kebepa
Senior Member
- Dec 20, 2009
- 133
- 14
Mambo ambayo yamepelekea madaktari kugoma yamejikita katika mfumo mzima wa utoaji huduma za afya katika nchi yetu.
Mfumo wa afya unatakiwa kuwa na nguzo sita ( kwa kadri ya Shirika la Afya duniani) ambazo ni
i)utoaji wa huduma za matibabu
ii)Rasilimali watu
iii)Mfumo wa taarifa za afya
iv)Madawa, vifaa tiba na teknolojia za tiba
v)Rasilimali fedha
vi) uongozi, será na uratibu
Nguzo hizi kwa kufanya kazi kwa ushirikiano ndipo mfumo wa utoaji huduma za afya huimarika. Madai ya madaktari yamegusa kila kipengele na yanaashiria kuwa mfumo mzima wa afya katika nchi yetu unatakiwa kufumuliwa na kusukwa upya.Hadi sasa serikali (executive) imeshindwa kusimamia ufanisi wa uratibu wa nguzo zote sita.Kwa kupeleka suala hili mahakamani inaonyesha wazi kabisa kuwa limewashinda na wanahitaji msaada wa muhimili mwingine(mahakama) , lakini hili siyo suluhisho la kutatua matatizo ya kimfumo, ila linachochea tatizo kuwa kubwa zaidi. Kama muhimili wa tatu ( bunge) halitaingilia, baadala ya serikali kutoa huduma za afya kwa wananchi, watakuwa wapo busy kufuatilia mgogoro huu mahakamani wakati wananchi wakiendelea kufa.
Katika mazingira haya, bunge lilitakiwa lije na mswada wa dharura ( au suluhisho lolote) ambao utaweza kutatua matatizo yaliyopo kwenye mfumo wa utoaji huduma za afya katika nchi. Inashangaza kuona hadi sasa bunge lipo kimya wakati wananchi wanaendelea kufa na wengine kukosa huduma za matibabu au kama wakipata wanapata kwa bei kubwa kana kwamba hawana wawakilishi wanaoweza kuwasemea na kuhakikisha kuwa huduma za afya zinapatikana.Wabunge hawa wanasahau wajibu wao kuwa wao ndio waliopewa dhamana ya kutunga sheria na kurekebisha zile zinazokuwa na utata na kuleta migogoro isiyo ya lazima katika nchi yetu.Wapo wapi sasa, ina maana kuwa katika bunge letu hakuna watu makini wanaoweza kufikiria na kutatua mgogoro huu? Nachelea kufikiria hivyo, nadhani wamesahau kuwa wanatakiwa kusimamia maslahi ya wananchi kwanza kuliko vyama vilivyowasimamisha ( eti wale wa chama tawala hawataki kuonesha kuwa serikali imechemsha, na wale wa upinzani hawaeleweki…hapa ndipo ilitakiwa hata kugomea mjadala unaendelea sasa bungeni na kutoka nje kama walivyowahi kutuaminisha siku za nyuma kwamba wapo kwa ajili ya wananchi).
Hii inaonyesha wazi jinsi ambavyo bunge letu limekuwa linausikiliza muhimili mwingine ( executive) baadala ya kuusimamia kwa manufaa ya wananchi ambao ndio wanaowapeleka hawa wabunge mjengoni. Kama ni watu makini, wanatakiwa wasisubiri kuletewa miswaada na serikali na wao kuchangia tu badala ya wao kuhusika moja kwa moja kwenye utengenezaji wa miswaada.
Umefikia wakati wa kila Mwananchi kumuuliza mbunge wake kuwa kama hasimamii upatikanaji wa huduma za afya na huduma nyingine za kijamii, anafanya nini bungeni?na kumwambia wazi kuwa sisi wananchi hatutaki kusikia eti suala la mgomo wa madaktari upo mahakamani wakati tunaendelea kufa.
Asasi za kiraia na viongozi mbalimbali wa kijamii wanatakiwa wasikae kimya kwa suala hili.
Mfumo wa afya unatakiwa kuwa na nguzo sita ( kwa kadri ya Shirika la Afya duniani) ambazo ni
i)utoaji wa huduma za matibabu
ii)Rasilimali watu
iii)Mfumo wa taarifa za afya
iv)Madawa, vifaa tiba na teknolojia za tiba
v)Rasilimali fedha
vi) uongozi, será na uratibu
Nguzo hizi kwa kufanya kazi kwa ushirikiano ndipo mfumo wa utoaji huduma za afya huimarika. Madai ya madaktari yamegusa kila kipengele na yanaashiria kuwa mfumo mzima wa afya katika nchi yetu unatakiwa kufumuliwa na kusukwa upya.Hadi sasa serikali (executive) imeshindwa kusimamia ufanisi wa uratibu wa nguzo zote sita.Kwa kupeleka suala hili mahakamani inaonyesha wazi kabisa kuwa limewashinda na wanahitaji msaada wa muhimili mwingine(mahakama) , lakini hili siyo suluhisho la kutatua matatizo ya kimfumo, ila linachochea tatizo kuwa kubwa zaidi. Kama muhimili wa tatu ( bunge) halitaingilia, baadala ya serikali kutoa huduma za afya kwa wananchi, watakuwa wapo busy kufuatilia mgogoro huu mahakamani wakati wananchi wakiendelea kufa.
Katika mazingira haya, bunge lilitakiwa lije na mswada wa dharura ( au suluhisho lolote) ambao utaweza kutatua matatizo yaliyopo kwenye mfumo wa utoaji huduma za afya katika nchi. Inashangaza kuona hadi sasa bunge lipo kimya wakati wananchi wanaendelea kufa na wengine kukosa huduma za matibabu au kama wakipata wanapata kwa bei kubwa kana kwamba hawana wawakilishi wanaoweza kuwasemea na kuhakikisha kuwa huduma za afya zinapatikana.Wabunge hawa wanasahau wajibu wao kuwa wao ndio waliopewa dhamana ya kutunga sheria na kurekebisha zile zinazokuwa na utata na kuleta migogoro isiyo ya lazima katika nchi yetu.Wapo wapi sasa, ina maana kuwa katika bunge letu hakuna watu makini wanaoweza kufikiria na kutatua mgogoro huu? Nachelea kufikiria hivyo, nadhani wamesahau kuwa wanatakiwa kusimamia maslahi ya wananchi kwanza kuliko vyama vilivyowasimamisha ( eti wale wa chama tawala hawataki kuonesha kuwa serikali imechemsha, na wale wa upinzani hawaeleweki…hapa ndipo ilitakiwa hata kugomea mjadala unaendelea sasa bungeni na kutoka nje kama walivyowahi kutuaminisha siku za nyuma kwamba wapo kwa ajili ya wananchi).
Hii inaonyesha wazi jinsi ambavyo bunge letu limekuwa linausikiliza muhimili mwingine ( executive) baadala ya kuusimamia kwa manufaa ya wananchi ambao ndio wanaowapeleka hawa wabunge mjengoni. Kama ni watu makini, wanatakiwa wasisubiri kuletewa miswaada na serikali na wao kuchangia tu badala ya wao kuhusika moja kwa moja kwenye utengenezaji wa miswaada.
Umefikia wakati wa kila Mwananchi kumuuliza mbunge wake kuwa kama hasimamii upatikanaji wa huduma za afya na huduma nyingine za kijamii, anafanya nini bungeni?na kumwambia wazi kuwa sisi wananchi hatutaki kusikia eti suala la mgomo wa madaktari upo mahakamani wakati tunaendelea kufa.
Asasi za kiraia na viongozi mbalimbali wa kijamii wanatakiwa wasikae kimya kwa suala hili.