Mgodi wa Shanta Singida usiwabague wazawa

Suphian Juma

Senior Member
Apr 2, 2019
133
546
MGODI WA SHANTA SINGIDA USIWABAGUE WAZAWA.

BARUA YA WAZI KWA WAZIRI WA MADINI DOTO BITEKO

Na: Suphian Juma Nkuwi

Mheshimiwa Waziri,

Nakusalim kwa Jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pole na hongera kwa majukumu ya kujenga Taifa letu.

Awali ya yote nitangulize Kongole nyingi kwa Rais Dkt Samia kwa kurejesha na kuimarisha Sera rafiki kwa Wawekezaji na Wafanyabiashara ndani ya miaka miwili ya Uongozi wake kiasi cha kwamba sasa kila mara sote tunashuhudia makampuni mengi ya Uwekezaji ya ndani na nje ya nchi yanawekeza kwa kasi kubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo madini ukilinganisha na muongo mmoja nyuma.

Pamoja na matunda haya ya kiuongozi na Uwekezaji, jambo la pili kuu ambalo sote Watanzania tuna kiu ya kulionja ni kuona pasina shaka Uwekezaji huo wa madini unatuletea Chakula mezani kama wananchi wenye Nchi na kukuza pato la Taifa kwa ujumla wake.

Na hapa si Serikali tu pekee bali nasi wananchi mmoja mmoja tuna uhuru, Haki na wajibu wa kufuatilia, kutathimini na kusimamia Uwekezaji ndani ya raslimali zetu zinazotuzunguka kuona zinatufukuzia umaskini na sio kutuvutia umaskini.

Mheshimiwa Waziri,

Na hapa ndio pamenifanya nishike kalamu yangu niseme jambo.

Mkoa wa Singida tuna bahati ya kuwa na Madini ya dhahabu. Rejea kuu kwa sasa ni Mgodi mpya wa uchimbaji dhahabu wa Kati wa Singida Gold Mine unaomilikiwa na Kampuni ya Shanta Gold Mining Company Limited uliopo wilaya ya Ikungi ambao kwa mujibu wa Kaimu Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Singida Mjiolojia Chone Malembo mgodi huu umezalisha zaidi ya kilo 49 za dhahabu tangu kuanza uzalishaji mwezi Machi, 2023.

Aidha pia kwa mujibu taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa mgodi huu wa Shanta Mining Limited Honest Mrema aliyoitoa mwanzoni mwa mwaka huu ni kwamba mgodi ungeaajiri zaidi ya wafanyakazi wa moja kwa moja 220 na wafanyakazi 150 wa muda mfupi.

Mheshimiwa Waziri,

Kwa nyakati tofauti katika ya Machi na Mei mwaka huu kama mdau wa agenda za vijana, madini, Mazingira na kipekee mzawa wa Wilaya ya Ikungi nimepokea malalamiko lukuki ya vijana na wakazi wa vijiji vya Ikungi kwamba mgodi wa huu wa Shanta hauwatendei haki ya kuajiriwa licha ya kwamba wana uzoefu katika kada hitajika katika kuleta ufanisi wa mgodi huo badala yake idadi kubwa ya waajiriwa "wasomi" ni wafanyakazi kutoka nje ya Wilaya ya Ikungi na Mkoa wa Singida.

Hii ni kinyume Sera ya Madini ya Mwaka 2009 na Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 pamoja na Marekebisho yake ya Mwaka 2017 ambazo zinatoa mwongozo wa namna Kampuni za madini zinavyopaswa kufungamanisha Sekta ya Madini na sekta nyingine za kiuchumi ikiwemo pia uajiri unapaswa uwe 7/3 yaani uwiano (ratio) uwe wazawa 7 kwa wageni wa 3.

Mheshimiwa Waziri,

Idadi kubwa ya vijana wazawa wanaolalamika ni wale wenye ujuzi wa kitaaluma hususani katika nyanja za ikolojia, afya, Mazingira na ICT (TEHAMA) ambapo madai yao makuu ni kwamba wamejaribu kutuma maombi, na wengine hadi kupeleka nyaraka za kitaaluma hapo mgodini tangu mwaka 2020 punde ulipowekewa jiwe la msingi, ila si tu hawakuteuliwa kuajiriwa bali hawakuitwa kabisa kwenye usaili badala yake wanastaajabu kuona waajiriwa ni wageni bila hata wakati mwingine kuona matangazo ya kuomba kazi humo.

Mheshimiwa Waziri,

Madai haya nimeyafanyia pia utafiti usio rasmi kwa kuwahoji "randomly" wananchi wazawa kutoka Mkoa wa Singida hususani Wilaya ya Ikungi na kipekee wengi kutoka Kijiji cha Mang'onyi ambapo mgodi upo, na kubaini madai haya yamebeba asilimia kubwa ya ukweli.

Mheshimiwa Waziri,

Jambo hili linakingana na Juhudi za Rais wetu Dkt Samia na Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi CCM za kuutangaza umma wa Watanzania kuagana na umaskini kutokana na ujio ridhishi wa Wawekezaji wa Sekta ya madini nchini.

Mheshimiwa Waziri,

Kabla ya kuendelea naomba kuambatanisha ujumbe wa moja ya vijana wasomi kutoka Wilaya ya Ikungi ambaye amenitumia kupitia mtandao wa WhatsApp Machi 02, 2023 akilalamikia madhila haya. Naomba jina lake nisilitaje, na pale anapojitaja niondoe kwa Usalama wake na kulinda faragha yake.

NANUKUU:


Hello bro,

Habari. Natumai uko poa.

Ndg Suphian, Mimi naitwa.... (jina nalihifadhi), kijana wa chama cha mapinduzi na mkazi wa Kijiji cha Puma, nilikufahamu 2020 wakati wa uchaguzi mkuu, lakini zaidi nimekufahamu kupitia machapisho yako katika kurasa za mitandao ya kijamii ukuweka bayana yale mazuri yanayo fanya na Rais wetu mpendwa, Mhe, Samia Suluhu Hassan, hongera sana Kaka.

Ndg Suphian, ni muda mrefu sasa nimekuwa nikikufuatilia na nimeona dhahiri uwezo na karama ya uongozi ndani yako! Wilaya ya Ikungi, hususani jimbo la Singida-Magharibi linahitaji watu wa kariba yako kutuwakilisha na kutusemea katika Bunge letu tukufu.

Ndg Suphian, katika wakati huu wa mpito jina na sauti yako imezidi kuwa kubwa! Mungu ameshakupa kibali, ni wakati sasa wakutafuta kibali kwa wananchi wa jimbo la Singida magharibi.

Ndg Suphian, yapo mengi yanayoweza kukupa kibali kwa wananchi wa jimbo la Singida-Magharibi, ila leo nataka niseme jambo moja tu.

Ndg Suphian, bila shaka unatambua mradi mkubwa wa uchimbaji wa madini ya dhahabu unaotekelezwa na kampuni ya Shanta gold mining Ltd ndani ya wilaya yetu ya Ikungi.

Ndg Suphian, mradi huu ni fursa kubwa kwa maendeleo ya ujumla ya wilaya yetu ya Ikungi na maendeleo ya mtu mmoja mmoja (wazawa). Pamoja na mgodi kuwa ndani ya wilaya yetu, ni vijana wachache sana wazawa (local content) walio nufaika na kupata ajira katika mgodi huu ingawa wapo vijana wengi wazawa wenye sifa za kupata ajira katika mgodi huu.

Ndg Suphian, walio stahili kutusemea wamenyamaza kimya! Ikikupendeza, paza sauti yako kwa viongozi wa chama na serikali wa wilaya ili vijana wenye sifa ndani ya wilaya tunufaike kwa mradi huu.

Kumbuka: Kuna sauti yao, halafu kuna sauti ya mteule wa Mungu Suphian Juma Nkuwi

Kwa hayo machache ya muhimu naomba kuwasilisha.

Ni mimi,

....... . (Jina nalihifadhi).

MWISHO WA KUNUKUU.

Mheshimiwa Waziri,

Raia zangu kwako;

1) Naomba uunde Kamati/Tume kuchunguza madai haya na kupata taarifa rasmi ya Serikali na kuchukua hatua stahiki.

2) Naomba Wizara yako ya madini iagize viongozi wake wakazi pamoja na Taasisi na mamlaka zingine za Serikali kuchukua hatua za makusudi kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi wazawa uliopo mgodi huu ili wafahamu haki zao na kufaidika na ushirikishwaji wa uhakika kufaidi keki itokanayo na dhahabu hii iliyovumbuliwa katika ardhi yao.

Mheshimiwa Waziri,

Napenda pia kutumia baraza hii kuwaomba kwa unyenyekevu mkubwa viongozi wa Chama changu cha Mapinduzi CCM na Jumuiya zake zote ngazi ya Wilaya ya Ikungi na Mkoa wa Singida kukupa Ushirikiano, ikiwemo kwa kufanya ziara kufuatilia jambo hili na kutafuta ufumbuzi wake kwani kulipuuza litasababisha chama chetu kukosa mvuto hao wazawa ambapo kimsingi ndio wapiga kura wetu wenye imani kubwa nasi kwa zaidi ya nusu karne sasa.

Mheshimiwa Waziri,

Nawasihi pia ndugu zetu Wawekezaji wa mgodi wa Shanta kuwa waaminifu na waadilifu kwenye eneo la kuwashirikisha na kuwaajiri wazawa kwani kinyume chake tumeshuhudia maeneo kadhaa nchini na mengi duniani yenye madini wazawa na wanaponyanyapaliwa kugeuka "mbogo", kuanzisha mgogoro na kusababisha uharibifu wa migodi na kuleta maafa yasiyotamanika. Tusifike huko.

Mheshimiwa Waziri,

Samahani na Ahsante kwa kutumia muda wako kukushirikisha jambo hili adhimu, na muda wowote utapohitaji Ushirikiano wangu kwenye hili, nipo tayari.

Katika Serikali ya Rais Samia, wananchi tunaimani.

Suphian Juma Nkuwi,
Kada wa CCM,
Mzawa wa Ikungi, Singida,
Mei 04, 2023.
Simu: +25517027973
Email: yessuphian@gmail.com

_20230504_094554.JPG
_20230504_094706.JPG
_20230504_094847.JPG
IMG_20230503_101815.jpg
 
Kampuni ni yangu halafu unipangie wa kuajir!!i, acheni kunyanyasa wageni, ndio maana wanakimbia nchi kwa manyanyaso, hii ardhi ni ya Mwenyezi Mungu tunaitumia, tunaishi, tunakufa wanakuja wengine


ALEYOMBA GEKKE acheni kunyanyasa wageni, waacheni wapumue. Life is too short bwana acheni hizo
 
Wageni wananyanyasika sana na sijaona kiongozi yeyote wa kuwasemea watu hawa, hawaishi kwa amani, mnawalipiza makodi ya ajabu, ada za kuishi, na bado mnawapangia watu wa kuajiri kweli!!! wewe kama ni kiongozi/kada wa ccm hiki kinachofanyika kwa wageni ni haki kweli!! Juzi tu hapa mwekezaji wa kampuni ya mafuta GBP bomba lake la mafuta limepasuka tena kwa bahati mbaya na sio kukusudia eti ametozwa faini ya m400, hasara amepata yeye, na faini atozwe yeye, na isitoshe ameajiri watanzania wengi tu halafu anakuja mtu from nowhere anamlipiza faini za kipumbavu, hivi hizo hela mnajua anazipata vipi!!! kama mtu anavyookota maembe eti!

aise jehanam itasomba sana watenda dhambi,,, Dhulma haimuachi mtu salama ndio maana wenye tamaa, chuki, roho mbaya, dhuluma n.k huwa hawaendelei and mwisho wa siku wanakufa na maradhi makubwa na yasiyotibika,

ALEYOMBA GEKKE life is too short bwana, fanyeni mfanyavyo kwa wageni lakini mtakufa tuu, na cha moto mtakikutananacho huko mbele

Sol de Mayo
 
Kampuni ni yangu halafu unipangie wa kuajir!!i, acheni kunyanyasa wageni, ndio maana wanakimbia nchi kwa manyanyaso, hii ardhi ni ya Mwenyezi Mungu tunaitumia, tunaishi, tunakufa wanakuja wengine


ALEYOMBA GEKKE acheni kunyanyasa wageni, waacheni wapumue. Life is too short bwana acheni hizo
Ukienfa hizo nchi zao utapata kazi? Hebu nenda hapo Kenya tu uone mtiti wa wewe mgeni kuoata kazi? Shida sijui mnawaza kwa kutumia utumbo mpana? Yaani kichwani eneo la ubongo mmejaza kamasi tupu
 
Mining jobs ni kazi za hatari sana na ni mazingira hatarishi yenye hazards nyingi sana.

Tunapozungumzia kuajiri kwenye operation hasa za miradi mikubwa kama hii ambayo investment cost zake ni kubwa sana na wahusila wanahitajo returns basi Lazima tufahamu kwenye kuajiri kunahitaji umakini na watu wenye weredi ili kazi ianze mara moja, uelekeo uonekane na faida ipatikane.

Hii ni project tayari na sio uwanja wa majaribio au sehemu ya watu kwenda kukua bali ni business inayohitaji userious na uharaka kila mahala...
 
Ukienfa hizo nchi zao utapata kazi? Hebu nenda hapo Kenya tu uone mtiti wa wewe mgeni kuoata kazi? Shida sijui mnawaza kwa kutumia utumbo mpana? Yaani kichwani eneo la ubongo mmejaza kamasi tupu

Ulishawahi kujaribu ukanyimwa kazi? Halafu hii ni mada nyingine wala haihusiani na ulichokiongea


Bhujiku ng'waka
 
Siyo hayo tuu tenda za kazi ambazo zina ratibiwa na Shanta gold iliyoko Songwe kama hujatoa hongo hata kama una sifa huoati kazi. Kitengo kinacho shughulika na kupitisha tenda kimekuwa kina fanya biashara ya hongo. Lazima mpatane bei mtakayo wapa ndipo upewe kazi. Mfano mkuu ninwanao fanya kazi TSF sasa hivi Shanta Singida na Shanta Songwe, walitoa hongo kubwa sana kupata hiyo kazi. Kama atatokea wa kubishia hili niko tayari kutoa facts zote hapa. Na walio pokea hiyo rushwa .
 
Siyo hayo tuu tenda za kazi ambazo zina ratibiwa na Shanta gold iliyoko Songwe kama hujatoa hongo hata kama una sifa huoati kazi. Kitengo kinacho shughulika na kupitisha tenda kimekuwa kina fanya biashara ya hongo. Lazima mpatane bei mtakayo wapa ndipo upewe kazi. Mfano mkuu ninwanao fanya kazi TSF sasa hivi Shanta Singida na Shanta Songwe, walitoa hongo kubwa sana kupata hiyo kazi. Kama atatokea wa kubishia hili niko tayari kutoa facts zote hapa. Na walio pokea hiyo rushwa .
Asante kwa taarifa.
 
Siyo hayo tuu tenda za kazi ambazo zina ratibiwa na Shanta gold iliyoko Songwe kama hujatoa hongo hata kama una sifa huoati kazi. Kitengo kinacho shughulika na kupitisha tenda kimekuwa kina fanya biashara ya hongo. Lazima mpatane bei mtakayo wapa ndipo upewe kazi. Mfano mkuu ninwanao fanya kazi TSF sasa hivi Shanta Singida na Shanta Songwe, walitoa hongo kubwa sana kupata hiyo kazi. Kama atatokea wa kubishia hili niko tayari kutoa facts zote hapa. Na walio pokea hiyo rushwa .
Mwaga kila kitu hadharani turuke nao
 
Wageni wananyanyasika sana na sijaona kiongozi yeyote wa kuwasemea watu hawa, hawaishi kwa amani, mnawalipiza makodi ya ajabu, ada za kuishi, na bado mnawapangia watu wa kuajiri kweli!!! wewe kama ni kiongozi/kada wa ccm hiki kinachofanyika kwa wageni ni haki kweli!! Juzi tu hapa mwekezaji wa kampuni ya mafuta GBP bomba lake la mafuta limepasuka tena kwa bahati mbaya na sio kukusudia eti ametozwa faini ya m400, hasara amepata yeye, na faini atozwe yeye, na isitoshe ameajiri watanzania wengi tu halafu anakuja mtu from nowhere anamlipiza faini za kipumbavu, hivi hizo hela mnajua anazipata vipi!!! kama mtu anavyookota maembe eti!

aise jehanam itasomba sana watenda dhambi,,, Dhulma haimuachi mtu salama ndio maana wenye tamaa, chuki, roho mbaya, dhuluma n.k huwa hawaendelei and mwisho wa siku wanakufa na maradhi makubwa na yasiyotibika,

ALEYOMBA GEKKE life is too short bwana, fanyeni mfanyavyo kwa wageni lakini mtakufa tuu, na cha moto mtakikutananacho huko mbele

Sol de Mayo

Wewe sio mtanzania.
 
Yaaan niazishe kampun yangu unilazimishe kuajiri wataalam ambao hatufahamian.....labda ungesema kaz zle ambazo hazna skills zozote kama ulizi, udereva etc ....
Kwa hyo unafikiria, ni kazi mtu anzaliwa hapo hapo anaijua ???

Ndio maana sera ya serikali, kama umeanzisha plant, inabid ulete expert kwa ajili ya kufundisha wazawa ili wakijua mitambo, wao ndio wanfanya..

Kama unasema kila mtu ajiri mtu anemfahamu, hakuna maana ya taifa na hakuna maana ya sera ya nchi kuhusu ajira...

Anywaya inawezekana uelewa wako ni mdogo sana

Sent from my M2010J19SI using JamiiForums mobile app
 
Kama ni Suala la kazi na ajira kwa wazawa na pia kupata tenda kiukwel tu sahau na ujue hakuna sehemu zenye figisu, rushwa , kujuana, wizi na pia kubaniana kama kwenye migodi we waone tu watu wanatinga. Na siyo hapo Shanta mine tu hiyo Iko migodi yote unayoijua wewe hapa Tz , na ujue waziri wako Hilo analijua vizuri na Hana Cha kufanya kikubwa plan b, Kuna nafasi huwa zinaombwa na hao hao wakubwa kwa ma GM unashangaaa mara paaa mtu amekuja na wewe upo hapo hapo, 10 percent muhimu aiseee¹
 
Yaaan niazishe kampun yangu unilazimishe kuajiri wataalam ambao hatufahamian.....labda ungesema kaz zle ambazo hazna skills zozote kama ulizi, udereva etc ....
Yaani vijana wa leo ni shida,,eti moja ya vigezo kijana ili nikufikirie kukuajiri, unaniambia mimi ni mwanachama wa CCM....Sasa si tusio na vyama itakuwaje???....kazi sekta binafsi mie naangalia ' competency' ya mtu' na sio uchawa' wako au vinginevyo!....kaazi kwelikweli..
 
Bwana Suphian Juma,
Usitumie jukwaa hili kuuchonganisha mgodi wa Shanta na Wananchi wake kana kwamba hakuna kitu shanta imefanya kwa Jamii ya Wana Ikungi.
1. Wodi ya kinamama hospitali ya Mangonyi.
2. Ujenzi wa Vyoo na Madarasa Shule ya Mwau, shule ya Mlumbi, shule ya Banda Saba.

3. Mradi wa Maji toka kisima namba 8 hadi Banda mbili.

4. Visima vitatu vinavyotumia umeme jua .

5. Marekebisho ya Uwanja wa Mpira wa Liti stadium Singida Mjini.

Yote hayo yametekelezwa na Vijana wa Kitanzania wakishirikiana na Vijana wengi wa Ikungi.
Lakini pia unapaswa utambue kuwa hayo yote yamefanyika wakati mgodi haujaanza uzalishaji. (Rejea sheria ).

Changamoto.
Vijana wengi wa Ikungi ni WAVIVU , rejea mkutano katibu mkuu wa CCM bwana Chongole alipokuja Ikungi pale kwenye mradi wa Mzungu . Walimwambia inawalazimu kutoa vibarua kanda ya Ziwa kuja kufanya kazi hapo . Maana nyie mkilipwa mshaara hamji kazini mpaka hele iishe.

Mnapenda Sana Kesi zisizo na vichwa wala miguu mahali pa kazi.

Rai Yangu.
Tembelea ofisi ya Mkuu wa Wilaya Ikungi ili uweze kupata taarifa sahihi.

Nenda pia kwa Mkurugenzi utapata kujua taratibu zote.

Ukishindwa nenda Tume ya Madini Dodoma Utapata kuelewa Taratibu za Migodi inavyotakiwa kufanya Kazi.

Kwa leo Niishie hapa.
Siku nyingine nitakuambia juu ya Madini ujenzi yote yametoka hapo hapo Ikungi.

Ni wakati sasa Tuitangazie Dunia Mazuri yaliyofanywa na vijana wa Kitanzania kwa Kujenga Mgodi Mkoani Singida (Migodi mingine yote imejengwa na Wageni).
 
Yaani vijana wa leo ni shida,,eti moja ya vigezo kijana ili nikufikirie kukuajiri, unaniambia mimi ni mwanachama wa CCM....Sasa si tusio na vyama itakuwaje???....kazi sekta binafsi mie naangalia ' competency' ya mtu' na sio uchawa' wako au vinginevyo!....kaazi kwelikweli..
Yaani ni Shida. Mwenyezi MUNGU awajalie vijana wa CCM wawe na Ufahamu
 
Wageni hawana amani kabisa na hii nchi, yani kila pahala wamebanwa yani hawapumui, muda wote wanawasiwasi na hili liserikali la kidhalimu. Hivi mnajua watanzania wangapi wameajiriwa na makampuni ya nje!!! Hivi mnavyowanyanyasa wageni na kuwabambikia makodi n.k, je! wakifunga makampuni yao na kuondoka, je! watanzania walioajiriwa ndani ya makampuni hayo wataishije kwa mfano, je!!!!! Huu upumbafu sidhani kama upo kwingine ila ni bongo tu.
 
Back
Top Bottom