Miaka 3 ya Hayati Magufuli vs Miaka 3 Rais Samia madarakani

Rais Samia ametimiza miaka 3 tangu achukue madaraka ya urais lakini ukilinganisha na miaka 3 ya hayati Magufuli akiwa madarakani ni kama mlima na kichuguu kwa matokeo.
Rais Samia amefanya semina nyingi kwa mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi na wakuu wa mikoa lakini bado utendaji wa serikali yake uko duni sana! Matokeo baada ya semina hizo hayaonekani kabisa.
Rushwa, uzembe, mfumuko wa bei, kupandisha gharama za miradi, kuchelewesha miradi imekuwa ndiyo sifa kuu ya serikali ya Rais Samia.
Hayati Magufuli alijenga majengo ya wizara na kuhamishia serikali yote Dodoma ndani ya miaka 3 lakini Rais Samia kwa miaka 3 hakuna jengo hata moja lililokamilika kiasi cha kuanza kukaliwa na watu. Kwenye serikali ya Samia hamna mradi hata mmoja ulioanzishwa unaoweza kusema kwamba angalau hapa Kuna watu walikaa na kutumia akili.
Rais Samia amefanya vizuri sana kwenye ujenzi wa madarasa kwa kutumia mkopo wa fedha za Uviko.
Labda bado anaweka fedha mifukoni mwa watu kama ambavyo aliwahi kujinasibu.
Lakini kiukweli hali ya maisha ya siku hizi imekuwa changamoto sana. Ukienda dukani bei utakayoikuta asubuhi ni tofauti na utakayoikuta jioni, na kwa bahati mbaya vitu vinazidi kupanda tu bei na wala haijawahi kushuka toka aingie madarakani
 
Labda bado anaweka fedha mifukoni mwa watu kama ambavyo aliwahi kujinasibu.
Lakini kiukweli hali ya maisha ya siku hizi imekuwa changamoto sana. Ukienda dukani bei utakayoikuta asubuhi ni tofauti na utakayoikuta jioni, na kwa bahati mbaya vitu vinazidi kupanda tu bei na wala haijawahi kushuka toka aingie madarakani
Wafanyabiashara wameachwa wafanye wanavyotaka
 
Nonsense. Nilidhani utakuja kwa takwimu kumbe ni maelezo ya jumla. Tutajie kukua kwa pato la Taifa ongezeko la ajira miundombinu FDI . Mapato ya nchi. Demokrasia nk. Twende kwenye hizo parameters na njoo tena na ulinganishi mzuri
Wewe njoo na hizo takwimu kama unazo
 
Umeandika vizuri ukweli ni kwamba kwasasa hapa hakuna Rais zaidi ni bomu Tena la kienyeji.taarabu nyingi vitendo zero. Huwezi kupewa heshima na mungu ya kuongoza Watanzania halafu ukaishia kuwafilisi kwa kula starehe. Ondoka tuachie nchi yetu bana
Kwahiyo unakiri CCM imefeli ilihali kuanzia bunge hadi serikali zote ni za kwenu?
 
Wote ni CCM, wanafanya mambo ili kupata kura tu zinapokuja chaguzi...

Kuanzisha vitu na kushindwa kuvisimamia, ndio ugonjwa namba moja wa CCM...
 
Umeandika vizuri ukweli ni kwamba kwasasa hapa hakuna Rais zaidi ni bomu Tena la kienyeji.taarabu nyingi vitendo zero. Huwezi kupewa heshima na mungu ya kuongoza Watanzania halafu ukaishia kuwafilisi kwa kula starehe. Ondoka tuachie nchi yetu bana
Umeshapita Busisi ukaona kazi zinavyofanyika?

Huyu Mama amepambana haswa Mzee aliacha mamiradi makubwa utafikiri nchi inaenda kutoweka soon, mega projects kibao na bado human capital inatakiwa kuendelezwa, ajira mpya,mishahara kupanda, vyeo etc.

Mama amepambana haswaa hakuna alichoanzisha Mzee kimesimama. Hapa wenye roho mbaya mtakwepa kuusema huu ukweli.
 
CCM.jpg

Mama Anaupiga mwingi Masha-Allah
 
Shida ninayoiona kwa Samia ni hali ngumu ya maisha kwa watu wa hali ya chini hasa vijijini.
Huu ni uthibitisho anuai kabisa wa ama uchawa au usisiemu, huhitaji ubongo ukiwa mwanachama wa sisiemu au chawa, UTI wa ubongo unatosha!

Swali, watu wa hali ya chini ni asilimia ngapi ya watu wote ndani ya Tanzania au Tanganyika?
 
Rais Samia ametimiza miaka 3 tangu achukue madaraka ya urais lakini ukilinganisha na miaka 3 ya hayati Magufuli akiwa madarakani ni kama mlima na kichuguu kwa matokeo.
Rais Samia amefanya semina nyingi kwa mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi na wakuu wa mikoa lakini bado utendaji wa serikali yake uko duni sana! Matokeo baada ya semina hizo hayaonekani kabisa.
Rushwa, uzembe, mfumuko wa bei, kupandisha gharama za miradi, kuchelewesha miradi imekuwa ndiyo sifa kuu ya serikali ya Rais Samia.
Hayati Magufuli alijenga majengo ya wizara na kuhamishia serikali yote Dodoma ndani ya miaka 3 lakini Rais Samia kwa miaka 3 hakuna jengo hata moja lililokamilika kiasi cha kuanza kukaliwa na watu. Kwenye serikali ya Samia hamna mradi hata mmoja ulioanzishwa unaoweza kusema kwamba angalau hapa Kuna watu walikaa na kutumia akili.
Rais Samia amefanya vizuri sana kwenye ujenzi wa madarasa kwa kutumia mkopo wa fedha za Uviko.
Mkuu hivi Samia angekuwa haendelezi miradi ya Magufuli, as ingekuwa kafanya miradi mingi?

Mkuu umesema kuwa hajaweza kujenga jengo lolote likakamilika na kukaliwa na watu, je majengo ya madrasa na vituo vya afya nchi nzima sio majengo? Je binadamu wanao yatumia sasa hivi sio watu?

Mkuu ukisema ukweli haupungukiwi na chochote bali unaheshika zaidi!
 
Back
Top Bottom