Mbowe aungana na Mnyika kusema serikali ya Kikwete dhaifu

Katika mchango wake juu ya bajeti, Kiongozi wa kambi ya Upinzani Bungeni Mh. Freeman Mbowe ameonyesha ukomavu mkubwa wa kisiasa.

Mbowe amemsihi Spika ajitahidi kuwa fair, amelaani lugha za kejeli na matusi, ame advocate dhana ya wajibu wa kikatiba wa upinzani kukosoa bajeti pamoja na kulaani kitendo cha viongozi kupongeza kitendo kisicho cha kistaarabu cha kuchana bajeti mbadala, amelaani kitendo cha serikali kuona fahari kuongeza deni la taifa ambapo asilimia kubwa inaelekezwa katika administrative aspects, ameionya serikali juu ya swala la kujiingiza kwenye mikataba isiyokua na tija katika taifa letu na hivyo kufanya taifa letu kuwa soko la bidhaa (hadi pini na vifungo) mfano mkataba wa World Trade Organization (WTO) na haya yote ameyadadavua precisely kwa muda wa dakika kumi tu!

Nadhani wabunge wanapaswa kufwata ukomavu kama huu na siyo kuweka itikadi za vyama vyao mbele!
 
CDM ni wanafiki tunamwona Mdee asivyo na nidhamu kwa nini anatetea taarifa ambayo haikusahihishwa mezani kwanza, Zito kasema mapato ya TRA 0
Mbowe ashauri hata Bunge ni Legelege na livunjwe kura zirudiwe na nata Rais arudie hata km bbuu awamu ya 3
 
CDM ni wanafiki tunamwona Mdee asivyo na nidhamu kwa nini anatetea taarifa ambayo haikusahihishwa mezani kwanza, Zito kasema mapato ya TRA 0
Mbowe ashauri hata Bunge ni Legelege na livunjwe kura zirudiwe na nata Rais arudie hata km bbuu awamu ya 3

Mbona ilishasahihishwa? Hata Bungeni pia ilisahihishwa. Nahisi wewe hufatilii mambo. Lile kosa lilikuwa ni typing error, kuna jedwali halikuwekwa. Ila lilishafanyiwa usahihi. Hata Mh. Mdee ndiye aliyetolea taarifa hili
 
Hapo sawa lakini sio km wengine wanasimama bila ruhusa na kutoa kejeli litakuwa Bunge kweli
Kusema Ngeleja ana uchungu wa kukosa uwaziri au sura ka Sokwe au akili ya kukalia mata** au Silly season
 
CDM ni wanafiki tunamwona Mdee asivyo na nidhamu kwa nini anatetea taarifa ambayo haikusahihishwa mezani kwanza, Zito kasema mapato ya TRA 0
Mbowe ashauri hata Bunge ni Legelege na livunjwe kura zirudiwe na nata Rais arudie hata km bbuu awamu ya 3

CCM wana ugonjwa wa kutosoma na kutokuwa makini hata kusikiliza. Na ndio maana tuna mikataba mibovu kwa sababu watu hawasomi na wala hawasikilizi. Marekebisho ya speech ya Zitto yalitolewa siku mbili zilizopita, na hansard zinaonesha hivyo, lakini bado ccm wanauliza swali lile lile. No wonder nchi hii imekuwa shamba la bibi. Vichwa maji kabisa.
 
Naungana na wewe, kwa kweli Mh. Mbowe ameonyesha maturity ya hali ya juu leo Bungeni. Na ninaunga mkono kuwa anafaa sana kuwa kiongozi wa chama na kiongozi wa kambi ya Upinzani. Amesimama kitaifa zaidi kuliko ushabiki.
 
Katika mchango wake juu ya bajeti, Kiongozi wa kambi ya Upinzani Bungeni Mh. Freeman Mbowe ameonyesha ukomavu mkubwa wa kisiasa.

Mbowe amemsihi Spika ajitahidi kuwa fair, amelaani lugha za kejeli na matusi, ame advocate dhana ya wajibu wa kikatiba wa upinzani kukosoa bajeti pamoja na kulaani kitendo cha viongozi kupongeza kitendo kisicho cha kistaarabu cha kuchana bajeti mbadala, amelaani kitendo cha serikali kuona fahari kuongeza deni la taifa ambapo asilimia kubwa inaelekezwa katika administrative aspects, ameionya serikali juu ya swala la kujiingiza kwenye mikataba isiyokua na tija katika taifa letu na hivyo kufanya taifa letu kuwa soko la bidhaa (hadi pini na vifungo) mfano mkataba wa World Trade Organization (WTO) na haya yote ameyadadavua precisely kwa muda wa dakika kumi tu!

Nadhani wabunge wanapaswa kufwata ukomavu kama huu na siyo kuweka itikadi za vyama vyao mbele!

Mheshimiwa mbowe vema lakini mbona hakuna mbunge anaeomba kodi kupunguzwa katika mishahara ya wafanyakazi?
Pili, mbona kuna malalamiko ya wafanyakazi wa uDOM kuidai serikali pesa za promotions tangu 2010 na wameomba waziri kivuli ambae pia ni mwenyekiti wa mashirika ya umma awatembelee apate picha hiyo mbona haonekani?
Wamepigwa danadana muda mrefu sana kati yao na wizara za elimu, utumishi na fedha
 
chama cha chdm kimekua na maendeleo mazuri kisiasa ktk miaka 5 iliopita! ni jambo zuri linalo leta matumaini ya kuchukua dola! kufanya vizuri ni jambo moja na kutunza kiwango ni jambo lingine tofauti. kwa maoni yangu, chdm mnashindwa kutunza kiwango. mambo yafuatayo ni vielelzo tosha.


1- mh mbowe alikana gari la kiongozi wa upinzani hadharani. baada ya muda mfupi akalichukua kimyakimya!

2- wabunge wa chdm walikataa posho lkn wameendelea kuzichukua hadi hii leo!

3- wabunge wengi wa chdm wamehamia kwenye malumbano bungeni kuliko kujenga hoja. mtindo huu unongozwa na lissu, msigwa, lema (hayumo bungeni), wenje........ mnyika na zitto ni wajengaji wazuri wa wa hoja!


4- kibri alichokionesha mnyika kukataa kufuta kauli yke kuhusu rais kikwete siyo ueledi na busara. ni utovu wa nidhamu. ccm wamefanikiwa kuwatoa chdm kwenye kujenga hoja na kuwafanya waingie kwenye malumbano. chdm wakumbuke kuwa kabla ya mwaka 2010 walikua wachache sn bungeni lkn hoja nzuri zenye mantiki zilizojengwa na dk slaa, mdee na zitto, ziliijenga sn chdm. tafadhalini chdm jengeni hoja ili kurudisha heshima ya chdm bungeni


5- akina zitto, msigwa, lissu na wengineo walikimbilia majimboni kufanya mikutano ya hadhara kuambia wananchi kuwa bajeti ni mbovu wakaikatae! la haula!!!!!!!!!!!! nilivyoona mambo yamekua hayo, nikajiuliza: hivi chdm wanakwenda wapi? bajeti itasomwa bungeni ww ni mbunge unakimbilia kwa wananchi eti kukusanya maoni yao kuhusu bajeti! tunapoteza muelekeo sn! zitto siku moja kabla ya kusoma bajeti mbadala, alikua iringa kwa msigwa. hakupata hata muda wa kupitia bajeti yke kucheki erros! akawasilisha bajeti iliyo na makosa ya kiuchapaji. ccm wamebana hapohapo kuisulubu chdm na kweli hadi muda huu, chdm wameyumba sn bungeni! chama kinapelekwa wapi.



rudisheni chdm ile ya kabla ya mwaka 2010 iliosifika kwa kujenga hoja bungeni!!!:hand:!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Yan hilo liko wazi kabisa jk ni dhaifu sana.

Yan kama bunge leo limekili sasa mbona zomba ambaye ni kada tu anakataa.

Zomba kumbuka wabunge ni wengi sana mule,yan lukuvi,spika wametafakari wakaona ni kweli kabisa.

Ebu zomba twambie utawafanya nini wabunge wa nyinyiemu walio kubali leo jk ni dhaifu.

Na umepanga nini juu ya mtei,mbowe na spika?

Nime amini nawewe zomba ni dhaifu,yan huoni nape kakubaliana na kauli ya mnyika?
 
Back
Top Bottom