Mgodi mpya wa Tumbelo

Nelly16

New Member
May 30, 2012
1
0
Wananchi wa kondoa sasa wamepata mgodi mpya wa Tumbelo ambao unatoa dhahabu kwa sasa.Jana nilitembelea maeneo hayo nikiwa nimeambatana na Mkurugenzi wa Halimashauri ya Kondoa pamoja na Muhasibu wa Halimashauri na Mwanasheria.Tukakuta shughuli za mgodini zikiendelea.Pamoja na kuendelea kwa shughuli hizo ila mgodi huu bado unachangamoto nyingi zikiwamo hali ya usalama mgodini,Afya na barabara mbovu.Serikali kama itawawezesha wachimbaji hawa wadogo basi itakuwa imelisaidia sana taifa hili.
 

Attachments

  • Wanaapolo wakila bata mgodini.jpg
    Wanaapolo wakila bata mgodini.jpg
    189.8 KB · Views: 99
  • Gesti Mgodini.jpg
    Gesti Mgodini.jpg
    241.4 KB · Views: 70
  • Mgodi salama.jpg
    Mgodi salama.jpg
    181.4 KB · Views: 81
  • Eneo la Mgodi Tumbelo.jpg
    Eneo la Mgodi Tumbelo.jpg
    297.9 KB · Views: 101
  • Mchimbaji akitoka mgodini.jpg
    Mchimbaji akitoka mgodini.jpg
    244.2 KB · Views: 86
Mungu atupe nini Tanzania???? Kwa mawazo yangu Tanzania nzima imejaa madini ya thamani ila tumeshindwa kuyatumia vizuri kwa ajili ya maendeleo yetu.
 
Sasa hapo issue ni moja tu.........aliyegundua huo mgodi ni wananchi wenyewe..........lakini watakuja kufukuzwa kama mbwa hapo..

Subirini tu muone maajabu ya Serikali ya CCM!!!
 
Sasa hapo issue ni moja tu.........aliyegundua huo mgodi ni wananchi wenyewe..........lakini watakuja kufukuzwa kama mbwa hapo..

Subirini tu muone maajabu ya Serikali ya CCM!!!

Hifadhi ya mazingira wanatakiwa kuangalia sana maeneo haya,tumbelo ni sehemu ya mradi wa uhifadhi wa mazingira wa HADO lakini leo kijiji hiki kinageuka jangwa wakati miaka kumi iliyopita kijiji kilikuwa kikijitegemea chenyewe kwakuwa na springs nyingi kwa ufupi ni kijiji kilichokuwa na madhari ya kipekee na utajiri wa matunda ya asili kama vile majumbao machkai,mapera,makomamanga zambarau nakadhalika,si hivyo tu lakini tumbelo kwa wale waliosoma historia huko ndipo ya lipo kutwa michoro ya kale katika mapango,na leo hii pamegunduliwa madini bila shaka pana utajiri zaidi ya huo
 
Tanzania tumekosa umoja wa kitaifa,
Tuna matumaini makubwa,
kwa mkombozi tusiyemjua,
mipango yetu karibu yote,
Ni yamuda mfupi.
 
Tajiri ardhini na maskini vichwani. Bongo tunataka kuijenga kwa style ya bongo tambarale...kutengeneza mahela mengi bila kufanya kazi
 
Back
Top Bottom