Mengi alia na walioficha Mabilioni Ughaibuni!

JeiKei

Member
Sep 29, 2006
51
9
  • Asema Viongozi Wameficha mabillion Ulaya, Marekani
  • Ataka wanaonga'tuka, watangaze utajiri waliopata
  • Asema wapo walio madarakani, wengine wastaafu


MWENYEKITI wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi, amesema kuna kundi kubwa la viongozi wastaafu na walio madarakani, waliosafirisha mabilioni ya fedha na kuziweka katika benki za Ulaya na Marekani.

Ametoa wito kwa serikali kuhakikisha kuwa, fedha zinarejeshwa nchini ili zitumike kujenga uchumi wa nchi.

Mengi alisema hayo jana katika mjadala wa wazi wa kujadili rushwa na maadili, ulioandaliwa na Taasisi ya Kuzuia Rushwa (PCB), na kufanyika katika Hoteli ya Golden Tulip, Dar es Salaam.

"Uadilifu na heshima si vitu vya kupewa, bali unavipata katika maisha yako, naiomba serilali ihakikishe fedha zilizowekwa nje zinarudishwa nchini.
"Wanaojihusisha na biashara za rushwa na fedha haramu, na kuziweka katika mabenki ya huko Amerika na Ulaya, wazirudishe nchini fedha zote walizopata kwa rushwa, na walipe kodi, na baadaye wamrudie Mungu," alisema Mengi.

Pamoja na ‘kulipua bomu' hilo, Mengi hakuwa na ujasiri wa kuwataja viongozi wastaafu na walio madarakani ambao ana hakika wametoroshea fedha nje ya nchi.

Akijibu hoja ya Mengi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Philip Marmo, alisema: "Msiwe na wasiwasi na vyombo vya dola nchini, kama mtu yeyote anamfahamu kiongozi aliye madarakani au aliyestaafu, aliyeweka fedha nje, amtaje na serikali itamshughulikia, na hata kama hakutaja jina la kiongozi, basi ataje hiyo taasisi ya fedha ya nje."

Mengi hakuishia kwenye hoja hiyo pekee, bali aligusia pia ufisadi miongoni mwa viongozi wa umma.

Alisifu utaratibu wa kisheria wa viongozi kutaja mali wakati wakiingia madarakani, lakini akasema utaratibu huo hautakuwa na maana kama viongozi wanashindwa kutaja ukwasi wanaoondoka nao baada ya kustaafu.

"Tunataka viongozi wataje mali mwanzoni wanapoingia madarakani na mwishoni, tunataka kujua wana nini, hatuna wivu, na hii ndiyo itakuwa njia sahihi ya kudhibiti rushwa kwa viongozi," alisema Mengi.

Maoni ya Mengi yanashabihiana na maoni ya wengi, ambao wamehoji mno kitendo cha viongozi katika awamu iliyopita, kutotangaza hadharani mali walizoondoka nazo.
Rais msaafu Benjamin Mkapa; na Waziri Mkuu, mstaafu, Frederick Sumaye, walitangaza kwa mbwembwe mali zao wakati wakiingia madarakani mwaka 1995, lakini hawakutaja ukwasi walioondoka nao miaka 10 baadaye.

Katika mjadala huo, Ofisa Uhusiano wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Josephine Mwakyuse, alisema pamoja na PCB kujitahidi kupambana na rushwa, imekuwa vigumu kufuatilia ushahidi kwa wale wanaoomba rushwa ya ngono, jambo linalosababisha wanawake kuendelea kukandamizwa.

"Ndugu Mwenyekiti, iko wapi haki ya mwanamke anapodaiwa rushwa ya ngono? Kuna ofisa mmoja wa jeshi amemsimamisha kazi na hatimaye kumfukuza kazi mwanamke kwa madai ya kuwa na matatizo ya akili, lakini baadaye imegundilika kuwa yule mama ni mzima ila alikataa kutoa rushwa ya ngono kwa mkuu wake wa kazi. Je, PCB itamsaidiaje mama huyu?" alihoji Josephine.

Akijibu hoja hiyo, Marmo alisema kukamatwa kwa mtuhumiwa wa rushwa ya ngono inategemea ushirikiano atakaotoa mwanamke anayeombwa rushwa, kwa kuwa si rahisi kumkamata kama ilivyo kwa rushwa ya fedha.

Akizungumzia zawadi zinazotolewa kwa watumishi wa serikali pindi waendapo vijijini au nje ya nchi, Marmo alisema kuwa utaratibu unamtaka mtumishi kuchukua sehemu ndogo ya zawadi na nyingine apeleke serikalini.

Washiriki waliomba serikali iipe madaraka PCB kwa kuwa hali ilivyo sasa haikiwezeshi chombo hicho kufanya kazi zake kwa uhuru.

"PCB wamebaki na sera, lakini hawana uwezo wa kumkamata ofisa wa polisi anapopokea rushwa, wamekuwa kama jogoo mkubwa aliyewekwa ndani ya tenga, hata akiwika hatanui mabawa, na wananchi sasa tuko katika gari ambamo sote ni viwete, lakini dereva na konda ndio wazima.

"Tunaisaidia PCB, lakini wao hawako tayari kutusaidia, hasa tukiwa na ushaidi wa polisi kupokea rushwa," alisema Mchungaji Nkuba ambaye alisema ni muathirika wa vitendo vya PCB kushindwa kuwakamata polisi.

Nkuba alisema aliwasilisha vielelezo vyote PCB vinavyohusu polisi waliomuomba rushwa, lakini badala yake hawakufanywa kitu, na sasa anatishiwa maisha, kiasi kwamba familia yake imesambaratika na yeye anaishi katika kijiji ambacho hataki kukitaja kwa kuhofia usalama wake.

Mkurugenzi wa PCB, Edward Hosea aliwataka wananchi kuwa na imani na taasisi yake kwa kuwa sasa inafungua ukurasa mpya.

Amewaagiza maofisa wa taasisi hiyo nchini kote, kuweka hadharani namba za simu ili waweze kuwasiliana na wananchi.


CHANZO: Tanzania Daima - ISSN 0856 - 9762 Toleo Na 733 - Jumatano, Desemba 6, 2006
 
mjomba nadhani unajua kuwa topiki za huyu mheshimiwa haziwekwi kwenye website hii kwa sababu ambazo ziko nje ya uwezo

Unaweza ku argue kuwa hii ni different topic lakini hebu nenda kwenye kabrasha utaona


chonde mwaya
 
DRWHO

Tumekusikia mtoa hoja kuhusu topick za Muh.Mengi kuwa katika forum hii ni wananchi wanatoa maoni yao kwa kila mtu wanaye mzania kuwa ni tunda la taifa hili,sioni kama kuna kosa muh. huyo kuandikwa humu.

Ninatumaini kwamba kama umefanya vizuri katika maisha yako basi watu wata kuandika kwa uzuri kama ni upande wa pili basi watakuandika hivyo hivyo,tunachotaka sisi watoto wetu wajue kila mtu maarufu historia yake kama vile wakina Mkwawa,Vasco Dagama Nyerere, na wengine wengi.

kama tutachagua watu wakuwaandika humu basi hii forum hifungwe haina maana lengo letu wajuwe kwamba tuna juwa wanacho kifanya siyo kuogopa mtu,kama waeshimiwa kama kina Mbowe Kikwete Lowassa wanaandikwa tena vibaya hawasemi kitu sasa Mengi ananguvu kuliko Kikwete.

Hi forum hakuna wakuifunga kwanza hatu mjui mwenye forum hii sasa tunaogopa nini aandikwe kama watu wengine,hii tekinolojia siyo MAGAZETI,TV,AU RADIO kwanza akuna sheria yakumshitaki mtu unapo andikwa ONLINE.ninarudia tena kama ulifanya mazuri uko uliko toka utaandikwa vizuri huko unako kwenda ;kama ni upande wa pili basi subiri majibu

Naomba kutoa hoja

by king
 
King
mheshimiwa huwa haandikwi humu na hii topik tukianza kuchangia. itafutwa,
hii forum imenunuliwa na Mzee Mengi sio jamvi huru kama unavyofikiria.
tunayo Mengi ya Mzee Mengi. ila hatuna pa kusemea.si kweli hii habari aliyoisema kwani yeye anahusika ktk hayo.
kuna deal na Sumaye kati yake. nikipewa ruksa nitaweka wazi. kuona kuwa kauli yake ni dhihaka kwa watanzania.
 
DrWHO,
Lakini this is a news item. Haimzungumzii Mengi as such but Mengi as a news maker. We can discuss the content of his message without discussing the man, no?
 
King
mheshimiwa huwa haandikwi humu na hii topik tukianza kuchangia. itafutwa,
hii forum imenunuliwa na Mzee Mengi sio jamvi huru kama unavyofikiria.
tunayo Mengi ya Mzee Mengi. ila hatuna pa kusemea.si kweli hii habari aliyoisema kwani yeye anahusika ktk hayo.
kuna deal na Sumaye kati yake. nikipewa ruksa nitaweka wazi. kuona kuwa kauli yake ni dhihaka kwa watanzania.

CHINGA

Nimekusikia mtoa hoja CHINGA hii forum sasa mimi ninakuakikishia hakuna hanaye jua hii forum niya nani,labda niwaeleze hii forum Mengi hawezi kuifunga hii forum niya WANAMTANDAO wako nje ya nchi wala Mengi hawajui naimeanzishwa makusudi kuwafichuwa ,WAUZA UNGA ,MAJAMBAZI, WALARUSHWA WAUJUMU UCHUMI,VIONGOZI WENYE SIFA MBAYA ,MENGINE MENGI

CHINGA unaruhusiwa kuandika kitu chochote katika forum hii tafadhali usichaguwe watu.
Rukusaaaaaaaa

Naomba kutoa hoja

by king
 
KIINI MACHO KINGINE?


Akijibu hoja ya Mengi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Philip Marmo, alisema: "Msiwe na wasiwasi na vyombo vya dola nchini, kama mtu yeyote anamfahamu kiongozi aliye madarakani au aliyestaafu, aliyeweka fedha nje, amtaje na serikali itamshughulikia, na hata kama hakutaja jina la kiongozi, basi ataje hiyo taasisi ya fedha ya nje."



Hiki ni kiini macho, hawa viongozi sasa wanataka kuwaambia watanzania kuwa mambo ni safi.

Philip Marmo – unataka kuwaeleza nini wananchi wakati rais amepewa majina miezi miwili imepita mpaka leo hakuna hata kigogo mmoja aliyeshitakiwa? Mbona mmeficha majina kwa watanzania? Sio wote wajinga – mmekaa mkao wa kula ndio maana hakuna maendeleo yoyote. Kila kukicha ahadi zisizo na msingi. Kwa kukukumbusha tu ni ahadi ngapi uongozi huu umeshindwa kutimiza?

Nini kazi ya BOT, PCB, police etc. kama haiwezi kuangalia transactions zinavyopita katika system na uhamishaji wa pesa haramu kupitia benki zetu wenyewe. Unahitaji western countries waje kukufanyia kazi wakati mambo yote yanatokea nyumbani kwako. Kazi tunayo bro.

Kupewa majina ni jambo la unafiki tu ambalo halisaidii kitu. Kwa nini hamnyamazi na muendelee kula bila kuwapa wananchi upuuzi huu.

Time will come when all your evil deeds will be exposed!!!!
 
nadhani tusifanye hasira kwa sababu mimiupande wangu ninaelewa nini kilichotokea na natumai tangu hii habari ya Mbowe naye kujimwaga humu website hii imekuwa na Trafiki ya ajabu hivyo inaweza ikawa ina impact

Wengi wenu mnaotaka kusema kila kitu mko nje na hamjui presha ya namna gani hawa jamaa wa Jambo forums wanapata tokea zile topiki z Mengi ,NSSF,Manji,CRDB na pesa za miradi UKIMWI za UNAIDS


JASUSI,
Nimekuelewa lakini pia vile vile usisahau kuwa tukianza kuzungumzia contents za hiyo thread hapo juu tutajikuta tumeingia katika mambo yale yale yanayopelekea threads za Mengi kuondolewa

Inasikitisha na sidhani kama uamuzi mzuri ila to be fair naelewa where hawa jamaa wa JAMBO FORUMS are coming from ndio maana hapo nyima tuliambiana kuwa tuwe standby kwa maana siku itafika ambako hii website itafungwa tu

Of course tunaweza kukimbilia kwa mwanakijiji na kwingineko lakini je watahimili hiyo mikwara?
 
Back to topic

Hivi kuna uharamu gani kiongozi au mtu yoyote wa serikali kuwa na account nje ya nchi au ndio tunatafutana uchawi tu?

kwani katiba inakataza hilo? kama halikatazi then lets bring some issues kama inakataza then tutaliangalia hilo vile vile maana tukifanya mchezo tuanza kuulizana kwa nini huyu ana wake wanne na huyu hajaoa sasa hiyo si namna ya kwenda
 
nadhani tusifanye hasira kwa sababu mimiupande wangu ninaelewa nini kilichotokea na natumai tangu hii habari ya Mbowe naye kujimwaga humu website hii imekuwa na Trafiki ya ajabu hivyo inaweza ikawa ina impact

Wengi wenu mnaotaka kusema kila kitu mko nje na hamjui presha ya namna gani hawa jamaa wa Jambo forums wanapata tokea zile topiki z Mengi ,NSSF,Manji,CRDB na pesa za miradi UKIMWI za UNAIDS


JASUSI,
Nimekuelewa lakini pia vile vile usisahau kuwa tukianza kuzungumzia contents za hiyo thread hapo juu tutajikuta tumeingia katika mambo yale yale yanayopelekea threads za Mengi kuondolewa

Inasikitisha na sidhani kama uamuzi mzuri ila to be fair naelewa where hawa jamaa wa JAMBO FORUMS are coming from ndio maana hapo nyima tuliambiana kuwa tuwe standby kwa maana siku itafika ambako hii website itafungwa tu

Of course tunaweza kukimbilia kwa mwanakijiji na kwingineko lakini je watahimili hiyo mikwara?

DRWHO
Mimi ninadhani wewe unakuwa muoga wewe uko nchi gani? kwanini una sita sita bro. kilakitu tunacho weka huku kiko kwenye gazeti sisi kazi yetu ni kunukuu na kuchunguza kama nikweli na tunauliza humu kwenye forum je nikweli? huyu mtu kafanya au vipi.

sasa wewe hakuna kitu chochote cha Mengi kilicho ondolewe humu vipi vitafute kwa jina lake utaviona haogopewi mtu huku ndani ni kama Gerezani.

kila mtu amekuja na makosa yake, nikama bungeni kila mbunge anatoa hoja yake ametumwa na wapiga kura wake, sasa basi mimi humu nimetumwa na kijiji.

naomba kutoa hoja

by king
 
OFF TOPIC

William najaribu kuweka AVATAR lakini naona inagoma

nishajaribu kuwekakibao lakini wapi na naona admin kaweza kazima iwe 100x100 pixels na picha yangu ni 80x80 hivyo it should fit au mtandao umeroga?
 
DrWHO,
Mie naona tushapewa assurance, may be a new starting, kuwa mambo yako shwari sasa, maana huyu KING anasisitiza, na sio mara moja, sasa unataka akwambie kabisa yeye ndiyo JK? It comes with a new style! Ruksaaaaaaa!
 
Mengi anaongoza kwa uharamu wa biashara yake .Ndiyo maana nashangaa kama kweli vita vita ua udhalimu rushwa nk itaisha Tanzania .Kuna mambo mangapi Mengi anaidaiwa kuhusika na wala si Hosea wa DCI kaamua kusema hatima ya uchunguzi wa madai yake ? Hapa tunachezewa na Mengi ni hatari mno kwa Taifa letu .
 
Wazee dou see any sense here? Akizungumzia zawadi zinazotolewa kwa watumishi wa serikali pindi waendapo vijijini au nje ya nchi, Marmo alisema kuwa utaratibu unamtaka mtumishi kuchukua sehemu ndogo ya zawadi na nyingine apeleke serikalini. What does sehemu kidogo mean, or its a loop hole ya ulaji?
 
DrWHO,
Kuwa na fedha katika benki ya kigeni kwa baadhi ya nchi kama vile Israel ni illegal. Kwa Tanzania sijui. Lakini point ni kwamba kwa ile mishahara ya nyumbani kweli realistically waziri anaweza kutimiza mahitaji yake na kubakia na fedha za kutosha kuweka katika benki za kigeni? I think the answer is no. Kwa uelewa wangu, wengi wa wale walioweka fedha nje ni wale ambao wamezipata kwa njia za rushwa. Na sababu ya kuweka fedha nje ni kwamba hawataki wajulikane wana fedha nyingi. Jiulize why? Because the following question will be wamezipataje.
 
DrWHO,
Kuwa na fedha katika benki ya kigeni kwa baadhi ya nchi kama vile Israel ni illegal. Kwa Tanzania sijui. Lakini point ni kwamba kwa ile mishahara ya nyumbani kweli realistically waziri anaweza kutimiza mahitaji yake na kubakia na fedha za kutosha kuweka katika benki za kigeni? I think the answer is no. Kwa uelewa wangu, wengi wa wale walioweka fedha nje ni wale ambao wamezipata kwa njia za rushwa. Na sababu ya kuweka fedha nje ni kwamba hawataki wajulikane wana fedha nyingi. Jiulize why? Because the following question will be wamezipataje.

nilifungua akaunti Halifax kwa paundi 10 sasa sidhani mtu kama Dialo ambaye alikuwa mfanyabiashara atashindwa kuwa na paundi elfu 1,000 kufungua akaunti wakati inawezekana kapinga wazungu kwenye nyumba yake wanamlipa dola elfu 4 kwa mwezi
 
Mengi anajua wazi Mkapa ana nyumba south Africa ya kukata na shoka.

Mengi ataje na mashamba ya Mkapa aliyonunua hivi karibuni Canada.
asituletee upuuzi, yeye ndiye mtu wa kati wa watu hawa,
ilikuwaje Mengi akamsomesha Mtoto wa Sumaye -UK?

JEE walivyomzima Mzungu wa U.K POUND milion 3.5 akishirikiana na kaka yake Benjamin si serikali ndiyo iliyomkingia kifua? mbona kasusura ananyea debe?
 
Wazee dou see any sense here? Akizungumzia zawadi zinazotolewa kwa watumishi wa serikali pindi waendapo vijijini au nje ya nchi, Marmo alisema kuwa utaratibu unamtaka mtumishi kuchukua sehemu ndogo ya zawadi na nyingine apeleke serikalini. What does sehemu kidogo mean, or its a loop hole ya ulaji?

Jamani mimi naona tungoje tu Yesu au Mtume SAW aje kutuokoa maana hawa viongozi wetu...my God..sometimes wanawaza utadhani wana maji kichwani. Kiongozi muadilifu na mwenye akili timamu hawezi kuwa na sera kama hizi...halafu eti huyu ndio Waziri wa Nidhamu...yaani wafanyakazi wote wa sirikali wanamuangalia yeye, akifungua mdomo ndio yanatoka haya.

Mimi naona Bunge letu tukufu lipitishe sheria ya kupima viongozi akili kabla hawajapewa madaraka...pengine wakina Dito, Marmo, Sumaye wasingekuwa viongozi kabisa.
 
nilifungua akaunti Halifax kwa paundi 10 sasa sidhani mtu kama Dialo ambaye alikuwa mfanyabiashara atashindwa kuwa na paundi elfu 1,000 kufungua akaunti wakati inawezekana kapinga wazungu kwenye nyumba yake wanamlipa dola elfu 4 kwa mwezi

Dr WHO,

Siwezi kuamini kama kweli unadhani Mengi anazungumzia akauti ya paundi 1000 au 10,000...!!!???

Anazungumzia zile nyumba 4 za waheshimiwa pale Golders Green (London) + akauti ya waziri mmoja mtoto wake ali-renew visa na BS yenye balance ya paundi 150,000 ya Stanbic Bank + wengine wengi tu...Ikiwa ni pamoja na ile 29% ya 50mil USD ya dili la Jet ya raisi ambazo zimehifadhiwa Uswiss.
 
Back
Top Bottom