Mpambano bado unaendelea kati ya Timu ya CCM na CDM. Mpaka sasa CCM wameshabadilisha wachezaji (CC) lakini bado wanazidiwa kimchezo.
Mechi ya kwanza CCM wamashapoteza baada ya kuleta Muswada wa Mapitio ya katiba wakati watu wanataka katiba mpya. Hata muswada huo pamoja na kwamba unazungumzia kitu kingine kabisa, tofauti na kile ambacho wanataka wananchi, ulikuwa na kasoro nyingi. Hapo CCm imerudi nyumbani ikiwa imepigwa bao moja kwa zero.
CCM wameamua kucheza kwa mtindo wa kujivua gamba. Kujivua gamba kunaweza kusisaidie CCM kwani mpaka sasa wanacheza mchezo wa kujilinda na siyo kushambulia. Jana wakati timu CCM inajilinda Dar wenzao CDM wanashambulia Tabora. Kwa ushauri wangu CCM waende wakalinde goli Tabora kwani mashambulizi ya CDM kule Tabora ni makali.
Tunaendelea kutazama mchezo unavyoenda. Tutaendelea kupeana matokeo.
Mechi ya kwanza CCM wamashapoteza baada ya kuleta Muswada wa Mapitio ya katiba wakati watu wanataka katiba mpya. Hata muswada huo pamoja na kwamba unazungumzia kitu kingine kabisa, tofauti na kile ambacho wanataka wananchi, ulikuwa na kasoro nyingi. Hapo CCm imerudi nyumbani ikiwa imepigwa bao moja kwa zero.
CCM wameamua kucheza kwa mtindo wa kujivua gamba. Kujivua gamba kunaweza kusisaidie CCM kwani mpaka sasa wanacheza mchezo wa kujilinda na siyo kushambulia. Jana wakati timu CCM inajilinda Dar wenzao CDM wanashambulia Tabora. Kwa ushauri wangu CCM waende wakalinde goli Tabora kwani mashambulizi ya CDM kule Tabora ni makali.
Tunaendelea kutazama mchezo unavyoenda. Tutaendelea kupeana matokeo.