Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,396
- 7,968
Kitendo cha waziri wa miundombinu Mh Mwakyembe kutoa miezi mitatu kwa shirika la ndege kuanza kujiendesha ni uendawazimu. Ni sawa na mwanaume ambaye hajaacha hela ya chakula nyumbani halafu anamwambia mkewe akirudi jioni akute wali kuku na Heinneken mbili za baridi...
Shirika lina ndege moja tu inayoruka, tena ya kukodi, shirika lina madeni kibao hadi Mwakyembe anawashauri kukwepa kwa kupitisha fedha za bima akaunti ya CHC, shirika lina wafanyakazi lukuki ambao halina fedha za kuwalipa mafao waende zao. Kwa msomi kama Mwakyembe angebuni namna ya kuliwezesha shirika kumiliki ndege, tena zinazoendana na soko la sasa sio zile dash 8 zao, ndio atoe muda angalau mwaka mmoja. Nina mashaka sana watu wa namna hii kuwa ndio washauri wa rais. Kwenye biashara akili nyingi, usimamizi halafu nguvu kidogo na siasa pembeni.
Shirika lina ndege moja tu inayoruka, tena ya kukodi, shirika lina madeni kibao hadi Mwakyembe anawashauri kukwepa kwa kupitisha fedha za bima akaunti ya CHC, shirika lina wafanyakazi lukuki ambao halina fedha za kuwalipa mafao waende zao. Kwa msomi kama Mwakyembe angebuni namna ya kuliwezesha shirika kumiliki ndege, tena zinazoendana na soko la sasa sio zile dash 8 zao, ndio atoe muda angalau mwaka mmoja. Nina mashaka sana watu wa namna hii kuwa ndio washauri wa rais. Kwenye biashara akili nyingi, usimamizi halafu nguvu kidogo na siasa pembeni.