Mhe Kikwete URAIS Chukua, Mchakato Mzima wa KATIBA MPYA ni ya Wananchi Wote

Chief Rumanyika

Senior Member
Dec 29, 2010
138
0
WATANZANIA MCHAKATO MZIMA WA KATIBA MPYA NI HAKI YETU NA WALA SI MILIKI YA RAIS

Heri ya Mwaka Mpya 2011 kila mmoja wetu!!

Ndugu zangu Wana-JF na Watanzania kwa ujumla wetu, tusisahau mambo ya msingi yaliotufikisha hapa hasa sisi VIJANA kutaka kujiandikia wenyewe KATIBA MPYA.

Sote tunaelewa ya kwamba KATIBA ni MKATABA rasmi kati ya WATAWALA (Serikali) na WATAWALIWA (Sisi Wananchi) kusimamia maendeleo yetu, usimamizi mzuri wa rasilmali zetu, na kuzingatia haki katika taifa letu.

Kimsingi mara baada ya wengi wetu kugundua ya kwamba WATALA WETU hawako tena darakani kwa MASLAHI YETU KAMA UMMA WA TANZANIA bali lao ni kushiriki uchafu mwingi ukiwemo UFISADI WA KUPINDUKIA hapo ndipo wazo la zaidi ya miaka 20 sasa likatujia upya KUANZISHA MARAMOJA MCHAKATO WA KUANDIKA KATIBA MPYA.

Lengo letu hapa ni kwamba tunataka kuwadhibiti WATAWALA na tamaa zao wasiathiri tena maendeleo ya taifa letu. Kitendo cha Rais Kikwete naye kupendezewa na wazo hili la wananchi KUJISHIRIKISHA KATIKA KILA HATUA YA MCHAKATO MPANA KUPATIKANA KATIBA MPYA ni jambo la kupongezwa kwake kama raia mojawapo nchini mwetu ambaye naye ana haki kulizungumzia katiba kama mzaliwa wa taifa hili.

Hoja Yangu:


Sote tunatambua ukweli kwamba TUNAPOZUNGUMZI UTEKELEZAJI WA KATIBA ILIOTAYARI hapo wanahitajika watendaji ambao ni WATAWALA kwa misingi ya vyeo vyao kufanya hiyo kazi.

Ila kwa upande wa pili, TUNAPOZUNGUMZIA UUNDWAJI UPYA WA KATIBA YA NCHI hapo WATAWALA huitajika kuchagua kujumuika pamoja na wananchi watawaliwa (kwa msingi wa haki yao ya uraia wao na wala si VYEO VYAO) kuja KUANZISHA MCHAKATO PAMOJA NA KUIENDELEZA KILA HATUA PAMOJA huku washiriki wote wakiwa na cheo cha URAIA TU kwenye kuunda KATIBA MPYA.

Kwa msingi huu, Mhe Kikwete, hawezi akajitwisha jukumu la RAIA WOTE WA TANZANIA kujiendeshea hatua zozote za mchakato mzima wa kupatikana kwa KATIBA MPYA. Endapo atakua na maoni yenye kusaidia basi awe huru kuja nayo kwenye MKUTANO MKUU WA TAIFAKUANDIKA KATIBA utakaoundwa na bunge.
 
Urais ni wa yule anayesadikiwa kuchaguliwa na wananchi jinsi ulivyo wewe.

Lakini kuhusu kuandikwa upya katiba, njoo tufanye hii kazi kwa pamoja kwa kofia yako ile ya kuwa raia wa Tanzania na wala usijiingize kwenye mchakato kwa cheo chako.
 
Naunga mkono hoja yako asilimia 101. Mojawapo ya athari za katiba ya sasa, ni madaraka makubwa aliyonayo rais yanayompa madaraka ya kuteua yeye peke yake, viongozi na watendaji wote waandamizi walio kwenye utumishi wa umma.

Kwa maoni ya wengi, rais wetu hajaonyesha umahili wa kutosha katika kutekeleza jukumu hilo. Kutokana na hayo, wadadisi wa mambo wameelezea azma ya rais ya kuunda yeye mwenyewe tume ya kuratibu mchakato mzima wa uandikaji wa katiba mpya. Kuwa ni hila zenye lengo kuzima moto ulio washwa na chadema juu ya jambo hilo.

Kwa maoni yangu ni kwamba, maadamu mfumo wa mchakato uliobuniwa na Kenya umeiwezesha nchi hiyo jirani kuwa na katiba ambayo raia wote wanajivunia, kwanini basi nasisi tusifuate mchakato huo katika kuandika upya katiba yetu.
 
Kukubali kwake kupatikana katiba mpya tukubaliane naye, lakini kufanya hiyo kazi yeye peke yake hata mimi sikubaliani.

Kama hakuifikiria swala la katiba tangu mwanzo mpaka tulivyoanza vilio nchi nzima sa tumuamini vipi kutufanyia peke yake hiyo kazi kwa mapenzi gani?
 
Naunga mkono hoja yako asilimia 101. Mojawapo ya athari za katiba ya sasa, ni madaraka makubwa aliyonayo rais yanayompa madaraka ya kuteua yeye peke yake, viongozi na watendaji wote waandamizi walio kwenye utumishi wa umma.

Kwa maoni ya wengi, rais wetu hajaonyesha umahili wa kutosha katika kutekeleza jukumu hilo. Kutokana na hayo, wadadisi wa mambo wameelezea azma ya rais ya kuunda yeye mwenyewe tume ya kuratibu mchakato mzima wa uandikaji wa katiba mpya. Kuwa ni hila zenye lengo kuzima moto ulio washwa na chadema juu ya jambo hilo.

Kwa maoni yangu ni kwamba, maadamu mfumo wa mchakato uliobuniwa na Kenya umeiwezesha nchi hiyo jirani kuwa na katiba ambayo raia wote wanajivunia, kwanini basi nasisi tusifuate mchakato huo katika kuandika upya katiba yetu.

Na mimi najiuliza kwa nini basi na sisi tusifuate taratibu zile zile mchakato kama walivyofanya Kenya katika kuandika upya katiba yetu?
 
Byendangwero ukitaka kujua kwamba Kikwete atekeleze hata kakijipande cha mchakato juu ya azma ya wananchi kujiandikia katiba hebu kwanza jiulize:

1. Ataitelezaje bila bias wakati yeye ndie MWENYEKITI CCM taifa; Chama ambacho hakipendi mabadiliko ya katiba?

2. Kwa mtaji wa kulalamikiwa KUCHAKACHUA UCHAGUZI; Moral Authority ya kuweza kuaminiwa na jukumu kubwa kama hili aipate wapi?

3. Kwa kauli yake mwenyewe kwamba "katiba haitobadilishwa ng'o" na sasa kutaka kutuaminisha ujemadari wake huku si kutaka kumteka kichanga chetu katiba kisha akaichinjie mbali?? Wanasheria fulani wamesekena kufanya hivyo kwa TANESCO na kuipa DOWANS ulaji tunaoupinga.

4. Kwa kawaida serikali ya CCM huwa haitekelezi jambo lisilokwepo ndani ya ilani yake ya uchaguzi, mwenzetu CCM kimekaa lini ndio wakakupa hizo baraka?
 
Kukubali kwake kupatikana katiba mpya tukubaliane naye, lakini kufanya hiyo kazi yeye peke yake hata mimi sikubaliani. Kama hakuifikiria swala la katiba tangu mwanzo mpaka tulivyo anza vilio nchi nzima sa tumuani vipi kutufanyia peke yake hiyo kazi kwa mapenzi gani?

Mashaka yako juu ya jambo hili nayaafiki kabisa.
 
Byendangwero ukitaka kujua kwamba Kikwete atekeleze hata kakijipande cha mchakato juu ya azma ya wananchi kujiandikia katiba hebu kwanza jiulize:

1. Ataitelezaje bila bias wakati yeye ndie MWENYEKITI CCM taifa; Chama ambacho hakipendi mabadiliko ya katiba?

2. Kwa mtaji wa kulalamikiwa KUCHAKACHUA UCHAGUZI; Moral Authority ya kuweza kuaminiwa na jukumu kubwa kama hili aipate wapi?

3. Kwa kauli yake mwenyewe kwamba "katiba haitobadilishwa ng'o" na sasa kutaka kutuaminisha ujemadari wake huku si kutaka kumteka kichanga chetu katiba kisha akaichinjie mbali?? Wanasheria fulani wamesekena kufanya hivyo kwa TANESCO na kuipa DOWANS ulaji tunaoupinga.

4. Kwa kawaida serikali ya CCM huwa haitekelezi jambo lisilokwepo ndani ya ilani yake ya uchaguzi, mwenzetu CCM kimekaa lini ndio wakakupa hizo baraka?

Na kweli Wadanganyika hatukawii kushangilia hata pale mtu anapotuandalia chakula pamoja na sumu ya panya, du!
 
Naomba ufafanuzi kidogo kama kweli swala la katiba mpya haipo kweli kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM ndiyo niweze kumwaga maoni zaidi.
 
Urais ni wa yule anayesadikiwa kuchaguliwa na wananchi jinsi ulivyo wewe.

Lakini kuhusu kuandikwa upya katiba, njoo tufanye hii kazi kwa pamoja kwa kofia yako ile ya kuwa raia wa Tanzania na wala usijiingize kwenye mchakato kwa cheo chako.

Nadhani hoja kama hii tulishaijadili hapa JF kama sikosei. Katiba kweli ni lazima iwe SHIRIKISHI kwa hatua zote za mchakato mzima.Chukua tano kwa hilo Chifu.
 
Naunga mkono hoja yako asilimia 101. Mojawapo ya athari za katiba ya sasa, ni madaraka makubwa aliyonayo rais yanayompa madaraka ya kuteua yeye peke yake, viongozi na watendaji wote waandamizi walio kwenye utumishi wa umma.

Kwa maoni ya wengi, rais wetu hajaonyesha umahili wa kutosha katika kutekeleza jukumu hilo. Kutokana na hayo, wadadisi wa mambo wameelezea azma ya rais ya kuunda yeye mwenyewe tume ya kuratibu mchakato mzima wa uandikaji wa katiba mpya. Kuwa ni hila zenye lengo kuzima moto ulio washwa na chadema juu ya jambo hilo.

Kwa maoni yangu ni kwamba, maadamu mfumo wa mchakato uliobuniwa na Kenya umeiwezesha nchi hiyo jirani kuwa na katiba ambayo raia wote wanajivunia, kwanini basi nasisi tusifuate mchakato huo katika kuandika upya katiba yetu.

Pengine kweli ni 'mzalendo' tangu January 2011 lakini kazinduku kwa mkurupuko mno.

Akawasikilize wenye hoja ya kuandikwa upya katiba laa sivyo janja za KUPOTEZA MUDA, KUHODHI MCHAKATO na pengine kuuteka nyara uamuzi wa wananchi kujiandikia katiba huenda ikampasukia vibaya mno usoni.

Hofu yangu kubwa ni tunda litakalozaliwa na ULAGHAI kwenye kuandika katiba huenda ikama mchungu kupita kiasi.
 
Watanzania, tukidanganyika katika ahadi za ajabu ajabu kukumbatia wachafu na tukijua fika kuwa ni wachafu kwa mienendo yao na wakaambukiza uchafu wao kutuchafulia nia yetu njema ya kujiandikia katiba mpya na baada tukaishia ama na mchezo mchafu au katiba mpya chafu, basi moja kwa moja kila mmoja wetu ajiandae kuhukumiwa vibaya mno na historia ya taifa hili.

Zingatieni hilo.
 
Back
Top Bottom