Michuzi faster than Ivorians on Didier Drogba's wedding...

...
Hawa Ivorians kumbe wametuzidi sana kwenye fani ya web design.
Sidhani kama kuna ukweli wa hili. Tatizo letu taaluma zote zimeingiliwa na virusi vya ufisadi. Yaani hata webdesigners nao wanachoangalia ni maslahi yao tu (yaani wale humo humo) badala ya kufanya kazi kwa uadilifu!
 
Sidhani kama kuna ukweli wa hili. Tatizo letu taaluma zote zimeingiliwa na virusi vya ufisadi. Yaani hata webdesigners nao wanachoangalia ni maslahi yao tu (yaani wale humo humo) badala ya kufanya kazi kwa uadilifu!

A very interesting proposition indeed. Kwa hiyo unataka kusema talentedness, ingenuity and creativity are all being held back by ufisadi?
 
Sidhani kama kuna ukweli wa hili. Tatizo letu taaluma zote zimeingiliwa na virusi vya ufisadi. Yaani hata webdesigners nao wanachoangalia ni maslahi yao tu (yaani wale humo humo) badala ya kufanya kazi kwa uadilifu!

Pamoja na ufisadi nafikiri pia Watanzania tuna kasumba ya kuridhika na tulichonacho.
 
Sidhani kama kuna ukweli wa hili. Tatizo letu taaluma zote zimeingiliwa na virusi vya ufisadi. Yaani hata webdesigners nao wanachoangalia ni maslahi yao tu (yaani wale humo humo) badala ya kufanya kazi kwa uadilifu!

Kama ni ufisadi, hata Cote D'Ivoire umeshamiri, pengine kuzidi hata ule wa Tanzania (achilia mbali ufisadi kutisha kwenye nchi kibao za Afrika), lakini kiujumla utaona fani ya webdesign kwa Tanzania is relatively mediocre ukilinganisha na nchi nyingi za Africa (at least from my own subjective point of view)
 
Bato bandugu na bajamaa, pia mgao wa umeme unasaidia kuzorotesha mambo. Dowans etc ndo ufisadi wenyewe. Fani ya mtandao bila umeme ni ndoto za alinacha. Anyway, bado nina imani na watz katika uwezo wa mambo mengi, manaake uzalendo nao ni muhimu!
 
Nafikiri talents tunao tena wazuri tuu. Tatizo wamepoliticised talents zao. Njaa nazo zinachangia. Na sio kwa web designers au waandishi wa habari tuu. Hata kwenye fani nyingine kama wanamuziki na comedians. Nafikiri tuliona mengi kwenye kampenni za uchaguzi uliopita.
 
Nafikiri talents tunao tena wazuri tuu. Tatizo wamepoliticised talents zao. Njaa nazo zinachangia. Na sio kwa web designers au waandishi wa habari tuu. Hata kwenye fani nyingine kama wanamuziki na comedians. Nafikiri tuliona mengi kwenye kampenni za uchaguzi uliopita.

Sasa kwenye private, not for profit, individual level, hizo politics na na njaa zinazozuia creativity zinatoka wapi? Achilia mbali for-profit private sector, ambao wanatumia ready-made webdesigns, templates etc kutoka nje. Ungeniambia kwamba fani ya webdesign na teknolojia nzima ya internet bado haijakomaa vilivyo kutokana na uduni wa infrastructure nzima wa Internet (ikiwamo upatikanaji wa umeme) na mapungufu ya elimu husika, ningekubali. Lakini to blame it on ufisadi tena? It sounds too far fetched kwa kweli.

Mfano, nenda website ya Muhimbili hapa http://www.mnh.or.tz/ ni aibu tupu!
 
Nafikiri talents tunao tena wazuri tuu. Tatizo wamepoliticised talents zao. Njaa nazo zinachangia. Na sio kwa web designers au waandishi wa habari tuu. Hata kwenye fani nyingine kama wanamuziki na comedians. Nafikiri tuliona mengi kwenye kampenni za uchaguzi uliopita.
Nakubaliana na uyasemao. Manaake nakumbuka mwaka 1969 tuliishangilia Yanga sana (sintosahau) ilipofika robo fainali ya kombe la Africa walipocheza na Asante Kotoko ya Ghana. Wakati ule tulikuwa na wachezaji kama Salehe Zimbwe, Maulidi Dilunga na Kitwana Manara. Kiwango cha soka kilikuwa juu sana lakini baada ya TANU kulazimisha kwenye kila timu kuwepo na tawi la chama (kuchanganya michezo na siasa) fani ya michezo yote ilianza kuzorota (mid-70's).

Vile vile katika fani ya muziki watemi na magwiji kama Mbaraka Mwinshehe (Morogoro Jazz na mtindo wa Likembe Mahoka), Shem Karenga (Tabora Jazz na mtindo wa Segere Matata) au hata Wema Abdallah (Western Jazz na mtindo wa Saboso) waliwatetemesha wakongo hata wengine walianza kuwaiga akina Wema na Mbaraka (kitu kilichokua ni maajabu enzi zile). Lakini baada ya bendi kulazimishwa waanze kuimba nyimbo za kisiasa ili waweze kurekodiwa au kurushwa hewani na RTD fani ya muziki ilianza kudidimia na kuporomoka.

Kwa hiyo ukweli ni kwamba vipaji Tanzania vipo, tena vingi, lakini mfumo mzima wa jamii bado una mushkeli. Kipaji cha ufisadi ndio kinachopewa kipaumbele kwa hivi sasa na sio kipaji cha kitaaluma!
 
Nakubaliana na uyasemao. Manaake nakumbuka mwaka 1969 tuliishangilia Yanga sana (sintosahau) ilipofika robo fainali ya kombe la Africa walipocheza na Asante Kotoko ya Ghana. Wakati ule tulikuwa na wachezaji kama Salehe Zimbwe, Maulidi Dilunga na Kitwana Manara. Kiwango cha soka kilikuwa juu sana lakini baada ya TANU kulazimisha kwenye kila timu kuwepo na tawi la chama (kuchanganya michezo na siasa) fani ya michezo yote ilianza kuzorota (mid-70's).

Vile vile katika fani ya muziki watemi na magwiji kama Mbaraka Mwinshehe (Morogoro Jazz na mtindo wa Likembe Mahoka), Shem Karenga (Tabora Jazz na mtindo wa Segere Matata) au hata Wema Abdallah (Western Jazz na mtindo wa Saboso) waliwatetemesha wakongo hata wengine walianza kuwaiga akina Wema na Mbaraka (kitu kilichokua ni maajabu enzi zile). Lakini baada ya bendi kulazimishwa waanze kuimba nyimbo za kisiasa ili waweze kurekodiwa au kurushwa hewani na RTD fani ya muziki ilianza kudidimia na kuporomoka.

Kwa hiyo ukweli ni kwamba vipaji Tanzania vipo, tena vingi, lakini mfumo mzima wa jamii bado una mushkeli. Kipaji cha ufisadi ndio kinachopewa kipaumbele kwa hivi sasa na sio kipaji cha kitaaluma!

Mifano mizuri sana, lakini ukumbuke zama za leo siyo zile za "kidumu" na "saboso", "sendemaa" etc,: lazima mifano iende na wakati bro. Nchi kama Angola na Msumbiji (na hata Uganda) zilizopata vita vya wenyewe vya muda mrefu na jamii kuharibika kwa kila namna, zimeshatupita mbali kwenye taaluma nyingi pamoja na ufisadi mkubwa uliokithiri MPLA na FRELIMO. Hiyo ni mifano miwili tu.
 
Mifano mizuri sana, lakini ukumbuke zama za leo siyo zile za "kidumu" na "saboso", "sendemaa" etc,: lazima mifano iende na wakati bro. Nchi kama Angola na Msumbiji (na hata Uganda) zilizopata vita vya wenyewe vya muda mrefu na jamii kuharibika kwa kila namna, zimeshatupita mbali kwenye taaluma nyingi pamoja na ufisadi mkubwa uliokithiri MPLA na FRELIMO. Hiyo ni mifano miwili tu.
Sikatai, lakini kufuta kasumba huchukua vizazi vingi. Kwa mfano, hadi leo hii bado tunayo kasumba ya ukoloni ingawa "tuliagana rasmi" na ukoloni miaka hamsini iliyopita. Vile vile athari za utumwa bado zinatuandama hata baada ya zaidi ya miaka mia nne.

Angalizo: Naona ka vile unataka kuiponda saboso na sendemaa eti imepitwa na wakati, haya bana. Aisee zama hizo ndio zilikuwa zenyewe basi. Hii mambo mbofu mbofu ya bongo fleva, sijui flava, sijui nini ni wizi mtupu. Jamaa hawaendi na vipaji, yaani ni mashine mashine kwa kwenda mbele. Mtu hajui hata kupiga gitaa au hata kuchanganya tumba eti anaibuka na kutangaza uanamuziki, wapi na wapi?
 
Sikatai, lakini kufuta kasumba huchukua vizazi vingi. Kwa mfano, hadi leo hii bado tunayo kasumba ya ukoloni ingawa "tuliagana rasmi" na ukoloni miaka hamsini iliyopita. Vile vile athari za utumwa bado zinatuandama hata baada ya zaidi ya miaka mia nne.

Angalizo: Naona ka vile unataka kuiponda saboso na sendemaa eti imepitwa na wakati, haya bana. Aisee zama hizo ndio zilikuwa zenyewe basi. Hii mambo mbofu mbofu ya bongo fleva, sijui flava, sijui nini ni wizi mtupu. Jamaa hawaendi na vipaji, yaani ni mashine mashine kwa kwenda mbele. Mtu hajui hata kupiga gitaa au hata kuchanganya tumba eti anaibuka na kutangaza uanamuziki, wapi na wapi?

Sasa hao Angola, Cote D'Ivoire, Mocambique etc, kwani wao hawana legacy ya utumwa, ukoloni, ukoloni mambomboleo na on top of it all, massively destructive civil warfare, genocide, tribal conficts etc na ufisadi mkubwa kwenye vyama tawala tokea uhuru ambao umezidi hata ule wa CCM, lakini wametupita kwenye taaluma mbalimbali, uchumi, na maendeleo ya jamii kwa ujumla?

By the way: "Sendemaa" na Vocalist wao, Mtoto Mzuri, Tshimanga Assosa, Chinyama Chiyaza et al (bila kuwataja Wanamuziki na bendi nyinginezo kibao za wakati huo) walikuwa wakinipa taabu sana enzi zile za 80's. Kila wakipiga Amana Club nillikuwa silali hadi usiku wa maanane kutokana na sauti kubwa kutoka maspika yao ya "Orange". Lakini "wana saboso" kwa kweli nilikuwa nawasikia tu kwenye kipindi cha "Zilipendwa" Radio Tanzania kila J'pili. Its all good though.
 
Sidhani kama kuna ukweli wa hili. Tatizo letu taaluma zote zimeingiliwa na virusi vya ufisadi. Yaani hata webdesigners nao wanachoangalia ni maslahi yao tu (yaani wale humo humo) badala ya kufanya kazi kwa uadilifu!
Hiyo isikushangaze kwa sababu nao wanaishi kwenye national culture. Katika Tz ukitaka excellence utagombana na watu wengi sana. Lakini hili si ajabu kwa sababu linaanzia vyuoni ambapo lengo la mwanafunzi ni kupata cheti na siyo elimu/utaalamu. Wanafunzi wengi wakiishahitimu chuo wanatangaza uadui na vitabu au kitu chochote ambacho ni source ya knowledge. Unategemeaje watoe quality products?
 
Back
Top Bottom