Wa kusoma
JF-Expert Member
- Jul 30, 2011
- 3,454
- 2,975
Membe ameyasema hayo akiwa Mpanda mkoani Katavi, kwamba mpaka sasa roho yake inadunda mapigo mawili Pinda/membe ana uhakika akishinda yeye ameshinda Pinda akishinda Pinda ameshinda yeye
===================================
Chanzo: Mwananchi
===================================
Mjini Sumbawanga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe amesema kwamba katika kinyang'anyiro cha urais ndani ya CCM mtu anayemnyima usingizi ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Membe alisema kuwa iwapo Pinda asingechukua fomu ya urais, angekuwa anafurahia ushindi tu.
Akizungumza kwenye ukumbi wa CCM Sabasaba, Membe alisema kuwa Waziri Pinda ni mtu mchapakazi, asiye mbinafsi, mwadilifu, mvumilivu sana mwenye hekima na busara ya hali juu, mwanasheria aliyebobea na ndiye mwalimu wake ambaye alimfundisha kazi.
"Wengine wote hawanitishi nitawagonga, nitawagonga, lakini nikifika kwa Pinda itabidi nipumue kwanza. Kwa hiyo mimi na Pinda ni pacha nikishindwa mimi nitamuunga mkono," alisema Membe ambaye pia aliwahi kusema atamuunga mkono Profesa Mark Mwandosya.
Awali, katibu uenezi wa chama hicho mkoani hapa, Clement Bakali alisema Membe amepata wadhamini 855.
Chanzo: Mwananchi