ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Wakati baadhi ya dini zinafundisha kuwa dhambi zote ni sawa, nimesikia kwa waumini wa dini fulani kuwa "dhambi mbaya kabisa kwenye vitabu vya Mungu" ni dhambi ya "kumegana" , "kura uroda" au "Kuzini".
Watetezi wa hili wanadai kuwa dhambi hii inaambatana au kumalizikia na kuvunja amri zote kumi za agano kati ya Mungu na wanadamu kupitia Musa.
Kwa dhambi ya kuzini, mtu anakuwa amesema uwongo kwa mwenzi wake na huyo atakaezini nae au watu wengine ili kuficha uovu nk. Kwa kupenda zinaa, mtu anakuwa hajamheshimu Mungu wake, wala hajaheshimu wazazi au wanaomzidi umri, anaweza kutoheshimu pia siku ya ibada kwa kuwaza zinaa kichwani hata akiwa kanisani au msikitini, anakuwa ametamani mali ya mtu mwingine (mke,gari, nguo, nyumba nk). Kwa zinaa mtu anaweza kuua (kupitia magonjwa au kuua mwenzake ili ampate huyo wa kuzini nae). Anakuwa ametamani mke asiye wake (wa jirani, rafiki nk) ili atende nae zinaa. Utamu wote wa zinaa kwa wanadamu ni uchafu na chukizo mbele za Mungu na Malaika wake.
Kwamba, zinaa inahusisha mawazo, maneno na matendo na kushindwa kutimiza wajibu. Ikiwa Mzazi au mtu mwenye majukumu, anaweza kutelekeze familia kwa sababu ya kujikita kwenye fani ya kubwinya "tunda la katikati" nk. Aidha, tafsiri ya zinaa inakuwa imekamilika baada ya mwili na roho kukubaliana (kufanya agano la mapatano ya kutenda dhambi) kwa kukubali kukutanisah ndimi mbili ambazo pengine hazifkuwahi kufahamiani hata kidogo katika maisha na hata malaika walinzi wa ndimi hizo wanaweza kuwa na sifa zisizo sawa machoni pa Mungu.
Kwa tendo hilo, zinaa inahesabika kuwa ni dhambi ya machukizo kwa Mungu wako na Malaika mlinzi na ndio maana baada ya tendo hilo, ubinadamu huwa unatoweka kwa sekunde kadhaa na hapo huwezi kutambua uzuri au ubaya wa tendo ulilolifanya na pengine ujutie moyoni mwako kwa nini umefanya vile na unapojitambua upo vile ulivyo aibu inakushika (upo uchi!).
Wakati mwingine, inaweza kukupelekea kwenye ugomvi na huyo uliezini nae kwani maelewano yanakuwa yameisha (kw mf: ukipewa "invoice" ya kulipia huduma uliyopewa na kutoona hailingani na thamani halisi ya kupurudika kwako).
Enyi wanazuoni, nini ukweli wa habari hii?.
Watetezi wa hili wanadai kuwa dhambi hii inaambatana au kumalizikia na kuvunja amri zote kumi za agano kati ya Mungu na wanadamu kupitia Musa.
Kwa dhambi ya kuzini, mtu anakuwa amesema uwongo kwa mwenzi wake na huyo atakaezini nae au watu wengine ili kuficha uovu nk. Kwa kupenda zinaa, mtu anakuwa hajamheshimu Mungu wake, wala hajaheshimu wazazi au wanaomzidi umri, anaweza kutoheshimu pia siku ya ibada kwa kuwaza zinaa kichwani hata akiwa kanisani au msikitini, anakuwa ametamani mali ya mtu mwingine (mke,gari, nguo, nyumba nk). Kwa zinaa mtu anaweza kuua (kupitia magonjwa au kuua mwenzake ili ampate huyo wa kuzini nae). Anakuwa ametamani mke asiye wake (wa jirani, rafiki nk) ili atende nae zinaa. Utamu wote wa zinaa kwa wanadamu ni uchafu na chukizo mbele za Mungu na Malaika wake.
Kwamba, zinaa inahusisha mawazo, maneno na matendo na kushindwa kutimiza wajibu. Ikiwa Mzazi au mtu mwenye majukumu, anaweza kutelekeze familia kwa sababu ya kujikita kwenye fani ya kubwinya "tunda la katikati" nk. Aidha, tafsiri ya zinaa inakuwa imekamilika baada ya mwili na roho kukubaliana (kufanya agano la mapatano ya kutenda dhambi) kwa kukubali kukutanisah ndimi mbili ambazo pengine hazifkuwahi kufahamiani hata kidogo katika maisha na hata malaika walinzi wa ndimi hizo wanaweza kuwa na sifa zisizo sawa machoni pa Mungu.
Kwa tendo hilo, zinaa inahesabika kuwa ni dhambi ya machukizo kwa Mungu wako na Malaika mlinzi na ndio maana baada ya tendo hilo, ubinadamu huwa unatoweka kwa sekunde kadhaa na hapo huwezi kutambua uzuri au ubaya wa tendo ulilolifanya na pengine ujutie moyoni mwako kwa nini umefanya vile na unapojitambua upo vile ulivyo aibu inakushika (upo uchi!).
Wakati mwingine, inaweza kukupelekea kwenye ugomvi na huyo uliezini nae kwani maelewano yanakuwa yameisha (kw mf: ukipewa "invoice" ya kulipia huduma uliyopewa na kutoona hailingani na thamani halisi ya kupurudika kwako).
Enyi wanazuoni, nini ukweli wa habari hii?.