Mbunge Kwagilwa: Tuwe na Tume ya Mipango ya Kudumu

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,903
945

MBUNGE KWAGILWA: TUWE NA TUME YA MIPANGO YA KUDUMU

Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini mkoani Tanga, Kwagilwa Ruben amesema, umefika wakati kwa Tanzania kuwa na Tume ya Kudumu ya Mipango ili kuwa na chombo cha kupanga maendeleo ya Taifa kwa kipindi kirefu tofauti na ilivyo sasa.

Akiwasilisha mada kuhusiana na Tume ya Mipango na namna bora ya kuwa na mipango ya kitaifa, Kwagilwa ambaye pia ni Mtaalam wa Mipango amesema, tume ya mipango imekuwa ikihama hama jambo ambalo halitoi nafasi kwa tume hiyo kupanga mipango ya kitaifa.

Kwagilwa amesema, kukiwa na Tume ya kudumu ya mipango kutarahisisha upangaji mipango ya maendeleo kwa kipindi kirefu na ufuatiliaji wake utakuwa rahisi kutokana na chombo hicho kuwa cha kudumu.

Kongamano la Wanamipango 2023 linafanyika kwa siku nne mkoani Arusha na linawakutanisha Wanamipango kutoka taasisi, idara, wizara na halmashauri zote hapa nchini.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-11-28 at 16.14.17.jpeg
    WhatsApp Image 2023-11-28 at 16.14.17.jpeg
    93.9 KB · Views: 1
  • WhatsApp Video 2023-11-28 at 00.24.43.mp4
    7.1 MB
Back
Top Bottom