Mbona Rais hajapiga marufuku siasa? Au kuna jingine?

Tatizo vyama vya upinzani na wapinzani uwezo wa kufikiri umefika kikomo maana hawataki kuendana na mazingira tuliyo nayo kwa sasa.
Unawaona vijana wa swissm lakini ambao hawaja fika kikomo mwingine akililia sanamu ya diamond na kuvuliwa kibarakashee na mwingine akililia bunge live lisionyeshwe.
Kati ya hawa na vijana wa upinzani ni nani kafikia kikomo kufikiri na kuanza comedy kama si vioja tena sehemu inayoitwa Takatifu.
 
Upinzani unafanya siasa za kwenye utawala wa Kikwete kwenye utawala wa Magufuli.

Kikwete alikuwa Rais wa kupooza Mambo, Magufuli ni Rais wa kuangalia hoja.

Na ikitokea siku wapinzani wakialikwa Ikulu wawe Na hoja zenye mshiko kwa Taifa sio kukimbilia juisi..... la sivyo Magufuli atawapozea jumla.

Ukiona mtu anakimbilia mambo ya kula kama hoja ujue fikra zimefikia ukomo! With all due respect Mbowe ananjaa ya kwenda kunywa Juisi Ikulu? w...t...f
 
Yaani Raisi "awaombe" wanasiasa wasifanye siasa?, kweli siku hizi common sense is not common at all!

Inaelekea hata matatizo yako yana matatizo licha ya kutojua taratibu za siasa zikoje. Kuna siasa za kiushindani zile za kampeni, hakuna demokrasia yeyote duniani inayoruhusu kampeni kufanyika miaka mitano. Fuatilia siasa za maraekani, fuatilia kama atakayeshindwa atakuwa na mikutano ya siasa baada ya uchaguzi. Au hata sasa katika uchaguzi wa ndani wa vyama angalia kama walioshindwa wana mikutano na wanachama wao.Kuna siasa na uanaharakati, kama watu wanataka kuwa wanaharakati basi watumie civil societies kufanya hivyo kwani wanaruhusiwa kujiunga
 
Hapana wenye msimamo ni Wakwapuzi wa nyumba za Serikali, mafisadi wa EPA, Rada, IPTL, Escrow, Lugumi, Wakwapuzi wa UDA, Wakwapuzi wa Pride, wanunuzi wa MV Dar na mafisadi wa wizara ya ujenzi. Hawa ndiyo wenye msimamo.

Hivi nyinyi ndio wenye msimamo?
 
Tatizo vyama vya upinzani na wapinzani uwezo wa kufikiri umefika kikomo maana hawataki kuendana na mazingira tuliyo nayo kwa sasa.
Mazingira yaliyopo ya kuifuta demokrasia? Au mazingira yapi labda! Mna macho lakini hamuoni na mna masikio ila hamsikii. Kubalini tu kuwa mwanasiasa ili afanye Nazi take Hana budi kukutana na kukusanyika na watu wengine wenye itikadi au imani inayofanana na yake ili kuwekana sawa katika masuala ya uchumi, afya, maendeleo na AMANI kwa ujumla. Ukisema siasa marufuku in batili kwani hata yeye anafanya siasa muda wote. Ina maana na yeye aiache shughuli ya siasa akafundishe kwani huko darasani hakuna siasa. Bado nalia na washauri wake, wanampotosha mno. No kiongozi mzuri mwenye malengo na maono ila hao washauri wake ni shida tupu. Alhaji fulani uliyekaa hapo jirani usimpotoshe mkulu kwa tamaa zako za kubaki wazazi kampani iliyojifia natural death.
 
Tatizo vyama vya upinzani na wapinzani uwezo wa kufikiri umefika kikomo maana hawataki kuendana na mazingira tuliyo nayo kwa sasa.
Kwahiyo Katiba iendelee kukanyagwa au tuibadilishe? hebu siku moja moja uwe na Busara... au mpaka maaskofu waambie mtumie busara ndio mnawasikiliza?
 
Magufuli ni adui wa kwanza wa demokrasia Tanzania.

Usisikilize sana maneno yake, angalia matendo yake.

Kilio cha wanademokrasia wote sio cha bure!

Siasa ni elimu ya haki, ni elimu ya uraia na hakuna maisha bila siasa.

Mheshimiwa aondoe miguu yake juu ya demokrasia yetu!

Mkuuu nadhani umetoa maoni yako ambayo yapo nje ya mada
 
Maana yangu ilikuwa ikiwa kuna mapungufu kuanzia kamati ya maadili nadhani kanuni na taratibu za bunge zinaruhusu kukata rufaa maana hiyo kamati huwa na mamlaka sawa na mahakama.

Nakumbuka NS alianza mzozo na wabunge baada ya kukataa hoja ya Lema kujadiliwa bungeni kuhusu wanafunzi wa kozi maalum ya ualimu kuondolewa chuoni! UDOM... Sasa hapo wabunge bado nilidhani walitakiwa kwa ujumla wao na kwa kutumia busara wamweleze naibu Spika kwa kumtumia KUB (ndio kazi yake kama captain wa team) na kama NS asingewatendea haki angelipeleka kwenye kamati ya maadili (ndio mahakama ya bunge) au kwa Spika Ndungai ingawa nasikia anaumwa lakini bado kwa mamlaka yake angeweza kupendekeza Chenge au Zungu waisikilize hiyo hoja..

Hofu yangu huku nje ya Bunge kuna mihimili mingine ambayo haifuati kanuni za Bunge kwa wabunge, kitu ambacho nadhani upinzani wanaona polisi wanatumika kuwazuia. Na hapa nadhani JPM ndio alipopalenga (kwa kusema wabunge Wafanye siasa bungeni)

Kuna swala jingine ambalo tawala nyingi zililipuuzia lakini zilikwama, sasa wale wa mfumo au nadharia ya communist na socialist countries walipata dawa yake kwamba utawala wao ni kama dume kwenye zizi la ng'ombe likikubali vidume chipukizi vimchome pembe na dume la mbegu likakaa kando kwamba na wao ni madume mwisho wa siku yeye ndio atatimuliwa zizini anyway I don't want be ingratiating person to my political observations nasema tu nachokiona na kukitafakari.
Ila inahitaji akili ndogo tu kuelewa tofauti ya USA na Tanzania kuanzia mindset za viongozi/watawala mpaka mindset za wapigakura. Kwamba mwenendo wa mabunge ya USA na Bunge la Tulia tofauti yake ni kubwa mno...asante kwa kuja!
 
Hivi kuna kitu nimemiss.. maana nimesikia kuna watu wanalalamika Rais kapiga marufuku siasa. Nimetoka kuangalia hotuba yake lakini sijaona mahali alipopiga marufuku siasa. Inawezekana ametoa hotuba nzuri na ya kirafiki zaidi kwa wanasiasa. Au kuna agizo jingine limetolewa nje ya hii hotuba ya leo?

Nimeona tamko la chama cha ACT na limenifanya nikimbie haraka kusoma na kusikiliza hiyo hotuba kabla ya kutoa maoni yangu. Lakini sikusikia agizo au tamko lolote lile za kupiga marufuku siasa au kazi za siasa nchini. Nimeona Rais ametoa "ombi" ambalo ukijumlisha na aliyoyasema baadaye linaashiria tu kuwataka wanasiasa kufanya siasa nzuri zaidi bila kusababisha kukwamisha juhudi za maendeleo au kuonekekana wanaendekeza mno siasa kuliko kazi za kulijenga taifa.

Au baada ya hotuba yake Rais ametoa agizo jingine rasmi la kupiga marufuku kazi za siasa nchini? Au labda uzee ndio unazidi kasi nimeshindwa kuelewa.

Sehemu ya Hotuba:


Sikiliza hotuba hiyo kwa umakini halafu changanya na yale yanayowapata wapinzani ndio utamuelewa mjomba wangu. Lakini ni wazi wala hakuna la ajabu kwani ukiwa na mahaba hata "chongo utaita makengeza". JK alitufundisha eti "Za kuambiwa-changanya na zako".
 
Lakini sikusikia agizo au tamko lolote lile za kupiga marufuku siasa au kazi za siasa nchini. Nimeona Rais ametoa "ombi" ambalo ukijumlisha na aliyoyasema baadaye linaashiria tu kuwataka wanasiasa kufanya siasa nzuri zaidi bila kusababisha kukwamisha juhudi za maendeleo au kuonekekana wanaendekeza mno siasa kuliko kazi za kulijenga taifa.
Nina wasiwasi na uwezo wako wa kuchambua mambo! kama kweli umeisikiliza hiyo hotuba na hujahadithiwa na mtu.
Hivi unataka kutuambia kauli ya rais ni sawa na kauli ya m/kiti wa kitongoji?
Kwa taarifa yako kauli yoyote ya rais husimama kama agizo/ Sheria.
Usijitoe ufahamu huku ungali unatambua na unafahamu kamili labda kama umetumwa.
 
Maana yangu ilikuwa ikiwa kuna mapungufu kuanzia kamati ya maadili nadhani kanuni na taratibu za bunge zinaruhusu kukata rufaa maana hiyo kamati huwa na mamlaka sawa na mahakama.

Nakumbuka NS alianza mzozo na wabunge baada ya kukataa hoja ya Lema kujadiliwa bungeni kuhusu wanafunzi wa kozi maalum ya ualimu kuondolewa chuoni! UDOM... Sasa hapo wabunge bado nilidhani walitakiwa kwa ujumla wao na kwa kutumia busara wamweleze naibu Spika kwa kumtumia KUB (ndio kazi yake kama captain wa team) na kama NS asingewatendea haki angelipeleka kwenye kamati ya maadili (ndio mahakama ya bunge) au kwa Spika Ndungai ingawa nasikia anaumwa lakini bado kwa mamlaka yake angeweza kupendekeza Chenge au Zungu waisikilize hiyo hoja..

Hofu yangu huku nje ya Bunge kuna mihimili mingine ambayo haifuati kanuni za Bunge kwa wabunge, kitu ambacho nadhani upinzani wanaona polisi wanatumika kuwazuia. Na hapa nadhani JPM ndio alipopalenga (kwa kusema wabunge Wafanye siasa bungeni)

Kuna swala jingine ambalo tawala nyingi zililipuuzia lakini zilikwama, sasa wale wa mfumo au nadharia ya communist na socialist countries walipata dawa yake kwamba utawala wao ni kama dume kwenye zizi la ng'ombe likikubali vidume chipukizi vimchome pembe na dume la mbegu likakaa kando kwamba na wao ni madume mwisho wa siku yeye ndio atatimuliwa zizini anyway I don't want be ingratiating person to my political observations nasema tu nachokiona na kukitafakari.
Mkuu Akazuba naielewa sana hoja yako from the beggining, tatizo ninaloliona kwako (samahani lakini) hata kwa post hii bado unajadili kwa kuliona bunge letu kama chombo kinachofanya kazi zake sawa sawa na mabunge kama ya Marekani au tuseme nchi nyingine zilizoendelea. Unasahau kwamba bunge letu linatumika kisiasa zaidi ili kulinda maslahi ya watawala badala ya kuwa chombo cha kuisimamia serikali. Sasa ni rahisi tu kuelewa kwamba mkuu wa nchi anaposema wabunge wafanye siasa bungeni anajua tayari bungeni wameweka "miundombinu" inayowadhibiti wapinzani!
 
Nimekuelewa kwenye miundo mbinu... so how opposition can reach the beginning by boycotting NS's chair? Consider to get the end go to the beginning theory. Au ndio maana wanamshambulia JPM?
Mkuu Akazuba naielewa sana hoja yako from the beggining, tatizo ninaloliona kwako (samahani lakini) hata kwa post hii bado unajadili kwa kuliona bunge letu kama chombo kinachofanya kazi zake sawa sawa na mabunge kama ya Marekani au tuseme nchi nyingine zilizoendelea. Unasahau kwamba bunge letu linatumika kisiasa zaidi ili kulinda maslahi ya watawala badala ya kuwa chombo cha kuisimamia serikali. Sasa ni rahisi tu kuelewa kwamba mkuu wa nchi anaposema wabunge wafanye siasa bungeni anajua tayari bungeni wameweka "miundombinu" inayowadhibiti wapinzani!
 
Magufuli ni adui wa kwanza wa demokrasia Tanzania.

Usisikilize sana maneno yake, angalia matendo yake.

Kilio cha wanademokrasia wote sio cha bure!

Siasa ni elimu ya haki, ni elimu ya uraia na hakuna maisha bila siasa.

Mheshimiwa aondoe miguu yake juu ya demokrasia yetu!
hiv nan muumin wa democrasia kati ya rais na wenyeviti wa hvyo vyama? mtazame mbowe, yy ni mwenyekiti sijui wa kudum? angalia anachofanya yaan anawabuluza tu wenzake, halafu anasema anaomba democrasia, m nadhan kabla ya kuomba hyo democrasia kama wanaona Rais anakiuka, waanze kwanza wao...
 
Hata kama ukuu wa mkoa lakn hautafutwi hvyo. Wote hatujamwelewa ila ww tu!! Police wanaozuia mkutano hujawaona au umevaa akili za kushikiwa?? Duu masn ukiwa ccm ghafa akili hupotea
 
Nimekuelewa kwenye miundo mbinu... so how opposition can reach the beginning by boycotting NS's chair? Consider to get the end go to the beginning theory. Au ndio maana wanamshambulia JPM?
Sina uhakika kama wanamshambulia JPM au wanasimama kutekeleza majukumu yao kama wapinzani. Hii inaweza kuwa fursa ya watu wanaofikiri kwa kujisimamia wenyewe kutoa tafsiri ya kinachofanywa na opposition. Lakini, tatizo ninaloliiona liko zaidi kwa wananchi kudhani kwamba ni wabunge wa opposition peke yao ndio wanaweza kurejesha heshima ya bunge kuwa chombo cha kuisimamia serikali.

Mkuu Akazuba, mimi mtazamo wangu ni kwamba this time bunge limetuangusha sana na limekuwa sababu ya yote yanayoendelea sasa. Nafahamu watu wengi, na nitasikitika kama na wewe utakuwa miongoni mwao, wanaunga mkono udhibiti wa wabunge wa upinzani bungeni unaofanywa kwa kivuli cha kusimamia kanuni as if ni kanuni peke yake ndizo zinaendesha bunge. Nanmna hii ya uongozi wa bunge imetengeneza ufa mkubwa ndani ya bunge na ufa huo taratibu umeanza kuhamia nje ya bunge. Hili si jambo jema hata kidogo!

Hoja yangu hapa ni kwamba, wananchi wanapaswa kutambua kwamba bunge kuhodhiwa na serikali kama inavyoonekana kufanyika sasa, athari yake inaenda kwao moja kwa moja. Kwamba si jambo la afya kwa wananchi kubeza harakati za wabunge wa upinzani kudai bunge huru na lenye uwezo wa kuisimamia serikali. Kuna watu wanazungumza kuwa haiwezekani kuwa na bunge huru linaloweza kuisimamia serikali iwapo ndani ya bunge majority ni wabunge wa CCM. Ingawa hilo lina ukweli sehemu fulani, lakini bado mimi ninaona tunaweza kuwa na bunge imara kama tuna spika/naibu spika anayeweka mbele maslahi ya taifa na sio maslahi ya chama. Ukweli huu ulithibitika wakati wa Sitta, na tuliona pia kwa Makinda japo alilazimishwa na nguvu kubwa iliyotumika kumweka namna hiyo!

Sasa kuna swali kama approach ya wabunge wa UKAWA ikiwemo kususia vikao vinavyoongozwa na NS ni sahihi au la. Tunaweza kuwa na mjadala hapa, lakini hata kabla ya kuwa na mjadala wenyewe tunaweza tu kuangalia pande zote; upinzani,chama tawala/serikali na wanannchi wanauchukuliaje mvutano huo.

Kwa mabunge yanayofikiria sawa sawa(kama ulivyotolea mfano mwanzo) mvutano uliopo lisingekuwa suala dogo, lakini unaona hapa kwetu badala ya kulimaliza kwa kutumia hekima na busara kiti kila siku kinafanya vitendo vinavyokuza mvutano huo. Kama naibu spika, kwa mtazamo wangu, asingekuwa na jambo kifuani mwake asingekuwa na "furaha" kuendesha bunge likiwa namna ile. Tena, kwangu mimi, kwa kuwa ni kweli kwamba hata miongoni mwa wabunge wa CCM NS hakubaliki angeweza kuachia nafasi hiyo kuliko kung'ang'ania kiti kuongoza chombo nyeti kwa mustakabali wa nchi kikiwa katika hali ile.

Nafahamu jambo hili linaweza kuwa lisilokubalika kwa wengine, lakini binafsi siioni Tanzania yenye asali na maziwa kama tutaenda na bunge la namna hii hadi kufikia 2020. kauli zinazotolewa kujibu zile zinazotaka mwafaka haziashirii mwisho mzuri katika jambo hili. Time will tell.

Mimi ninafikiri kinachoendelea bungeni, kwa kuwa mwisho wa siku athari zinatugusa sisi wananchi, ni vyema tukaanza kufikiri tofauti-tuwaongezee nguvu wabunge kwa kuchagua wabunge kwa namna ya "kubalance" idadi yao kwa maana ambayo haiufanyi upande mmoja kuwa na nguvu kubwa ya kuamua mambo yanayotuhusu wote hata ambao hatuna mapenzi au ushabiki wa vyama. Na mbaya zaidi mambo mengine yanayopitishwa hayatoi mwelekeo mwema katika maisha yetu!
 
Chadema ni bora mngejikita kuhoji ni kwa nini Mbowe aliuza chama chenu???

Naamini bila mbowe kuuza chama msingekengeuka kiasi hiki.

Leo mnapinga kila kitu na kujidai mnadai democrasia wakati ndani ya chadema hamna hata tone la democrasia.

Hebu jiulize wakati Mbowe anabadili gia angani alishilikisha wanachama wa ngapi??
 
Tatizo vyama vya upinzani na wapinzani uwezo wa kufikiri umefika kikomo maana hawataki kuendana na mazingira tuliyo nayo kwa sasa.

Kama uwezo wa wapinzani umefikia kikomo mbona wanaemdelea kudhibitiwa? Tena kwa kuitumia vyombo vya dola na siyo katiba
 
Ma
Hivi kuna kitu nimemiss.. maana nimesikia kuna watu wanalalamika Rais kapiga marufuku siasa. Nimetoka kuangalia hotuba yake lakini sijaona mahali alipopiga marufuku siasa. Inawezekana ametoa hotuba nzuri na ya kirafiki zaidi kwa wanasiasa. Au kuna agizo jingine limetolewa nje ya hii hotuba ya leo?

Nimeona tamko la chama cha ACT na limenifanya nikimbie haraka kusoma na kusikiliza hiyo hotuba kabla ya kutoa maoni yangu. Lakini sikusikia agizo au tamko lolote lile za kupiga marufuku siasa au kazi za siasa nchini. Nimeona Rais ametoa "ombi" ambalo ukijumlisha na aliyoyasema baadaye linaashiria tu kuwataka wanasiasa kufanya siasa nzuri zaidi bila kusababisha kukwamisha juhudi za maendeleo au kuonekekana wanaendekeza mno siasa kuliko kazi za kulijenga taifa.

Au baada ya hotuba yake Rais ametoa agizo jingine rasmi la kupiga marufuku kazi za siasa nchini? Au labda uzee ndio unazidi kasi nimeshindwa kuelewa.

Sehemu ya Hotuba:


Maneno yake hanaakisiwa na kinachoendilea mitaani. Polisi wanazuia mikutano ya kisiasa, manavyuo waupinzani wanazuiwa kuuagana nk
 
Back
Top Bottom