wasaimon
R I P
- Oct 6, 2010
- 220
- 45
Kuna mgomo wa madereva ulioanza toka saa nne asubuhi leo mpaka muda huu hakuna gari yeyote ya utalii inaweza kupita eneo la Oldupai, mpaka sasa magari zaidi ya 100 yameshindwa kuendelea na safari.
Chanzo cha mgomo huo ni gari moja ya utalii limeanguka leo asubuhi likiwa na wageni, watu wa Hifadhi ya Ngorongoro walipewa taarifa lakini hawajajitokeza ktk kutoa msaada, madereva wa utalii wamekasirishwa na hicho kitendo.
Sababu kubwa ya ajali hiyo kutokea ni ubovu wa barabara na hii barabara inamilikiwa na wao (Ngorongoro Conservations Area) na tambua kila gari na abiria wake wanalipia transist ambayo kwa kila mgeni ni $ 50 na Mtz ni Tsh 1500/= gari ndogo lenye 2000kg Tsh 10,000/=, gari zaidi ya 2000kg - 7,000kg Tsh 20,000/= wanahoji kama kila gari na kila mwanadamu anepita tu analipa pesa iweje washindwe kutengeneza barabara.
Na ukipata ajali ndani ya eneo lao faini ni Tsh 50,000/= kwa gari lenye kg 2000 na zaidi ya 2000kg - 7000kg faini yake ni Tsh 100,000/=
Chanzo cha mgomo huo ni gari moja ya utalii limeanguka leo asubuhi likiwa na wageni, watu wa Hifadhi ya Ngorongoro walipewa taarifa lakini hawajajitokeza ktk kutoa msaada, madereva wa utalii wamekasirishwa na hicho kitendo.
Sababu kubwa ya ajali hiyo kutokea ni ubovu wa barabara na hii barabara inamilikiwa na wao (Ngorongoro Conservations Area) na tambua kila gari na abiria wake wanalipia transist ambayo kwa kila mgeni ni $ 50 na Mtz ni Tsh 1500/= gari ndogo lenye 2000kg Tsh 10,000/=, gari zaidi ya 2000kg - 7,000kg Tsh 20,000/= wanahoji kama kila gari na kila mwanadamu anepita tu analipa pesa iweje washindwe kutengeneza barabara.
Na ukipata ajali ndani ya eneo lao faini ni Tsh 50,000/= kwa gari lenye kg 2000 na zaidi ya 2000kg - 7000kg faini yake ni Tsh 100,000/=