Mgonja, Ndulu differ on Tangold ownership

jamani msipate pressure bure mkafa. hapa mnazunguka mbuyu tu. Muhusika kamili kakaa kimya hataki hata kuongea, na huyo si mwingine bali ni Mjasiriamali mpendwa sana Mr. Clean. Bila huyo tutajadili hapa mpaka mishipa ya shingo itauma bila ufumbuzi wowote
 
Ngabu,

Hawa watu wenye "akili sana" ndio wanatuponza... hebu fuatilia profile ya Chenge, Balali, na huyu Mgonja ....

Grrrrrrrrr

Mwafika wa kike,

wanaotupoza sio wenye "akili sana" bali yule tuliyempa uwezo wa kuwaadhibu lakini anashindwa kwa kuwaonea "aibu"!!

sijui anataka uwezo gani tena mwingine!
 
Mtasemaaaa Weee!!!!!!!!!! Mwisho Mtalala. Au Mnabisha?

Si Unaona Ya Balali?
Ya Iptl?
 
Nasikia kizunguzungu nikisijia Mgonja ni almost director wa kila kampuni la ummma!!! sh**t Watanzania wote muna makengeza... badilisheni sheria please!
 
Bubu,
Labda haya madudu yamefanyika ktk awamu ya tatu of uor gorvenment, so ni vigumu sana kumlaumu Gray Mgonja, kwani pale BoT mambo ni mengi
 
Bubu,
Labda haya madudu yamefanyika ktk awamu ya tatu of uor gorvenment, so ni vigumu sana kumlaumu Gray Mgonja, kwani pale BoT mambo ni mengi

Hata kama madudu yamefanyika katika awamu ya tatu. Hawa jamaa kama viongozi wa juu ndani ya serikali na pia wasomi inabidi waongee kwa uhakika wakiwa na supporting documents wa kile wanachoongea, vinginevyo wote wanaonekana ni wababaishaji tu.

Documents za awamu ya tatu zipo, kama zimeshaharibiwa ili kuficha ushahidi basi watwambie hivyo kwamba hawana uhakika na wanachoongea.
 
Nafikiri Wakurugenzi wa TANGOLD Walisha jitaja kuwa ni CHenge, Rutabanzibwa, Mgonja na wengine tuwaombe tu kwa busara warudishe pesa hizi.

Kashfa ya mgodi wa dhahabu Buhemba, bilioni 30/- `zaliwa`

Kashfa ya ufisadi katika mgodi wa dhahabu wa Buhemba ulioko mkoani Mara, umesababisha mapato ya nchi yenye thamani ya Sh. bilioni 30 `kuliwa` na wajanja.

Fedha hizo `zilitafunwa ` katika Awamu ya Rais Benjamin Mkapa, kuanzia 2003 hadi 2006 kupitia wawekezaji wa kampuni ya Tangold `iliyojimilikisha` mgodi huo kinyemela.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopatikana kutoka Benki Kuu (BoT), jijini Dar es Salaam, Tangold ilichukua mgodi wa Buhemba ambao kuanzia mwaka 1997 ulikuwa ukiendeshwa kwa ubia na kampuni ya MEREMETA, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Triennex Properietary Limited ya Afrika Kusini.

Nyaraka nyeti kutoka BoT zilisema kuwa JWTZ na mbia huyo walianza kuchimba dhahabu Oktoba 1997 na baadaye mkataba ulimalizika na Tangold ilijimilikisha mgodi huo kuanzia mwaka 2003 hadi 2006.

Ziliibua kuwa mambo ya MEREMETA hayakwenda vizuri kwani miradi yote iliyoanzishwa ilitumia fedha za mikopo kutoka Benki ya Nedcor ya Afrika Kusini ambayo ilichukuliwa na kampuni ya Triennex Properietary kwa niaba ya Serikali ya Tanzania.

``Kwa kuhofia athari za mkopo huo kwa uchumi wa nchi, Rais mstaafu Benjamin Mkapa, aliunda Kamati maalum (task force) mwaka 2003 kwa ajili ya kuhakikisha mkopo unalipwa , kusimamia uendeshaji wa miradi ya MEREMETA na kuchunguza matatizo ya kampuni hiyo ya JWTZ na wawekezaji kutoka Afrika Kusini``, kilisema chanzo cha BoT.

Wajumbe wa kamati ya kuchunguza matatizo ya MEREMETA walikuwa ni Gavana wa BoT aliyefutwa kazi Dk. Daudi Balali, aliyekuwa Mwenyekiti.

Wengine ni Makatibu Wakuu Bw. Gray Mgonja wa Wizara ya Fedha, Bw. Patrick Rutabanzibwa -Madini na Nishati, (sasa Wizara ya Maji na Umwagiliaji), Bw. Vincent Mrisho aliyekuwa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (sasa Ofisi ya Waziri Mkuu) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya awamu ya tatu, Bw. Andrew Chenge.

Bw. Chenge mwezi uliopita alijiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu kufuatia tuhuma za kuhifadhi zaidi ya shilingi bilini moja zinazodaiwa kuwa ni rushwa aliyopewa katika ununuzi wa rada iliyogharimu bilioni 70/-

Baada ya Tangold kuchukua Buhemba, ilichimba dhahabu yenye thamani ya Dola milioni 121.3 sawa na Sh. bilioni 147.

Dhahabu iliyochimbwa kwa kipindi hicho ni mali ya serikali kwani mgodi huo ulikuwa ni mali ya umma na ilikuwa na thamani ya Dola.

Taarifa zilizoifikia Nipashe Jumapili zilieleza kuwa katika kipindi hicho cha miaka minne, Tangold ilichimba karibu kilo 10,000 za dhahabu kutoka mgodi huo na kupata faida ya bilioni 30/-.

Tangold ilionyesha kuwa ililipa mrahaba wa Dola milioni 3.6 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Vijijini ambao ni sawa na Sh. bilioni 4.36 kwa muda wote.

Takwimu za uchimbaji zilionyesha kuwa mwaka 2003 zilichimba kilo 2,848. 874, wakati mwaka uliofuata zilipatikana kilo 291.290. Mapato yanaonyesha kuwa mwaka 2005 ilipata kilo 2,220. 560 na mwaka 2006 ilipata kilo 1,890.934 na kwa jumla zilipatikana kilo 9, 941.658.

Hata hivyo, baada ya kupata kiasi hicho BoT ilionyesha kuwa Tangold iliilipa kampuni moja ya Afrika ya Kusini gharama za kuendesha mgodi ambazo ni kati ya Dola milioni 80 na 90 kwa miaka minne ambazo ni sawa na Sh. bilioni 100 mpaka 116.3.

Hata hivyo, licha ya kupata mabilioni hayo Tangold haikuwasilisha fedha hizo serikalini.

``Taarifa za Tangold haziko Wizara ya Fedha-Msajili wa Hazina , wala kwa Msajili wa Biashara (BRELA) hata BoT hazikuwahi kuwasilishwa,`` kilisema chanzo cha BoT.

Pesa hizo bilioni 30 ni mali ya umma lakini hazijulikani zilipo na swali linaloendelea kuulizwa ni wamiliki wa kampuni hiyo ni akina nani?

Katika Mkutano wa Bunge wa mwezi uliopita Mbunge wa Musoma Vijini Bw. Nimrod Mukono, alitaka kufahamishwa wamiliki wa mgodi wa Buhemba.
Source http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2008/05/11/114166.html.
 
Back
Top Bottom