Mjadala: Upinzani utaanzaje kujipanga kwa uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na hatimae uchaguzi mkuu wa uraisi wa 2025 ndani ya mazingira magumu?

Get prepared, bt usisahau KANU kiliangushwa na majabali yaliyotoka ndani ya chama kuungana na wapinzani .

CDM ikinyamaza, tegemea uasi Kutoka ndani ya chama tawala, lazima watagombana kugombea madaraka.

Bora kusubiri huo uasi ndani ya ccm, lakini kwa mwenendo huu wa chaguzi ambazo rais na genge lake wanaamua nani atangazwe mshindi, kisha watu kuachwa na vilema vya maisha, halafu viongozi wanaenda kwenye maridhiano sijui muafaka ni upuuzi tu.
 
Vyombo vya dola hufanya vitendo vya kikatili kutokana na hali yao kiuchumi kuwa mbaya kwao , au tu ni roho mbaya na ukatili, je, ni elimu duni juu ya sheria au tu ni kufuata amri kutoka juu?

Kwa katiba hii ambayo viongozi wa vyombo vya dola wanapewa vyeo kama hisani na rais, usitegemee vyombo vya dola kufanya kazi kwa mujibu wa sheria, zaidi ya utashi wa rais na genge lake. Tuliona jinsi Magufuli alitumia waziwazi vyombo vya dola kufanya mambo yaliyo nje ya sheria.
 
Time frame ya Maridhiano ninayomaanisha ni:

1. Ikiwa, Maridhiano yataendelea Hadi 2024, halafu yakavunjika, CDM itakuwa imepata hasara Kwa kiasi Gani??? Lazima iwe calculated.

2. Ikiwa watakubalina RASIMU alosimamia Judge WARIOBA irudishwe mezani, na wakiruhusu uundwaji wa Tume na Katiba mpya ya Zima moto mwaka 2024 Kwa mfano, je muda wa kikatiba wa kiuchaguzi utawatosha kuwashirikisha wananchi?
Ahsante sana nimekuelewa.

Hata hivyo maana sahihi ya maridhiano ni kuweka mawazo au imani ya pande mbili yawe sawa yaani kuwiana.

Lakini Chadema lazima itambue kuwa CCM inanunua muda hadi 2024 na 2025 hiyo ipo wazi.

Hapo ndipo unapokuja na mikakati ya namna ya kujiandaa maana umeshatambua azma ya mtesi wako.

Pili, hiyo ya kupanga RASIMU ya Warioba irudishwe mezani nalo pia CCM yanunua muda.

Sasa ni mwisho wa September na mwakani ni 2023 na chaguzi ni 2024 kisha 2025.

Upo sawa.

Hapo ndipo nnapokuja na nyenzo namba 4 iitwayo kuunganisha yaani "Connect" ambayo itafanywa na Chadema digital katika mtandao wake.

Hii nyenzo au "tool" itasaidia sana kati ya sasa na ifikapo wakati wa uchaguzi wa 2024 na ule wa 2025.

Lakini "CHADEMA UNGANISHA" yafanyaje kazi?

Kwa kuwa njia hii yaingia zaidi kimkakati sitaweza kuijadili sana hadi hapo ntaporidhika na maoni ya wapinzani wenyewe kwani kweli Chadema ikitumia njia hii basi CCM itapata taabu sana.
 
Mara nyingi vurugu hutegemea na hali halisi ya jamii kiuchumi na kiakili huwezi fahamu kama wale wafanyao vurugu uwezo wao kiakili umekaaje ukaja kujutia uamuzi wa kuleta vurugu.

Nchi ilipo saa hii ina shida kubwa ila twasema kwa kiingereza ipo "contained within" yaani wananchi wameamua kunyamaza. Sasa ukija na kuhamasisha vurugu utaleta hali ya zaidi ya yale yalotokea Kimbari.

Sasa hivi tuna Panyaroad na vijana wengi wasajiriwa hili ni jeshi tayari sasa upo tayari kuona ndugu zako na familia yako zinapata taabu?

Sisi wenye kujadili kwa makini hatutaki hali hiyo itokee hata kidogo.

Majadiliano au "Dialogue" bado ndo njia sahihi ya jamii ilostaarabika hadi kitapoeleweka. Cha msingi ni masuala yepi Chadema wayaweka mezani kwenye majadiliano na huyafuatilia kwa kiasi gani.

Hata uamuzi wa kususia chaguzi si sahihi kwani pia huwanyima wapiga kura wa Chdema haki yao ya msingi ya kupiga kura.

Kwa taarifa yako vyama aina ya CCM huwa havijali majadiliano, bali huogopa tu nguvu ya umma. Hayo majadiliano yanaendelea sasa ni furahisha genge. Kama watu wataendelea kukaa kwenye meza ya maridhiano, tegemea viongozi kupewa ulaji huku madai yako yakipuuzwa. Nikusaidie kitu, wananchi hawajaamua kukaa kimya, bali uoga ndio umewaingia.

Hilo la kususia uchaguzi ni jambo sahihi, maana kwenda kila siku kwenye box la kura, kisha mabox ya kura kuletwa kwa uratibu wa vyombo vya dola, mbele ya wasimamizi wa uchaguzi, utakuwa una matatizo ya kiakili kama utaendelea kushiriki uchaguzi wa aina hiyo. Inshort hakuna uchaguzi wa CDM na wafuasi wake wa kwenda zaidi ya kupotezeana muda. Bado nasisitiza, machafuko au nchi kupinduliwa ndio yatarejesha heshima ya box la kura.
 
Ahsante sana nimekuelewa.

Hata hivyo maana sahihi ya maridhiano ni kuweka mawazo au imani ya pande mbili yawe sawa yaani kuwiana.

Lakini Chadema lazima itambue kuwa CCM inanunua muda hadi 2024 na 2025 hiyo ipo wazi.

Hapo ndipo unapokuja na mikakati ya namna ya kujiandaa maana umeshatambua azma ya mtesi wako.

Pili, hiyo ya kupanga RASIMU ya Warioba irudishwe mezani nalo pia CCM yanunua muda.

Sasa ni mwisho wa September na mwakani ni 2023 na chaguzi ni 2024 kisha 2025.

Upo sawa.

Hapo ndipo nnapokuja na nyenzo namba 4 iitwayo kuunganisha yaani "Connect" ambayo itafanywa na Chadema digital katika mtandao wake.

Hii nyenzo au "tool" itasaidia sana kati ya sasa na ifikapo wakati wa uchaguzi wa 2024 na ule wa 2025.

Lakini "CHADEMA UNGANISHA" yafanyaje kazi?

Kwa kuwa njia hii yaingia zaidi kimkakati sitaweza kuijadili sana hadi hapo ntaporidhika na maoni ya wapinzani wenyewe kwani kweli Chadema ikitumia njia hii basi CCM itapata taabu sana.

Kama una mbinu iweke hapa au wapelekee CDM huko ofisini kwao. Lakini ninavyoona sioni kama utakuwa na mbinu yoyote yenye nguvu, na ifanye kazi zaidi ya machafuko. Njia za kistaarabu zimeproove failure katika kupambana na CCM. Ifahamike CCM haitumii njia za kistaarabu kubaki madarakani, itakuwa ni kosa la wazi kutegemea njia za kistaarabu wakati wenzako wanatumia uhuni kubaki madarakani.
 
Nimesema mara kadhaa humu jukwaani kuwa katika mambo Mbowe na CDM wamechemsha ni kukubali huo utapeli uitwao maridhiano. Unakubali maridhiano ili aliyeko madarakani atawale bila pressure, matokeo yake amejua unatii atakacho, anafanya yale yale anayokuzuia ww kufanya.
Huu ujinga unao itwa maridhiano baina ya mwenye madaraka na wasio nayo, una zalisha aina ya utawala kama uliopo Zanzibar Rais [ CCM ] , makamu wa Rais wa kwanza & wa pili [ ACT + CCM ] hapa pote bado mamlaka yapo kwa CCM . Labda kama Chadema wanataka kuwa tawi la CCM-B

Njia ya maridhiano haiwezi kuleta matokeo chanya kama bado CCM ana madaraka zaidi tu yataifanya Chadema kuwa tawi la CCM.
 
Hebu wakati mwingine tuache ushabiki na tuongeage ukweli...pamoja na matatizo ya chama tawala yaliyopo(mimi sina chama)....je pale Chadema kama wakipewa nchi , kuna team yakutosha kabisa inayoweza kuongoza nchi?Yaani kuanzia Rais,Waziri Mkuu, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Kiongozi nk nk....mbona sioni mtu wa level hizo pale??? au ndiyo akina Lema,Mbowe?
Katiba ya warioba ilisema mawaziri hawatokani na wabunge, ma DC sijui RC kufutwa meaning huhitaji wanasiasa wengi kuongoza nchi Una source tu professionals unaoona Wana uwezo wa kuongoza kama tu alivyofanya JPM kwa kina Mpango, Kabudi n.k ndio haswa katiba mpya ilitaka.

Kingine CHADEMA Ina watu wengi sana na Sio wote mpaka wawe wabunge ndio uwajue, binafsi nafahamu Wana CHADEMA wapo serikalini, mashirika ya kimataifa kama World Bank wengine ma doctor UD pale so usidhani kina Lema ndio cream utakua unaona kichuguu tu wakati kuna mlima wa Viongozi kibao wametapakaa ila sheria tu zinawabana kuwa active majukwaani ila siku CCM ikidondoka utawaona wazi wazi.

Mfano hii kata nayoishi anayedhamini vikao vya CHADEMA na mambo ya CHADEMA digital ni kigogo mmoja mstaafu wa JWTZ, so unaweza ona network za chama zilivyopenya hadi jeshini.
 
Nimesema mara kadhaa humu jukwaani kuwa katika mambo Mbowe na CDM wamechemsha ni kukubali huo utapeli uitwao maridhiano. Unakubali maridhiano ili aliyeko madarakani atawale bila pressure, matokeo yake amejua unatii atakacho, anafanya yale yale anayokuzuia ww kufanya.
Mkuu nadhani Iko wazi Mbowe alitaka siasa za amsha amsha ila umeona kesi ya ugaidi na Ile ilikua message kwamba tukichagua njia hiyo basi tutegemee watu wafungwe, kunyongwa, mitutu ya risasi n.k so Mbowe hakua na choice kwakweli ni sawa tu na Mandela alipokua gerezani.

2. Maridhiano nadhani ni nia ya kuingia Dili kwamba tutakuacha ufanye mipango Yako bila bughudha sisi utupe katiba mpya na time huru Ili 2025 wananchi waamue!!! Mama akakubali hayo madai ya katiba sasa time frame ni mpaka 2023 wakiona hakuna progress obvious watajitoa kwenye hiyo arrangement.

Nadhani sio jambo baya kama mtu kakubali "myamalize" mezani why mparuane barabarani, Mnyika aliomba tuwe watulivu mpaka mwisho wa vikao then ndio tuone mulekeo na mafanikio
 
Yes, afafanue.

Tangu UHURU hajatokea Bado mtu starategic, forward looking LEADERS aina ya Mbowe Kwa vyama vya upinzani.

Sijawahi mpuuza MWAMBA.
Mbowe wa maridhiano?😆.Mara 100% Tundu Antipas Lissu kuliko mbowe wa maridhiano upinzani/chadema kuchukua nchi kutoka kwa CCM ina wahitaji wanasiasa wenye kaliba za Lissu kuwatoa CCM madarakani na sio viongozi aina ya mbowe ana fanya siasa alizo fanya Mwalimu 1950s wakati ana dai Uhuru toka kwa Muingereza ana sahau kuwa mkoloni wa sasa karne hii ya 21 ni mweusi [ CCM ] asiye amini katika njia anayo amini mbowe.

Njia pekee itayo waondoa CCM madarakani ni revolution [ millitary revolution/ mass revolution ] na wala sio upumbavu unao itwa sanduku la kura wala ushenzi wa maridhiano.
 
Mkuu nadhani Iko wazi Mbowe alitaka siasa za amsha amsha ila umeona kesi ya ugaidi na Ile ilikua message kwamba tukichagua njia hiyo basi tutegemee watu wafungwe, kunyongwa, mitutu ya risasi n.k so Mbowe hakua na choice kwakweli ni sawa tu na Mandela alipokua gerezani.

2. Maridhiano nadhani ni nia ya kuingia Dili kwamba tutakuacha ufanye mipango Yako bila bughudha sisi utupe katiba mpya na time huru Ili 2025 wananchi waamue!!! Mama akakubali hayo madai ya katiba sasa time frame ni mpaka 2023 wakiona hakuna progress obvious watajitoa kwenye hiyo arrangement.

Nadhani sio jambo baya kama mtu kakubali "myamalize" mezani why mparuane barabarani, Mnyika aliomba tuwe watulivu mpaka mwisho wa vikao then ndio tuone mulekeo na mafanikio

Sipingi usemacho, lakini sikioni kwenye utekelezaji. Ngoja nitulie, lakini najua ni kupotezeana muda.
 
Mkuu, umesema maneno machache lakini ni maneno mazito sana.

Ni kwanini wadhani Upinzani nchini hawana mpango wowote wa kushinda chaguzi za 2024 na 2025?

Karibu sana mkuu, fafanua.
Kwa sababu moja kuu , ni kwamba vyama vyote vya upinzani vinahitaji kufanyiwa “polical reform” mpya kifalsafa na kimuundo wa vyama . ili kuweza kupambana na CCM na kumyang'anya madaraka njia wanazo tumia sasa hivi kupambana na CCM ni za kijinga sana zina wafanya wacheze vizuri ngoma zinazo pigwa na CCM huku wenyewe wakiwa hawajui ni kwa namna gani njia zao zina wanufahisha CCM mfano wa ujinga mmoja ni hii taka taka inayo itwa maridhiano.
 
Unataka watu wachapane ngumi baadhi ya wanaccm wafe na baadhi ya upinzani wafe ndipo uje na hiyo hoja ya kuwa na mpango wowote?
mao_zedong_quote.jpg
 
Mkuu nadhani Iko wazi Mbowe alitaka siasa za amsha amsha ila umeona kesi ya ugaidi na Ile ilikua message kwamba tukichagua njia hiyo basi tutegemee watu wafungwe, kunyongwa, mitutu ya risasi n.k so Mbowe hakua na choice kwakweli ni sawa tu na Mandela alipokua gerezani.

2. Maridhiano nadhani ni nia ya kuingia Dili kwamba tutakuacha ufanye mipango Yako bila bughudha sisi utupe katiba mpya na time huru Ili 2025 wananchi waamue!!! Mama akakubali hayo madai ya katiba sasa time frame ni mpaka 2023 wakiona hakuna progress obvious watajitoa kwenye hiyo arrangement.

Nadhani sio jambo baya kama mtu kakubali "myamalize" mezani why mparuane barabarani, Mnyika aliomba tuwe watulivu mpaka mwisho wa vikao then ndio tuone mulekeo na mafanikio
Ndugu ingekuwa Rahisi mama kutimiza Masharti ya CDM ikiwa tu Hana Nia ya kugombea 2025.

Ingekuwa mapema tu baada ya kuanza vikao angefuta Lili zuio Batili.

Bado Pana utata sana ktk jambo Hilo.
 
Ndugu ingekuwa Rahisi mama kutimiza Masharti ya CDM ikiwa tu Hana Nia ya kugombea 2025.

Ingekuwa mapema tu baada ya kuanza vikao angefuta Lili zuio Batili.

Bado Pana utata sana ktk jambo Hilo.
Mkuu hii mbinu alitumia Tshisekedi na alipopata upenyo tu wote mnajua alivyokigeuka chama tawala kilichopita, so ikifanikiwa huwa ni mbinu nzuri ya kumaliza adui Yako kimya kimya.

2. Kuhusu incumbency ya Samia, kwa maoni yangu dili lilivyokaa ni kwamba Samia ataendelea 2025 ila obviously kwingine kote wananchi waamue, which is a win kwa upinzani maana wameingia kwenye meza ya mazungumzo wakiwa hawana hata madiwani 10 nchi nzima so kupata wabunge hata 120+ na halmashauri za kumwaga kama 2015 hivi ni mafanikio makubwa kuelekea kuifuta CCM 2030.

Kitila Mkumbo amesema chance ni hii tu, akiingia Rais mwingine tusahau katiba mpya Wala tume huru na CCM itatawala milele. So ni bora ujifanye mjinga katiba ipatikane afu mnyooshane baadae maana hatokua na la kufanya tena.
 
Mkuu hii mbinu alitumia Tshisekedi na alipopata upenyo tu wote mnajua alivyokigeuka chama tawala kilichopita, so ikifanikiwa huwa ni mbinu nzuri ya kumaliza adui Yako kimya kimya.

2. Kuhusu incumbency ya Samia, kwa maoni yangu dili lilivyokaa ni kwamba Samia ataendelea 2025 ila obviously kwingine kote wananchi waamue, which is a win kwa upinzani maana wameingia kwenye meza ya mazungumzo wakiwa hawana hata madiwani 10 nchi nzima so kupata wabunge hata 120+ na halmashauri za kumwaga kama 2015 hivi ni mafanikio makubwa kuelekea kuifuta CCM 2030.

Kitila Mkumbo amesema chance ni hii tu, akiingia Rais mwingine tusahau katiba mpya Wala tume huru na CCM itatawala milele. So ni bora ujifanye mjinga katiba ipatikane afu mnyooshane baadae maana hatokua na la kufanya tena.
Hizo hesabu ni ngumu kuliko Function, matrix, log,nk.

CCM Kwa HILA, akitoka shetani, wanafuatia.!!!!
 
Lengo la mada hii ni kuona wale wapenda demokrasia na siasa za kweli wakijongea hapa na kushusha nondo na madini mbalimbali katika kufanya kitu chitwa "brain storming".

Katika muktadha huo basi, tutaweza kuangalia sera za chama cha CCM ambacho ndicho chaongoza serikali ya Tanzania kwa sasa na pia ilani ya chama hicho na utekelezaji wake na wapi wamefikia.

Pia mada hii itatoa fursa ya kuangalia hali ya uchumi wa Tanzania kati ya 2015 na 2021 na baada ya hapo ni wapi tumekwama, sababu za kukwama na nini kifanyike kwa maana ya kwamba je, serikali ina washauri wanofaa wa uchumi "Think Tanks", taasisi binafsi za kuchambua sera za kiuchumi na wadau mbalimbali na nini nafasi yao katika kuishauri serikali katika nyakati ngumu au nyakati tata.

Hali kadhalika mada itakaribisha maoni ya upinzani, hali yake kisiasa, uwezo wake wa kuendeleza harakati na nini kifanyike ili kuleta chagizo ambalo litaweza kutikisa hali ya kisiasa nchini hususan CCM.

Hakika uchaguzi wa Kenya umetoa funzo kubwa kwa wale wanofuatilia harakati za kisiasa na kutufumbua macho wengi wetu kuwa kweli Wakenya wana demokrasia ya kweli.

Lakini kuna mambo matatu makubwa ambayo ndiyo yaliyonichagiza kuamua kuanzisha mada hii.

Kwanza, ni Tume Huru ya Uchaguzi ya Kenya ambayo imeonyesha hali yake ya kuwa yajitegemea, ni huru na haina mashinikizo kutoka sehemu yoyote ile. Tume ikatangaza ushindi wa Rais Ruto licha ya kwamba Rais aliyepita Bwana Uhuru Kenyatta alikuwa waziwazi akimuunga mkono Bwana Raila Odinga. Hata humu JF yumo mwenzetu mmoja na wengine kadhaa ambao walionyesha kuumunga mkono Bwana Odinga.

Bwana Odinga alipinga matokeo hayo kwa kudai kulikuwa na mizengwe ya udanganyifu na mwishowe mahakama uamuzi wa kuthibitisha ushindi wa Bwana Ruto, uamuzi ambao wapiga kura wengi wa Kenya waliukubali kuwa ulikuwa wa haki na ukweli.

Lakini ushindi wa Rais Ruto ulionyesha kuwastua wana CCM na wafuasi wao kwani katika uchaguzi wa Kenya hakukuwepo na ahadi ya goli la mkono.

Hii dhana ya goli la mkono ni kuthibitisha kuwa CCM ni chama dola na kina uwezo wa kuamua kuwa madarakani kwa muda wowote ambao chama hicho kitapenda kukaa na chaguzi zote zitaamuliwa na wao kwa kutumia vyombo vya dola.

Pili, wenzetu Wakenya uchaguzi wao ulikuwa na maandalizi ya kutosha, kuanzia wapiga kura kujiandikisha hadi kila kituo cha kupigia kura kuwa tayari kimepokea fomu zote za kupigia kura.

Moja ya sababu kubwa ya hapa ni uwezo wa wagombea wa upinzani kuweza kuchukua fomu au kujiandikisha uzuri kituoni salama bila kubughudhiwa na kuthibitishwa na kisha kuketi mahala au kwenda nyumbani kusubiri matokeo salama.

Hali nyingine ni kwa vituo vya kupigia kira kuendelea kupokea wapiga kura na kufungwa mara tu na inapothibitika kwamba wapiga kura wote wa CCM na vyama vingine wametumia haki yao hiyo ya kikatiba kufanikisha zoezi hilo.

Tatu, mitandao ya "internet" ni muhimu sana katika nyakati za uchaguzi na husaidia taasisi kama tume ya uchaguzi kufanya kazi zake kwa ufanisi zaidi kwa kuweka fomu za kujiandikisha katika tovuti yake ambapo wapiga kura wataweza kunywila fomu hizo kwa haraka na kuzirudisha vituoni bila kuchelewa.

Pia hiyo itasaidia kuwawezesha wapiga kura kufuatilia matokeo ya uchaguzi mitandaoni bila kusubiri kwa muda mrefu. Pia mitandao itasaidia kurahisisha mawasiliano baina ya watanzania waliopo maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi bila kuzuiwa wala kukwamishwa.

Hayo mambo matatu ndiyo yamechangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha uchaguzi wa hawa majirani zetu jambo ambalo ni la kujivunia kwao na kulitamani hapa kwetu Tanzania.

Sasa basi, Tanzania yaelekea kufanya Uchaguzi wake Mkuu wa Urais mwaka 2025 na kabla ya hapo utakuwepo uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024. Jambo la msingi ambalo CCM na serikali yake yapaswa kufanya ni kutorudia hali ya mwaka 2019 ambapo vyama vya siasa baada ya kukaa pembeni kwa miaka mitatu hadi minne ndiyo vikaja kushiriki uchaguzi.

Jambo jingine ni CCM na serikali yake kuhakikisha wapinzani hawapati bughudha kutoka kwa vyombo vya dola hasa Polisi na Usalama wa Taifa.

Wakati sasa umefika wa wapinzani kuamua kuwa imetosha na kazi ianze. Lakini wanaanza vipi kampeni ilihali mikutano imepigwa marufuku?

Hapa ndipo penye kiini cha mada na wapinzani wapaswa kuja na mikakati na mipango sahihi na thabiti.

Kuna kitu chaitwa "Tools for Activists" au kwa kiswahili ni nyenzo kwa wanaharakati ambazo hutumika kuandaa shughuli za chama mbadala. Napenda kutoa picha ya chama mbadala yaani "alternative party" kwa CCM.

Chama mbadala kitatoa mawazo mbadala kuhusu nini kifanyike katika maeneo ya siasa, uchumi na kijamii.

Moja ya sababu kubwa ya vyama vya upinzani kama CHADEMA kushindwa katika kukabiliana na chama chenye nguvu kama CCM ni kushindwa kuunda nyenzo sahihi za wanaharakati wake na kuzitumia kufasaha. Nyenzo hizi husaidia shughuli za chama, wanachama na wafuasi kuwa pamoja na kueneza ujumbe.

Kwa kuwa CHADEMA ndiyo chama pekee na kikubwa cha upinzani kwa sasa, itabidi chama hicho kipigwe msasa na nakshi ili kiweze kuwa na taswira ya chama tishio na kilicho tayari hasa kuchukua madaraka ya kuongoza Tanzania.

Hivyo basi, tuangalie safu yake ya uongozi, makada wake na wanachama wake ambao wataamua kusimama katika chaguzi zijazo. Sasa hilo ni suala ambalo CHADEMA wenyewe wapaswa kuamua haraka maana katika saa ya kisiasa muda huu ndiyo chama kipo katikakati.

Baada ya kuangalia huko juu kwenye uongozi tushuke chini kidogo kuangalia idara ya uenezi na propaganda. Hivyo ni lazima kwanza CHADEMA wakiri kwamba hakuna watu wenye uwezo au waliopo ni wachache . Hivyo kuwepo na timu maalum ambayo itashughulika na masuala ya teknolojia na mitandao yote IG, Twitter na kwingine na hilo ni jambo la dharura.

Hizi nyenzo au "tools for activists" zipo za aina mbili zipo za kawaida kabisa yaani kwenye uwanja wa kisiasa na zipo zile ambazo hutumika mitandaoni.

Sasa baada ya kuongea hayo na kutambulisha mada hii ambayo kama nilivyoomba hapo mwanzoni kwamba iwe endelevu hadi ifikapo wakati wa chaguzi zote (2024 na 2025) ningependa kuungwa mkono na wadau wote ambao wanataka kuona Tanzania yarudisha uchumi wa kati na uchumi huo hautetereki.

Kisha nitaendelea kutoa kidogokidogo zile nyenzo ambazo wanaharakati na wanasiasa wa upinzani wazihitaji ili kuiga mazuri ya uchaguzi wa Kenya na busara za mzee Raila Odinga kukubali kushindwa uchaguzi bila kinyongo.

Karibuni sana ndugu zanguni na naomba tuache utani na maneno yasiyofaa.
Mimi nashauri hivi lile jopo zima la tume ya uchaguzi Nchini Kenya likiongozwa na Chebukati na mahakama ya Kenya lije Lisimamie uchaguzi wa Tanzania 2024-2025....la sivyo Hii nchi yetu ina waoga,wajinga,wahujumu uchumi,walamba Asali wengi mnooo....watakao fanya juu chini hata kushirikiana na mabeberu kuendelea kusalia Uongozini....ikishindikana hivi itabidi mtutu wa bunduki utumike kusambaratisha genge la wanyonyaji...
 
Kama una mbinu iweke hapa au wapelekee CDM huko ofisini kwao. Lakini ninavyoona sioni kama utakuwa na mbinu yoyote yenye nguvu, na ifanye kazi zaidi ya machafuko. Njia za kistaarabu zimeproove failure katika kupambana na CCM. Ifahamike CCM haitumii njia za kistaarabu kubaki madarakani, itakuwa ni kosa la wazi kutegemea njia za kistaarabu wakati wenzako wanatumia uhuni kubaki madarakani.
Ukisema kama nina mbinu niwapelekee huko ofisini kwao unakuwa hutumii njia sahihi ya kufikiri kwa undani kwani waonyesha kukata tamaa lakini amini nakuambia hiki tukiongeacho hapa kina maana kubwa sana.

Bado naamini machafuko si njia sahihi bali njia za kawaida tu zatosha. Lakini kwanza tuna budi kuangalia hali ya kiuchumi ya upinzani je, wana hali gani kifedha? Shughuli za uendeshaji wa chama wahitaji fedha na mipango, je Chadema ina vyanzo imara vya fedha ambavyo huko mbele vitaweza kuwa mbadala wa ruzuku kutoka serikalini?

Fedha nyingi huelekezwa katika maeneo kama ya kidijitali na huko ndiko kwenye kukiimarisha chama lakini je ni kwa mtindo upi?

Ok, tuseme Chadema yaanza na uchaguzi wa serikali za mitaa hii ndo njia sahihi ya kujenga "base" ya viongozi wengi ambayo itasaidia kupatikana wabunge wengi kwa mtindo mmoja tu.

Sasa basi, wewe wataka kuwa diwani wa kata fulani lakini si mhuni, umesoma uzuri hadi chuo kikuu na ni lazima ushinde katika kata yako. Hivyo Chadema digital itaandaa "profile" ya mgombea, vipeperushi vinavyomuongelea mgombea na mwisho sera zake zote anoziuza kwa wapiga kura. Hali ni hiyohiyo kwa wagombea ubunge na hiyo si tu bila mkutano wa halaiki bali vipeperushi vyenye ujumbe tosha kwa mpiga kura.

Hizi ni hatua ambazo zapaswa kutekelezwa mwanzoni katika ya upigaji kura ya maoni na namna ya kuufikisha ujumbe kwa wananchi kulinganisha sera au ilani ya CCM na ile ya kwenu, wapi CCM wameshindwa na ninyi au mgombea wenu atafanya nini tofauti.

Hii hatua ya Chadema UNGANISHA au "connect" ni hatua ambayo ikifika kwa walengwa mgombea anakuwa hana shida ya kujitambulisha maana tayari ajulikana kabla hata ya siku ya mkutano wa kampeni.

Mambo yaliyomo katika hii "Connect" au UNGANISHA ni pamoja na uchapaji, utumaji na uwasilishaji wa ujumbe ama kumtambulisha mgombea au kuweka msisitizo wa siku ya kupiga kura.

Hivyo katika eneo husika la kugombea udiwani au ubunge kipeperushi maalum kinachomhusu mgombea kwamba yeye ninani, na ana sera zipi na taarifa zingine atapewa mpiga kura ili achambue.

Asikwambie mtu, hakuna siri kubwa ya kupiga kura kama utumiaji wa sanduku la kura hivyo kwenye hili mbinu kadha wa kadha huitajika ili kuhakikisha wingi wa kura unaleta hofu kuu kwa watawala na DS yao.

Mbinu ingine ni ile ya mvuto na kusajili wanachama katika kila kata kwa kutumia mfumo wa kidijitali na sio kukusanya panyaroad mitaani na wahuni wengi ambao wataviuruga mrindimo wa kisiasa. Hivyo Chadema Digital yapaswa kuweka platform ndani ya tovuti yake ambayo itasajili wanachama wapya kwa kutumia Chadema Digital App ili kusajili vijana au kuwatambua na kuwafanyia uhakiki wale "grassroots" wote ambao ndo nguzo muhimu ya uimarishaji na uhamasishaji.

Eneo hili la Chadema Digital CDM hawajalitendea haki kwani bado tovuti yao imejazwa mipicha tuu kila kona badala ya mambo mengine muhimu sana katika ulimwengu wa mitandao.

Sasa nimalize kwa kusema zipo njia nyingi zaidi ambazo hata wewe bado huzifahamu na labda mwenyekiti Mbowe atanielewa, kuna "Doorstep App", kuna "contact creator" nyakati za kampeni na pia kuna "Word Press Network". Hizi ni zile za kuingia ndani zaidi kumpata na kumshinda mtesi wako.

Tuendelee ntazungumzia kiaina maana hizi ni mbinu na huwezi kuweka mbinu hadharani.
 
Back
Top Bottom