Hapo mama lema kweli huna mume. Nakushauri usijiingize kwenye huo mchezo wa mumeo maana kule jela hakufai. Kuna wanaume wana miaka kibao hawajui wake.Taarifa za sasa kutoka Arusha ni kwamba Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi Arusha na kuhojiwa kwa tuhuma za uchochezi wa vurugu za Wanafunzi wa chuo cha Uhasibu dhidi ya Mkuu wa Mkoa Arusha juzi.
Taarifa za uhakika kutoka kwa mke wa Mh. Lema sasa hivi ni kwamba Polisi wamekataa kutoa dhamana yake na kusema mpaka jumatatu ndio itajulikana.
Namkariri Mke wa Lema akiongea na TheTZA millardayo.com akisema jana usiku saa sita kasoro watu walikuja kugonga nyumbani kwetu tukamtuma kijana aende kutazama ni kina nani, aliporudi akasema ni Polisi.. sisi hatukuamini na tulikataa kwa sababu hatukujua kama ni Polisi kweli au ni watu wanataka kuitumia hiyo nafasi kufanya uhalifu, mimi nimeshinda Polisi kutwa nikifatilia gari mbona chochote hakikutokea?
Baada ya muda kusogea ikabidi Lema aanze kuwapigia marafiki, jamaa na baadhi ya viongozi wa Chadema, kabla ya hapo pia tuliamua kupiga kengele ya kampuni ya security ambao muda mfupi baadae walikuja na gari yao huku Polisi wakiendelea na vitisho kwamba watapiga mabomu na kuvunja ukuta la sivyo Lema ajisalimishe, Viongozi wa Chadema na marafiki walipowasili wakamshauri Lema ndio akajitokeza wakati huo ni saa tisa usiku Mama Lema
Alipojitokeza Polisi walimchukua na mimi nikaondoka nao, tulipofika kituoni walimtaka Lema kutoa maelezo lakini alikataa na kusema mpaka mwanasheria wake aje hivyo akapelekwa rumande, asubuhi tulipoamka na kuanza kufatilia.. R.C.O alisema yuko kwenye kikao na haongei na yeyote isipokua Mwanasheria wa Lema, walipomaliza kikao saa nane maelezo yakaanza kutolewa huku Mwanasheria akiwepo na kazi ikamalizika jioni saa 11 ambapo Polisi wamekataa kutoa dhamana mpaka Jumatatu Mama Lema
shitaka kubwa lililo mbele yake ni uchochezi na kauli ambayo anadaiwa Lema kuitoa mbele ya Wanachuo cha Uhasibu kwamba dhambi kubwa kuliko zote ni uoga, na hata leo kwenye maelezo Lema amewaambia watu wa Arusha mjini hivyohivyo, kwamba dhambi kubwa kuliko zote ni uoga Mama Lema
Kwa kumalizia, Mke wa Mbunge Lema amesema gari letu lililokua linashikiliwa na Polisi tumerudishiwa baada ya kutakiwa kulipia elfu 50 ya wale waliolivuta, gari liko zima kabisa toka nimeolewa na Lema nimeshuhudia akienda polisi zaidi ya mara 20, mara yake ya kwanza kushuhudia anapelekwa polisi ni wakati wa kampeni za Ubunge
Umeambiwa kuwa kilichompeleka lema lumande ni maneno yake ya uchochezi. Hapo mulongo anainiaje?HIVI Mulongo ana akili ndogo namna hiyo? Mbona kumkomoa mtu kwa kumweka rumande ni mambo ya kizamani na ushamba? Lema atatoka na hapo amempandisha chati na tunajua hiyo kesi ni nyepesi atashinda kwa sababu aliyeleta vurugu ni Mkuu wa mkoa na Mungu atashughulika naye.
ndugu AKA2030
umejiunga juzi tu Join Date : 5th January 2013
Posts : 233
Rep Power : 432
Likes Received36
Likes Given0
mleta mada ni wa tangu 2007 maribu miaka kumi
kama huna cha kuchangia bora ukae kimya au kwa vile umeahidiwa unapojibu post
ndivo utakavolipwa Lumumba? ok kachukue mshiko wao
sheria za JF soma vizuri usiwe na mdomo refu kama mbayuwayu.
Mtoa mada asante kwa taarifa
Viongozi wa chadema asilimia 80 wanakunywa na kula bangi.
Ndio ila udikteta wa kishamba sana. Kwani polisi walipeleleza wakagundua ana makosa gani? Au ni kiasi tu cha mkuu wa mkoa kuamua kamata fulani weka ndani? Mtu mmoja anawatishia nyau watu milioni?inasikitisha sana, tz tuna watawala madikteta
kuna mzee mmoja mwanajeshi mstaafu alikuwa studio za chanel ten asubuhi nilimpenda sana kwani anaijua dunia hii vibaya na alisema ukiona serikali inatumia mabavu ujue mwisho umefika.
haya ya lema kama ni siku ni saa kumi alfajiri.
Hamna kesi hapo!
Hiyo kauli inatafsiriwa vipi?
Mbona haina cha ajabu na cha kutisha bali inafundisha ujasiri wa kudai haki!
Mahakamini wataishia kuumbuka!
Lakini lengo inawezekana ni kumkomoa tu.
Hawana nia na kesi bali wana lengo la kutisha na kukatisha tamaa wapinzani!
Wanafungua kesi kutimiza mashariti ya kisheria tu!
Hapo mama lema kweli huna mume. Nakushauri usijiingize kwenye huo mchezo wa mumeo maana kule jela hakufai. Kuna wanaume wana miaka kibao hawajui wake.
Hamna kesi hapo!
Hiyo kauli inatafsiriwa vipi?
Mbona haina cha ajabu na cha kutisha bali inafundisha ujasiri wa kudai haki!
Mahakamini wataishia kuumbuka!
Lakini lengo inawezekana ni kumkomoa tu.
Hawana nia na kesi bali wana lengo la kutisha na kukatisha tamaa wapinzani!
Wanafungua kesi kutimiza mashariti ya kisheria tu!
Mimi niko hapa na ninaelewa bifu yake na Mulongo na ukitaka kujua amembambikizia kesi ili amwaibishe soma kesi inayompeleka mahakamani. Wewe elewa Mulongo alishangilia Lema alipovuliwa ubunge na ushahidi tunao. You're not informed tuulize sisi acha KUTUMIKAUmeambiwa kuwa kilichompeleka lema lumande ni maneno yake ya uchochezi. Hapo mulongo anainiaje?
Viongozi wa chadema asilimia 80 wanakunywa na kula bangi.
Akili zako zimetiwa maji na ndo maana unamtetea Mulongo ambaye alistahili kuwa rumande kwa kutangaza vita na mbunge wa arusha