MJADALA: Maswali, majibu na ushauri kuhusu Kilimo cha Mpunga cha kitaalam pamoja na masoko yake

Akitaka kuondoa shilingi, Mhe.Msnyika anashauli kufumua bajeti ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kwa kile anachodai kuwa bajeti hiyo imetenga fedha nyingi kwenye mafunzo na posho badala ya kwenda kwa wakulima.

Mhe. Halima Mdee na Machali wanasema ni aibu kwa kilimo kukua kwa asilimi 4 wakati kuna fedha nyingi zinatengwa kwenye utafunaji.

Sina hakika kama wabunge wa Upinzani wanajua wanachochangia. Mhe. Waziri wa Kilimo anaummuliza Mhe. Machali kama anajua "Systems of Rice Intensification" (teknolojia ya kilimo shadidi cha mpunga).

Ni wazi kuwa hakuna mtu yeyote anayezaliwa anajua chochote. Pia kila anayejua jambo flani huwa si kweli kuwa anajua mabo yote. Hata huyo anayefikiri yeye ndiye anyejua vizuri kilimo sidhani kama anajua kama nguruwe anazaa mara ngapi kwa mwaka!

So kuuliza swali kama hilo, kwa mtu mwelewa ni kutangaza ujinga wako hadharani kwamba wewe unaua kila kitu, wakati hata mjinga anajua kuwa hata mwenye akili hajui kila kitu!

Kwa upande mwingine, ni kweli kuwa bajeti inakuwa ya kipumbavu, kama fedha zinazoelekezwa kwenye semina na posho ni nyingi kuliko zinazoenda kwenye mambo mengine kama pembejeo na huduma za wakulima. Kwa kifupi nakusudia kusema kuwa ni bajeti za aina hii ndiyo zilizofikisha kilimo hapa kilipo. Binafsi nimefanya uchunguzi na naweza kusema tena bila hata kupepesa, kuwa mabwana shamba wanaowasaidia wakulima ni wachache sana. Katika mia labda mmoja au usipate kabisa. na pia utashangaa kuwa hata hapa mjini kuna mabwana shamba na mabibi shamba wakati kila mtu anajua mjini hakuna mashamba!

Kwa hali ilivyo sasa, kama nchi ingekuwa na viongozi wenye akili na makini ( namaanisha walioko sasa ni dhaifu, mafisadi, wapumbavu na wezi), Wizara ya kilimo ingeshafutwa kabisa kwani hakuna inachosaidia zaidi ya kutia hasara nchi. Hali kadhalika fedha zote zinazoenda kwenye wizara hiyo zingetafutiwa sehemu nyingine ya kwenda kama afya au elimu hii ikiwa ni baada ya kuondoa mawaziri hawa wa sasa ambao hata mbuzi wangu amewazidi akili, hekima na busara.(Mtanisamehe...inaniuma sana)

Kwa mtindo huo, kama bajeti hii siyo ya kijinga ni bajeti ya aina gani?
 
Asante kwa ushauri.

Mbali na kununua mpunga na kuuza, je, nikiamua kulima mpunga itaniletea faida?

helow neane mie natafuta ni nunue mchele asa naweza kupata naombaa uni tumie msg au whtsap number yangu 0768385006 ni muhimu sana nakuombaa
 
Kabla ya kuanza hiyo biashara fanya utafiti wa kutosha kwa kutembelea masoko makubwa ya Mchele I mean Tandale na Tandika. Pia zungukia unakopatikana huo Mchele itakusaidia kufanya maamuzi sahihi. Ila kwa biashara ya mpunga Tz kwa sasa ni bahati na sibu wengi walioingia kichwakichwa wamelizwa. Usitupe huko mtaji mkubwa (wote). Kila la heri ndugu.
 
habari yako mkuu kama wewe una mazao ya kulima ya maharage alizeti mpunga naomba tuwasiiliane number 0768385006 nitakuwa nachukua mzigo kwakoo
 
Katika hili nataka kujua tangu kuanza kupanda Inakuwaje! Mbolea aina gani inatakiwa,km ni dawa za aina gani,na Ipigwe wakati gani.namna yakupanda Umbali uweje kati ya Shina na Shina na kati ya Mstari na Mstari kwa Ujumla namna yakuhudumia SHAMBA kitaalamu ili mtu apate mavuno BORA wataalam karibuni!

Ikiwa unataka kulima large scale na hujawahi kulima ni vyema kupata extension officer akakuelekeza sawa sawa ni aina gani ya mbegu unahitaji kupanda. Jee unahitaji mbegu za kizamani (traditional) au za kisasa (improved)?.

Matumizi ya mbolea kwa aina hizi mbili za mbegu yanatofautiana. Vile vile aina ya udongo uliopo unaweza kuwa na mahitaji tafauti ya mbolea.
 
Mkuu ssl Endelea kubarikiwa thnx! kwa mwongozo! Ila bado nina maswali machache! DAP na UREA naweka wakati gani Shambani or Kwenye kiTALU kipimo chake? Kupandikiza kati ya mstari na Mstari na shina hd shina Umbali uweje? Hii mbegu ya TXD 306 ndoile wanaita Mbegu KUBWA inayolimwa kuanzia January? Inatofauti naile ya zamani wanaiita SUPER? ambayo chakula chake kinakuwa na Harufu nzuri? hz Mbegu KUBWA ziko zaaina ngapi? naweza kujua pia tabia zake? Natanguliza shukrani ndgu karibu kwa ELIMU!

Ijapokuwa siyo mimi uliyeniuliza lakini baadhi ya majibu yako ni kama yafuatavyo:

Standard spacing ya mpunga ni 20cm by 20cm ndiyo unapata optimum population. If you are serious get a small transplanter na hasa kwenye eneo lenye maji.

Mbegu kubwa ni zile za kienyeji akina jamii ya Supa, Kula na bwana, Shingo ya mwari na aina nyingi zaidi ya hamsini mdogo wangu. Hizi zinapandwa mwezi wa January au hasa Disemba baada ya Krismas na zinachukuwa muda mrefu (5 - 8 months), ziko photoperiod sensitive (ubebaji mimba wake unategemea masaa ya jua - daylight hours) na uzazi wake siyo mwingi sana lakini zina harufu nzuri (aromatic).

Mbegu fupi ni zile za kama miezi mitatu mpaka minne, zinawekewa mbolea nyingi kwa vile zinazaa sana (improved kama hiyo TXD), hazina photoperiodicity lakini kwa asilimia kubwa hazina harufu (non aromatic).

Aroma na yield huwa havikai pamoja genetically.

Natumai taarifa hii itakuwa imekusaidia kwa kiwango fulani.

Mimi nimefanya kazi kwenye utafiti wa mpunga kwa zaidi ya miaka kumi.
 
majibu mbona hayakuletwa yapata miaka 3 sasa toka huu uzi uwekwe humu na kuahidiwa majibu
 
Ukweli ni kwamba bado tupo shambani ingawaje changamoto kubwa ni hizi mvua ambazo huwezi kujua kiwango chake wala exactly lini zikakuja mwaka wa kwanza mvua zilikuwa nyingi kupita kiasi na ni wakati tunakaribia kuvuna hivyo mpunga ukazama kwanye maji ingawaje mtaji ulirudi, mwaka wa pili mvua zikawahi kabla hatujamwaga mbegu hivyo pia hakukuwa na matokeo mazuri mwaka huu nafikiria kilimo cha umwagiliaji so najipanga kama nitaweza kwenda kapunga ingawaje nako kuna unyonyaji Fulani hivi so Karibu
 
Ukweli ni kwamba bado tupo shambani ingawaje changamoto kubwa ni hizi mvua ambazo huwezi kujua kiwango chake wala exactly lini zikakuja mwaka wa kwanza mvua zilikuwa nyingi kupita kiasi na ni wakati tunakaribia kuvuna hivyo mpunga ukazama kwanye maji ingawaje mtaji ulirudi, mwaka wa pili mvua zikawahi kabla hatujamwaga mbegu hivyo pia hakukuwa na matokeo mazuri mwaka huu nafikiria kilimo cha umwagiliaji so najipanga kama nitaweza kwenda kapunga ingawaje nako kuna unyonyaji Fulani hivi so Karibu
hongera mkuu kwa kutokata tamaa. lakini unaweza dadavua ulilima ekari ngapi?, ulipata gunia ngapi? na bei ya kuuzia?.
 
Kubota,
Safi sana mkuu kuna watu kazi yao kukatisha tamaa hawana jema wanaloweza sema kazi ni kukandia na kukosoa tu...nitakapokuwa tayari nitaku-pm na mimi nataka nilime mpunga....kulima tutalima hata kama mnatukatisha tamaa tutalima tu cha msingi kutafuta wataalamu na watu wenye uzoefu ili upate elimu na msaada wa kitaalamu...ukifuata ushauri wa kitaalam ikiwemo kutokuuza mpunga bali mchele lazima utafanikiwa tu.big up kubota.
 
Ndugu habarini za muda huu.

Shida yangu ni moja tuu, ningependa kujua kilimo cha mpunga hususani idadi ya magunia ninayoweza kuvuna katika eka moja, na gharama zake kwa pamoja, na je soko la zao la mpunga kwa sasa hapa Tanzania
 
Habari wadau wenzangu wa Jamii Forum, naomba maoni yenu juu ya kilimo cha zao la mpunga. Napenda pata mawazo yenu juu ya suala zima la kilimo cha mpunga katika kujikwamua kimaisha, nimepata kiasi kidogo cha mkopo nataka peleka katika kilimo ili maisha yaweze songa mbele. Mchango wenu wadau.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom