Meno ya tembo 81 yakamatwa tanzania

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,331
33,141
130303065644_elephants_ivory_304x171_reuters_nocredit1_93ca2.jpg
Watu wawili wanashikiliwa na polisi nchini Tanzania baada ya kukamatwa na shehena ya meno ya tembo katika bandari ya Dar es Salaam, waliyokuwa wakisafirisha kiharamu maafisa wa nchi hiyo wamesema. (HM)



Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii wa Tanzania, Chikambi Rumisha

amesema meno hayo yapatayo 81 yana uzito wa kilo 303.


Kwa mujibu wa maafisa wa Wizara meno hayo ya tembo ni mapya ikiwa na maana yametokana na tembo 41

waliouawa ndani ya mwezi mmoja uliopita.


Naibu Waziri wa Maliasiali na Utalii wa Tanzania Lazaro Nyalandu amesema mauaji ya tembo yameongezeka

nchini humo baada ya operesheni ya kupambana na majangili iliyopewa jina la "Operesheni Tokomeza"

kusimamishwa kutokana na baadhi ya watendaji kukiuka haki za binadamu.


Mapema wiki hii Naibu Waziri huyo amesema tembo wapatao 60 wameuawa kati ya mwezi Novemba na

Decemba ikilingalishwa na tembo wawili waliouawa mwezi Octoba. Chanzo: bbcswahili


TANZANIA BILA UJANGILI HAIWEZI KWENDA KABISA KAZI KWELI KWELI IPO HAPO.

 
Hivi wa Tz kinawauma nini wachina na viongozi wetu wasikivu wakivuna meno ya tembo? Acheni roho mbaya. Viongozi wakiwa matajiri si ndio vizuri ili nanyi mpate khanga . kofia na t shirt waqt wa uchaguzi. Viongozi wanahodhi huu utajiri wa madawa ya kulevya na meno ya tembo kwa niaba yenu.
 
Wauwawe tu sioni faida yao. Hata wakichukuliwa wote haina tatizo. Watu wa hali ya chini hatuoni faida zake. Maisha kila siku yanapanda juu.
 
Baada ya miaka kadhaa tembo watakuwa historia Tanzania km ilivyo dinoserous watoto wetu wataenda ulaya kuangalia tembo Hui kali
 
Back
Top Bottom