Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Wana JF, hivi ikiwa hawa makaburu wanasema hawajawahi kupata faida mika 15 na kwa hivyo hawalipi kodi, je kuna haja gani ya wao kuendelea kuwepo hapo kwenye mgodi? Si bora wangeondoka afu tukawaruhusu wanaapolo wakawa wanachimba ili walau kiasi ya mboga ipatikane??
Kinachosikistisha na kushangaza zaidi ni pale Waziri Ngeleja anapotueleza kuwa Mwekezaji ndiye mwenye mamlaka ya kusema kuwa ataanza kupata faida lini na hivyo kumpa pia fursa ya kujipangia kulipa kodi. Tofauti na Mtanzania Mzawa ambaye pia ni Mtanganyika na mwenye mtaji mdogo anapoanzisha biashara yake hutakiwa kulipa kodi bila kujali kuwa atapata hasara au la. Kwani huyu yeye siyo mwekezaji? mbona tunasema kuna wawekezaji wa ndani na wa nje kwanini hawa wa ndani walipe kodi afu wa nje wasilipe kodi?
Kinachosikistisha na kushangaza zaidi ni pale Waziri Ngeleja anapotueleza kuwa Mwekezaji ndiye mwenye mamlaka ya kusema kuwa ataanza kupata faida lini na hivyo kumpa pia fursa ya kujipangia kulipa kodi. Tofauti na Mtanzania Mzawa ambaye pia ni Mtanganyika na mwenye mtaji mdogo anapoanzisha biashara yake hutakiwa kulipa kodi bila kujali kuwa atapata hasara au la. Kwani huyu yeye siyo mwekezaji? mbona tunasema kuna wawekezaji wa ndani na wa nje kwanini hawa wa ndani walipe kodi afu wa nje wasilipe kodi?