Makala Jr
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 3,395
- 1,110
Ni siku chache tokea wakuu wa wilaya walipokula kiapo cha uaminifu wa kuwatumia wananchi wote pasipokujali itikadi za wananchi husika. Cha kushangaza, leo hii Waziri mkuu, mhe.Mizengo Pinda a.k.a mtoto wa mkulima (asiye na shamba) amesema ni sahihi kwa wakuu wa wilaya kuinadi ccm (kama makatibu wenezi) wanapokuwa wilayani haswa katika mikutano ya hadhara.
Alipokuwa anajibu swali la Mb.Ezekiel Wenje kuhusu uhalali wa wakuu wa wilaya kukinadi chama wakati wanatumia kodi za watanzania wote kupitia mishahara,usafiri na posho wanazopewa Wakuu hao. Kwa mtazamo wa mtendaji mkuu wa serikali Mhe.Pinda aliyedai ni sawa kunadi chama na kuelezea utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi kinachokimbiwa na wanachama kila kukicha.
Baadhi ya wananchi niliowahoji mjini Mbeya...wamesema hawana imani na wakuu wa wilaya wakiwa kama Wakuu wa ulinzi na usalama wilayani kwani hawawezi kusimamia haki panapo matatizo kwa kuwa wanafungamana na chama cha (zamani).Katiba mpya itutatulie utata huu.
Alipokuwa anajibu swali la Mb.Ezekiel Wenje kuhusu uhalali wa wakuu wa wilaya kukinadi chama wakati wanatumia kodi za watanzania wote kupitia mishahara,usafiri na posho wanazopewa Wakuu hao. Kwa mtazamo wa mtendaji mkuu wa serikali Mhe.Pinda aliyedai ni sawa kunadi chama na kuelezea utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi kinachokimbiwa na wanachama kila kukicha.
Baadhi ya wananchi niliowahoji mjini Mbeya...wamesema hawana imani na wakuu wa wilaya wakiwa kama Wakuu wa ulinzi na usalama wilayani kwani hawawezi kusimamia haki panapo matatizo kwa kuwa wanafungamana na chama cha (zamani).Katiba mpya itutatulie utata huu.