuna mtu anayeetambulika kama ni Mzanzibari, matunda ya Muungano ni utambulisho wa uwepo wa Wazanzibari.
Wazanzibari wanaitaka Zanzibar ipi?
Kuna Zanzibar ya Mwarabu, Kuna Zanzibar ya Mwingereza, Kuna Zanzibar ya Sultan, Kuna Zanzibar ya Uhuru wa mwaka 1963, Kuna Zanziba ya Mapinduzi na kuna Zanzibar ya Muungano ambayo ndiyo hii. Hawa wanaitaka ipi?
Ijulikane wazi kwamba kabla ya Muungano haya makundi yote hayakuwa mamoja, yalikuwa makundi hasimu wakubwa, Muungano umewafanya wawe wamoja hawa.
Kiufupi, tujadili mstakabali wa Zanzibar nje ya Muungano kwa wanaoijua historia ya Visiwa hivi vikubwa vya Pemba na Unguja.
Nilikuwa naona ni rahisi kuuboresha Muungano huu ukawa wa wananchi kuliko kuuvunja pasipo kuyatazama haya mbele na nyuma.
Asante.
Nawaomba wanajamvi tuweze kulitazama na kulitafakali suala hili la Muungano wetu kwa kina na tahadhari kubwa ikiwa si kwa kukomoana, kuoneshana bali kutazama kwa mbele na nyuma.
Mjadala huu unapande mbili za mabishano, upande mmoja ukionesha kutokuridhishwa na upande mmoja ambao ni Tanganyika isiyokuwapo, inayojinufaisha kwa kujificha kwenye sura ya Muungano. Lakini wa upande wa bara wanashutumu juu ya hadhi iliyo nayo Zanzibar kwa maana ya utambulisho wake kama nchi.
Kiufupi matatizo makubwa ya Muungano wetu siyo hayo kimtazamo wangu bali ni uhusiano wa Muungano na Maisha ya Watanzania kama yanaenda sambamba.
Mfano: Wazanzibari na Waliokuwa Watanganyika wanatambuana kwamba ni wamoja? Wananufaika na Muungano? Au ni Muungano wa viongozi tuu kwamba ndiyo wanaofahamiana?
Hoja ya Zanzibar kuwa nchi au siyo nchi, hoja ya Zanzibar kuwa na uwakilishi sawa na bara ninaona haina Mashiko zaidi ya hayo machache niliyoyainisha hapo. Kwani nchi haiwi nchi kutokana na uwingi wa watu au ukubwa wa eneo lake bali ni kutokana na historia yake ya Mapambano ya kuitafta ujitambulisho wa nchi hyo.
Ndo maana japo Afrika ni bara kubwa lakini halina mwakilishi wa kura ya Veto umoja wa Mataifa, ndiyo maana nchi kama Nigeria ni kubwa kuliko Uingereza lakini Nigeria haina kura ya Veto nk.
Nilichotaka kukizungumzia ni Matarajio yetu juu ya Mapambano dhidi ya Muungano na hoja ya Zanzibar kutamani kujitenga.
Kihistoria kabisa hakuna mtu anayeetambulika kama ni Mzanzibari, matunda ya Muungano ni utambulisho wa uwepo wa Wazanzibari.
Wazanzibari wanaitaka Zanzibar ipi?
Kuna Zanzibar ya Mwarabu, Kuna Zanzibar ya Mwingereza, Kuna Zanzibar ya Sultan, Kuna Zanzibar ya Uhuru wa mwaka 1963, Kuna Zanziba ya Mapinduzi na kuna Zanzibar ya Muungano ambayo ndiyo hii. Hawa wanaitaka ipi?
Ijulikane wazi kwamba kabla ya Muungano haya makundi yote hayakuwa mamoja, yalikuwa makundi hasimu wakubwa, Muungano umewafanya wawe wamoja hawa.
Kiufupi, tujadili mstakabali wa Zanzibar nje ya Muungano kwa wanaoijua historia ya Visiwa hivi vikubwa vya Pemba na Unguja.
Nilikuwa naona ni rahisi kuuboresha Muungano huu ukawa wa wananchi kuliko kuuvunja pasipo kuyatazama haya mbele na nyuma.
Asante.