Membe: Musiba na Mchange anayewatuma kunichafua kwanini hamnipeleki mahakamani? Kama mnaweza kunirekodi mmeshindwa nini kutoa huo ushahidi

Haahaa dunia kweli duara, aliyekuwa waziri Wa mambo ya nje Leo analalamika kama sie RAIA.hili Ni somo kwa waliopo madarakani Leo wasidhani watadumu mamlakani milele.Ila membe kwa misemo hatari, eti wabwekaji Wa taifa.

Ni kweli cyprian Musiba na huyo mchange wanabweka hovyo hata Heche aliwahi kuwalalamikia kuwa walimbwekea akiwa break point anapata msosi lakini akawakabili vilivyo na kuwambia haogopi kufa wala chochote
 
Mchange wakati mwingine eti hujidai ni Afisa Usalama wa Taifa kasahau kuwa ipo siku utawala huu utamaliza mda wake utaenda na yeye yupo mtaani tu
 
Wabwekaji wa Taifa..!! Mmh ngoja niingize kwenye hansard yangu.. Kwa hiyo hata mm ninaemtetea usiku na mchana Mh. Rais wangu Magu ni mbwekaji wa Taifa.?

Cyprian Musiba ni kibwekaji tena kinabweka baada ya kuvuta Bangi
 
Wabwekaji wa Taifa..!! Mmh ngoja niingize kwenye hansard yangu.. Kwa hiyo hata mm ninaemtetea usiku na mchana Mh. Rais wangu Magu ni mbwekaji wa Taifa.?
Hivi huwa mnamtetea rais dhidi ya nani na kwa nini?Je kumtetea na kumkinga ili asikabiliane na waajiri wake mnamaanisha kwamba hatoshi kwa nafasi aliyoiomba mwenyewe,au ni ujinga wenu tu?
 
Anaandika Bernard Membe.
Rondo- Lindi.

Watanzania Wenzangu! Nawasalimia! Kwa siku tatu mfululizo magazeti ya makuhani wa fitina na unafiki Musiba na Mchange na wenzao wamekuwa wakinishambulia kwa uchochezi wa sintofahamu iliyotokea kuanzia Alhamisi tarehe 17 Octoba siku ambayo Mhe Rais ameondoka Lindi kuelekea Dar hadi Jumapili ya tarehe 20. Mimi nipo Kijijini kwangu Rondo kwa mwezi mmoja sasa.

Ni nini hicho nilichokisema au kukiandika kwenye mitandao ya kijamii? Kwa kuwa mawasiliano yangu yote nayafanya kwa simu yangu ambayo inasikilizwa na kudukuliwa, naviomba vyombo vinavyohusika vitoe hadharani mazungumzo na maandishi yangu ili watu wasikie, wasome na wanihukumu. Napenda niuhakikishie umma kuwa Mimi sikuwa mjinga! Nilijua kuwa nikisema au kuandika vibaya, wabaya wangu wataninyooshea vidole.

Sikuingia kwenye mitego yao hiyo. Mimi kama Watanzania wote wenye akili za kawaida nilishangazwa sana na ukimya wa Serikali huku damage na rumours zikiwa zimetanda kote nchini bila kuzitolea maelezo kwa siku 3 mfululizo! Mhe. Rais ni kiongozi wa Umma. Inapotokea sintofahamu au upotoshaji wowote ule, ulikuwa ni wajibu wa Msemaji wa Ikulu au wa Serikali kukanusha na kuweka mambo sawa kama wanavyofanya siku zote.

Vinginevyo wale wenye akili za mbilikimo na makuhani wa unafiki wanachukua mwanya huo kutunga ya kwao ili kumfurahisha Mhe. Rais. Good governance requires quick response to rumours. Rumours left unattended damages governance! Narudia! Naviomba vyombo husika vitoe hadharani nilichokisema au kupost kwenye mitandao ili nihukumiwe na Wananchi wenyewe na sio na Wabwekaji wa Taifa.

Ben Membe.
Rondo- Lindi.View attachment 1241102View attachment 1241103
Wabwekaji wa Taifa na matumbo yao, jitu zima likishakuwa livivu la.kufanya kazi likajipatia kipato, linaishia kuwa liilmba kwaya za kuwafurahisha maditete na kujiaibisha
 
Sikubaliani na Membe.

Ilichokifanya serikali nadhani ndicho kilikuwa sahihi.

Kwamba, tetesi za kijuha na kipumbavu, ni vyema kuzipuuza kwa maneno lakini pia kuzijibu kwa vitendo ndani ya muda mzuri.

Rais kujitokeza na kuendelea kufanya kazi zake, lilikuwa ni jibu murua kabisa kwa majuha wote walioshiriki kutunga na kueneza uzushi wao.

Hivyo ndivyo inavyotakiwa.

Msemaji wa serikali akianza kujibu kila aina ya uzushi, kufanya hivyo ni kuubariki na kuuhalalisha uzushi huo. Serikali itafanya hivyo kwa mangapi? Maana uzushi na uongo ni sehemu kubwa sana ya hii mitandao ya kueneza na kujazana ujinga.

Safi sana serikali. Safari hii mmetenda vyema.
Ulikuwa wapi wr mnafiki mbona ulipotea baada ta kufufka na wewe umeibuka kama mzuka. hahhaaaa wanafiki nyie.
 
Membe arudishe tu mabilion ya Watanzania aliyopora kutoka libya

Jamhuri ikiamua kumshitaki atafilisika


Pia sio vizuri kuwatumia vijana kubweka mtandaoni kuisema serkali

Tuendelee kumuunga mkono mh Rais Kwa uchapa kazi
hatuwezi kumuunga mkono Dikteta
 
Huyu nae anatishia “kunuka” akiguswa afu anaishia “kunukia” tu!
Angetuonesha ‘advataiz’ moja kwa Musiba au Mchange pale,’amnukishe’ weeee hadi ashike Adabu yake.Otherwise nae debe tupu
 
Membe nae anajishushia hadhi kukaa anajibishana na Musiba. Kwa hadhi alostaafu daaah! Make anaongeeea serikali imemnyamazia tu, hata chama kimemdharau tu! Yaani saizi yake ni Musiba dharau kubwa hii! Ha ha ha!
 
Sikuingia kwenye mitego yao hiyo. Mimi kama Watanzania wote wenye akili za kawaida nilishangazwa sana na ukimya wa Serikali huku damage na rumours zikiwa zimetanda kote nchini bila kuzitolea maelezo kwa siku 3 mfululizo! Mhe. Rais ni kiongozi wa Umma. Inapotokea sintofahamu au upotoshaji wowote ule, ulikuwa ni wajibu wa Msemaji wa Ikulu au wa Serikali kukanusha na kuweka mambo sawa kama wanavyofanya siku zote.

Vinginevyo wale wenye akili za mbilikimo na makuhani wa unafiki wanachukua mwanya huo kutunga ya kwao ili kumfurahisha Mhe. Rais. Good governance requires quick response to rumours. Rumours left unattended damages governance!

KWA PARAGRAPH HIZO HAPO JUU
MOJA KATI YA HAYA NI KWELI

1. Baada ya kuona serikali imeamua kufuata kile marehemu Mzee Samweli Sita alichosema nanukuu " dawa ya mpuuzi ni kumpuuzia" hivyo mwendelezo wa fitna yenu ikawa imegonga mwamba.

Au

2. Kwakua umewahi kujinasibisha kwa jeuri kipindi simu yako ilipodukuliwa kwamba nanukuu " sauti Ile Ni ya kwangu" na hukuchukuliwa hatua yoyote, Sasa umeamua kuudhihirishia umma wa watanzania kwamba hutishwi na wala humuogopi yeyote.

MZEE WANGU
Naomba nikusimulie kisa maarufu katika uislamu cha Bwana mmoja wa kuitwa Qaarun huyu alikua na mali ambazo farasi wapatao saba ndio waliokua wakitumika kubeba funguo kufungulia maghala ya mali. Akaleta jeuri, aliye juu yetu sote alimfilisi na kuwa ombaomba na hatimaye kufa masikini.

Inawezekana Wana CCM wenzako wakawa wanakutizama ukadhani hawatafakari uyafanyayo bali, wanakusukia mtego siku moja utanasa na ndipo habari yako itakua imeishia hapo, muda hautoshi ningekukumbusha kilichomtokea Joshua Nasar huyu akijifanya mwana intelijensia akarekodi akakusanya ushahidi kwa njia ya sauti na video badala ya kuwasilisha kwa mamlaka husika akaweka mtandaoni ushahidi ukawa umeharibika, kishapo wakamuweka kwenye kilengeo akaingia wakala kichwa na Mh. Tundu Lissu akachonga akazunguka ulaya na amerika akabwata hakujibiwa akajiona mshindi akategwa akaingia mtekoni kichwa kikaliwa na sasa hata kurudi nyumbani anaogopa.

NI HAYO TU.
 
Waziri alimkanya Musiba, lakini Musiba ameendelea kuisemea serikali na hachukuliwi hatua, maaskofu waliiuliza serikali ikiwa haimzuii Musiba na wengi wanaamini serikali inamtuma, kwanini serikali isijitenge naye na asiruhusiwe kuisemea serikali, na imchukulie hatua.
Waziri alimuonya hadharani na alisema akirudia vyombo vya dola vita mshughulikia.
Tunaona tena kafanya yale yale, sasa tusemeje?! Uhakika upi ungekufaa wewe?!
Yaani uko dunia gani Musibaaaaaaaaa njoo huku kuna huyu tena
 
Huyu nae hajakoma tu?

Alisema nchi imegawanyika vipande na haviungwi tena akapuuzwa akaaibika.

Sasa amekuja na ngonjera nyingine?

Hii muvi JPM kaijua kuicheza, wapo walitaka kupata popularity kupitia hii muvi ila wamechemsha.

Membe kaja kivingine hadi anatia huruma.

Huyu anakurupuka kujibu kila kitu hafai hata kuongoza nyumba mbili.
 
Back
Top Bottom