hahahahaha kweli huyu mchonganishiafu wewe mchonganishi nimekugundua lol
wadau naomba uzoefu wenu katika hili..
mke wangu ana mimba ya miez 6 sasa na ndo mimba yake ya kwanza. amepunguza mapenzi kwangu japo si saaana ila si kama zamani asiponiona atapiga simu weeee mpaka kero, siku hizi wala, nikichelewa nakuta keshalala wala hana habari na mim.
katika mimba yake hiyo ametokea kupanda kula miwa.. ebwana ikiksekana hakukaliki hom. huwa na kawaida ya kupitia miwa pale mwenge na kumpelekea kila siku. maana ukinunua mingi ukaweka kwenye frij hataki et iaisha utam (ilimradi visa tu)
sasa jana nilichelewwa kurudi kutoka job, kupita mwenge miwa hakuna, zunguka mpaka ubungo hakuna, ikabidi mwanawane kirud hom tu, kufika tu nikajitetea kuwa nilichelewa kurudi nikakosa miwa..,
weeee, aliporomosha matusi mpaka hasira, nikamwacha aongee tu maana nilimbembeleza anisamehe nitaitafta kesho maana ilikuwa saa nne tayari hakunielewa. mpaka akamwaga maji kitandani eti nisilale mpaka miwa ipatikane..,
basi nilizunguka mpaka saa 6 ndo nikaipata buguruni, hapo tuligonga hdi muuzaji keshalala nikidanganya nataka ya kutengenezea dawa.
jaman kuweni na huruma japo kidogo...., hivi baada ya mimba atabadilika kweli au ndo atabadilika mazima my wife wangu!!!...., naumia sana, kuna vituko kibao ila cha jana ndo kiboko...
nawasilisha.
itajitahidi mkuu, alilowanisha kitanda eti nisilale mpaka miwa ipatikane.., niliporudi na miwa aliniomba msamaha kwamba ilikuwa ni hasira tu, nikalala kwenye kochi mwanawane...Mhhhh! Pole sana!!! sasa hilo la kumwagia maji kitandani hata haliingii akilini. Wengine wenye bahati zao ujauzito huwa bomba tangu mwezi wa kwanza hadi kujifungua. Vumilia tu imebaki miezi mitatu tu ila hakikisha hata siku moja husahau miwa tena.
itajitahidi mkuu, alilowanisha kitanda eti nisilale mpaka miwa ipatikane.., niliporudi na miwa aliniomba msamaha kwamba ilikuwa ni hasira tu, nikalala kwenye kochi mwanawane...
nimevumilia na nitaendelea kuvumilia, na ham sana ya kubeba katoto.., namuomba sana mungu anitie nguvu katika hili.niwe mkweli kwako mimba inaleta hasira za haraka na kutamani vitu vya ajabuajabu na maamuzi ya kijinga kwa baadhi ya wanawake,jaribu kumuelewa kwa kipindi hiki na usitegemee mapenzi makubwa kwani anakuwa na uchovu .jitahidi sana kuwahi na kama umeona ana hasira na maamuzi ya ajabu jitahidi kutokumtega na chochote.kila la kheri mweshimiwa ukipata mtoto utushirikishe tukupe hongera.
asante sana mkuu kwa kunitia moyo, i cant wait to hold my own baby..ahaaa! Kumbe alielewa alichokifanya hakikuwa sawa. Utayasahau maudhi yote haya na pale utakamposhika mwanao kwa mara ya kwanza utajawa na furaha isiyo kifani. Mkikumbuka haya miwa na mengineyo yaliyosababishwa na ujauzito huu mnaweza mkawa mnacheka tu. Kila la heri kwenye ujauzito wenu.
Kuna jamaa alikurupushwa saa nane za usiku mkewe kamwambia anahitaji matango jamaa akabanwa kweli ikabidi akapige hodi kwa muuza matango kwa bahati nzuri akapewa!
Kuyaleta nyumbani akaambiwa ayakatekate kisha ampe akae nayo awe anayanusa maana anapenda harufu yake!
Chezeiya mimba wewe!