Misemo inayoandikwa kwenye vyombo vya usafiri, we acha tu!

Ukitaka kuliwa sharti na wewe uliwe
No pain no gain
Nioshe
Ni mtazamo tu.
Raha jipe mwenyewe..
Maji ukiyavulia nguo sharti uyaoge..
Mwanzo mgumu..
Kufa kufaana..
Ukitaka upakatwe...
Hapa stori tu,kula kwenu...
Alfa na omega...
 
Hata ukinawa huli
hapa story tu kula kwenu
Shose sha luwa
Sha ruwa shifoi
fukuza upepo
nipite nitakukuta
Mskini halali mchana
Igembe nsabo
Shule ya mjinga majungu
 
Chochote wasemacho
Na kile wakisikiacho
Muhimu ni walionacho
Kiwatiao wengine kicho

Nikija kukiandika jicho
Kiwe ni kile nitakacho
Basi sikiachi hicho
Kwani ndicho kinifurahishacho
 
Kunya lazima kuchamba hiari'....nimeyakuta kwenye choo cha kulipia stand kuu Iringa.
 
1. Mwisho wa ubaya aibu
2. Hata mbuyu ulianza kama uyoga
3. Nibora kuishi na nyoka pangoni kuliko kuishi na mwanamke mkorofi
4. Kuwa mkweli leo ili usiadhirike kesho
5. Iga ufe
6. Kunya kanya kuku bata akinya kaharisha
7. Kesi ya nyani kapelekewa ngedere
8. Mwanamke kiuno makalio hata kwa mchina yapo
9. Baba kanikataza
10. Mali ni mateso
 
ukiona wenzio wanapepeta pumba we chagua chuya..........huu msemo niliuona kwenye Hiace umenikaa sana
 
KUNA HIZI PIA

Fukara hatabiriki -Bajaji

Lawama kwetu cheo - Kipanya

Usipovaa Bwana atatwaa - DCM

Jiko la shamba halichagui kuni

Maanta utuh(sina hakika na herufi zake) ikimaanisha Ubinaadamu kazi!

Uza nyuba jenga heshima baa

Kuna jamaa alilowea mjini na akawa anapata lawama nyingi kutoka 'home' kuwa haendi kusalimia, alipozichonga akanunua gali na kuliandika hivi 'Baleke bajobheke, Pambwani panyafu'. Guess alikuwa mutu ya wapi?
 
'Mti Mkulu ugwa ulanga wela'............... hapo nipe mji

Chilumbilwe na nungu chakumemena

Sema na mshua

......... ila ile ya 'tunakodisha kondomu naona kali kweli' yaani iende irudi.
 
Ni kweli muungwana misemo ya kwenye vyombo vya barabarani ni mingi na baadhi inachekesha. Yote uliyoiandika imo ila nitaongeza baadhi. Umekuwa mtindo kwa wenye mabasi na malori kuandika pia majina ya vitu au kitu kinachojulikana na wengi.Nakumbuka kwa mfano mwaka 1997-2000 wakati kituo cha ITV kinaonyesha tanthiliya ya EGOLI, mabasi kadhaa ya abiria Yalichora neno EGOLI kwenye bodi za mabasi hayo, hasa kwenye kioo kikubwa cha nyuma. Baadhi ya misemo mingine ni:

Kama kuoga ni usafi kwanini taulo huchafuka?
Kama waijua kaizibe
Wakati mwingine hata majina ya watu maarufu duniani hutumiwa sana.Nilishapata kuona mabasi yameandikwa:
Hans Blix
George Bush
Osama bin Laden
Sylvester Stallone
Arnold Shwaznagger nk

Baada ya miezi miwili usishangae kuona basi limeandikwa "Mafuriko ya Dar"

Naomba wengine wachangie
 
Na hii

neno.jpg
 
Back
Top Bottom