Mikasa iliyowahi nikuta baharini

LA7

JF-Expert Member
Aug 26, 2019
457
1,746
Nahodha akanipigia kelele kwa sauti kwamba nizame chini kwamba mwenzangu amechoka niende kumsaidia na kweli nilivo mtazama alikuwa akiniita kwamba niende,

Naam natumaini humu wote hamjambo humu pia niwashukuru hawa jamiifurm kwa kuendelea kupeperusha nyuzi zetu hewani

Tukianza moja kwa moja kuhusu mambo yaliyonikuta nikiwa nafanya kazi za baharini

Nakumbuka nilipofika kwa mara ya kwabza msasani beach nilikuwa sijui hata kuogelea ila nilianza kujifunza kwa kujifunga chupa za maji ya lita moja na nusu miguuni na mikononi mpaka nikawa nimejua kuogelea kabisa, sasa tukianza na mkasa wa kwanza,

Siku hiyo tulienda kuvua uvuvi wa kuzamia chini au wanaita kokoro yaani hiyo nyavu huwa ikisha zungushwa kweny maji chini huwa haiachi kitu, sasa tukisha tupa nyavu chini ile nyavu inakuwa na kamba kwa bande mbili wakati tunaanza kuidondosha tubapoanzia kuidondoshea tunaacha alama ya boya tunaweza izungusha raundi kama kilometa moja hivi mpaka tunakutana tena na lile boya tunakuwa wastani wa watu kuanzia 12,

Sasa tunachukua lile boya tunalivuta mpaka tunaishika ile kamba tunaanza kuvuta kila upande halafu kuna watu wanajitosa majini wanaenda mpaka kule katikati kwenye nyavu wanakuwa wanatuelekeza ili kuivuta kwa usawa,

Pia kwaajili ya kuitoa inapotokea imenasa kwenye mawe maana ile kamba huwa ina zama chini kabisa ardhini ili kuwastua wale samaki hasa pono kukimbilia katikati,

Na inapo karibia karibu na boti tunashuka kwenye maji watu watatu au wanne ili kuwazuia wale samaki warudi kwenye nyavu, na pale katikati ya nyavu huwa tumeitoboa na kushonea likitu kama mfuki hivi, ambapo tundu lake limerudi kwa nyuma kama shimo,

Sasa siku hiyo nahodha akaniambia nishuke kwenye maji ili tukawazuie samaki tulivoshuka mtu 3 tuaenda wakwanza akaenda chini akawazuia wakati sisi huku juu tumevaa vioo vya kutazama na tunamtazama akikaribia kuishiwa pumzi anatuita kwa ishara sasa alivoita yule mwenzangu akaenda,

Pia na yeye alivochoka akaniita muda huo huko juu ya boti wanakazana kuvuta nyavu kwa kasi sana,

Nikazama chini yeye akapanda juu nikawa nawazuia samaki walikuwa wengi tu wakawa wanakimbilia kwenye hilo shimo nilivoona nimechoka nikamuita jamaa aje nikapanda juu kutema mate hivi nikashangaa natema damu, kwakweli hiyo ndo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuzamia kina kirefu hivo nahodha akanimbia nirudi tena kule chini ili tukawafungie hao samaki nikawa tu nimeshikilia kulikuwa na boya ambalo huwa linafanya nyavu isimame,

Kutazama chini jamaa ananiita niende aaa wapi ikawa ngumu muda wote huo bado natema damu tu nilipatwa na hofu sana japo tulifanikiwa mzigo ukawa umepanda juu, mimi ndo nilikuwa mdogo kuliko wote humo japo nahodha alikuwa ananielewa sana,

Lakini sikumwambia mtu yoyote kilicho tokea nashukuru mungu alinisaidia ila ndo ikawa mwanzo na mwisho kuzama kina kirefu hivo,

Ipo mikasa mingi ila nimmeanza na huoo ipo mingine ikiwemo

Kuvua samaki wengi mpaka tukawamwaga wengine maana tungezama

Kutumia siku mbili kutoka msasani mpaka bandarini tukiwa tumevuta chuma la kujengea madaraja lipo kama box mpaka kupata ajali ya kugongana na boti la kubeba mzigo

Kupinduka bongoyo na msanii mwigizaji lucy komba

Tuishie hapo kwanza
 
kwa mara ya kwanza tulitaka kuexperience usafiri wa majini kupitia kipumbwi

sikua najua usafiri wa huko ni wamajahazi, walikua wanatumia msamiati wa neno "chombo" mimi nikijua ni aina flani ya meli nabhata skujisumbua kujua chombo ni kipi


safari haikua mbaya had kufikia pangani kizaazaa kikaanza kuvuka pale na pantoni ikalala upande tulokua tumekaa wee nilipiga kelele naona watu wote waanitolea macho, mimi hapo ni yarabi tusitiri tuvuke, Allah akbar, subhanallah, astaghfirllah yan nilileta dhakari ambazo sijawah kufanya tangu nazaliwa tulifika kwa mbinde yan ile pantoni ilikua inavutana na maji naupepo

tukaelekea kipumbwi tulifika kama saa kumi jioni hoi hapo tukaulizia usafiri, nauli na taratibu zingine. Kweli tukalipa nauli pale kusubiri safar kuulizia hilo jahaz linaondoka saa tisa alfajiri kuelekea zenji - Mkokotoni, tukajiambia na mama hapa tutanyooka na njaa wasafiri wenzetu wakaanzisha utaratibu wa kuchangisha hela za kujipikilisha palepale kweli tukapika ugali wetu na kachumbari samaki ni kama wote yan bei chee nilikula ugali kwa uchu wa samaki tukalala nje na mizigo yetu yan kwa mara ya kwanza nalala nje kwenye mkeka ilipofika mda tukaamshwa haya amkeni wasafiri muda umewadia tukaamka kwenda baharini hammadi nafika nakuta mpaka kulifikia hilo jahaz mnafaulishwa na vijimashua vijidogo dogo sisi tulikua abiria wa mwisho kufaulishwa nakumbuka kitendo cha kuingia kwenye jahaz nilining'inia miguu iko chini mikono imeshikilia jahazi, dude lenyewe lilikua refu nikavutwa hapo nishachanganywa akili,nawaza hiki ndio chombo?? jamani tunakufa leo! najuta mimi nimekifata kifo bila kujua, yan majuto nafs inaniuma safa ilianza nilioga maji s kawaida, nililoa mno halaf tulifika huko katikati majini lile jahaz lilikua sawasawa na maji means kina ni kirefu nikiangalia mbele naona wingu limeshikana na maji pembeni hivohivo tulikotoka hamna hata kibanda ni maji kotekote sitakaa nikasahau mpaka nakufa wallah ,nilitapika mpaka niliishiwa nguvu kibaya zaidi mkitapika mnapewa huduma ya mifuko ukimaliza unaurusha baharini huko,


tulifika salama lakini nilimwambia mama kama usafiri wa kurudi ni huu utarudi mwenyewe mimi utaniacha unguja


salute sana wavuvi, mnarisk sana maisha yenu, bahari inatisha mno mno mimi mpaka leo hata nikipanda meli tukifika mkondoni lazima nilegee sembuse wewe unaezamia kuna mtu aliangusha mshipi alikua mzoefu tu et akashuka kuufata ikawa fatiha madaraka, alikutwa mikokoni amefariki.
 
kwa mara ya kwanza tulitaka kuexperience usafiri wa majini kupitia kipumbwi

sikua najua usafiri wa huko ni wamajahazi, walikua wanatumia msamiati wa neno "chombo" mimi nikijua ni aina flani ya meli nabhata skujisumbua kujua chombo ni kipi


safari haikua mbaya had kufikia pangani kizaazaa kikaanza kuvuka pale na pantoni ikalala upande tulokua tumekaa wee nilipiga kelele naona watu wote waanitolea macho, mimi hapo ni yarabi tusitiri tuvuke, Allah akbar, subhanallah, astaghfirllah yan nilileta dhakari ambazo sijawah kufanya tangu nazaliwa tulifika kwa mbinde yan ile pantoni ilikua inavutana na maji naupepo

tukaelekea kipumbwi tulifika kama saa kumi jioni hoi hapo tukaulizia usafiri, nauli na taratibu zingine. Kweli tukalipa nauli pale kusubiri safar kuulizia hilo jahaz linaondoka saa tisa alfajiri kuelekea zenji - Mkokotoni, tukajiambia na mama hapa tutanyooka na njaa wasafiri wenzetu wakaanzisha utaratibu wa kuchangisha hela za kujipikilisha palepale kweli tukapika ugali wetu na kachumbari samaki ni kama wote yan bei chee nilikula ugali kwa uchu wa samaki tukalala nje na mizigo yetu yan kwa mara ya kwanza nalala nje kwenye mkeka ilipofika mda tukaamshwa haya amkeni wasafiri muda umewadia tukaamka kwenda baharini hammadi nafika nakuta mpaka kulifikia hilo jahaz mnafaulishwa na vijimashua vijidogo dogo sisi tulikua abiria wa mwisho kufaulishwa nakumbuka kitendo cha kuingia kwenye jahaz nilining'inia miguu iko chini mikono imeshikilia jahazi, dude lenyewe lilikua refu nikavutwa hapo nishachanganywa akili,nawaza hiki ndio chombo?? jamani tunakufa leo! najuta mimi nimekifata kifo bila kujua, yan majuto nafs inaniuma safa ilianza nilioga maji s kawaida, nililoa mno halaf tulifika huko katikati majini lile jahaz lilikua sawasawa na maji means kina ni kirefu nikiangalia mbele naona wingu limeshikana na maji pembeni hivohivo tulikotoka hamna hata kibanda ni maji kotekote sitakaa nikasahau mpaka nakufa wallah ,nilitapika mpaka niliishiwa nguvu kibaya zaidi mkitapika mnapewa huduma ya mifuko ukimaliza unaurusha baharini huko,


tulifika salama lakini nilimwambia mama kama usafiri wa kurudi ni huu utarudi mwenyewe mimi utaniacha unguja


salute sana wavuvi, mnarisk sana maisha yenu, bahari inatisha mno mno mimi mpaka leo hata nikipanda meli tukifika mkondoni lazima nilegee sembuse wewe unaezamia kuna mtu aliangusha mshipi alikua mzoefu tu et akashuka kuufata ikawa fatiha madaraka, alikutwa mikokoni amefariki.
Hizo adhkar, umenikumbusha mwaka jana mwishoni nilipata ajali ya gari, moja ua watu niliokuwa nao ni dada yangu, baada ya ole ajali alileta adhkar si mchezo na kwa sauti kubwa mnoo, mpaka watu wanamshangaa, sie tunapiga za chini chini(moyoni) ye anapiga kelele ai mchezo, kiasi nikahisi ndugu yangu madubwasha umempanda au kapagawa 😂

Kifo kinatuogopesha soote.
 
Hizo adhkar, umenikumbusha mwaka jana mwishoni nilipata ajali ya gari, moja ua watu niliokuwa nao ni dada yangu, baada ya ole ajali alileta adhkar si mchezo na kwa sauti kubwa mnoo, mpaka watu wanamshangaa, sie tunapiga za chini chini(moyoni) ye anapiga kelele ai mchezo, kiasi nikahisi ndugu yangu madubwasha umempanda au kapagawa 😂

Kifo kinatuogopesha soote.
😂😂😂 we acha mimi mpaka leo najiuliza hio spirit na kupanda hilo dude niliwezaje wakat nilikua na uwezo wa kuicancel hio safar nikarudi nyumbani kuna muda hua nikikumbuka najicheka kama mjinga mana unamkumbuka Mungu ukiwa upo ndani ya shida
 
we acha mimi mpaka leo najiuliza hio spirit na kupanda hilo dude niliwezaje wakat nilikua na uwezo wa kuicancel hio safar nikarudi nyumbani kuna muda hua nikikumbuka najicheka kama mjinga mana unamkumbuka Mungu ukiwa upo ndani ya shida
Bahari inatisha sana, sijawahi fikiria kupanda yale majahazi kabisa,kuogelea kwenye hata maji ya kifua,huwa natoa macho
 
Bahari inatisha sana, sijawahi fikiria kupanda yale majahazi kabisa,kuogelea kwenye hata maji ya kifua,huwa natoa macho
vipi beach hua unaenda?? mimi napenda ile view yan niko nchi kav naiangalia bahar kwa umbali napenda sana nikiwa na safar ya zenji lazima nikase roho mara ya mwisho hata mtoto nilishindwa kumshika nikampa mama hapo nipo ya azam marine yan meli inakokota navurugika tumbo jamani ni hao ndugu wananipeleka ukiacha nakuipenda zanzibar vinginevyo nisingesafiri na meli kamwe
 
Humu siku hizi sijui pakoje yaani!!..pamegeuka kijiwe Cha 'mama na mwana'..tatizo waliokua form two 2017 wamekuwa wengi humu!!
 
Back
Top Bottom