kapuyanga mkware
JF-Expert Member
- Nov 16, 2013
- 589
- 143
Ndugu wana JF. Wanadamu tumezungukwa na mahitaji mbalimbali. Wakati mwingine tunafanikiwa kupata tunachohitaji na wakati mwingine hatufanikiwi. Mbinu mojawapo ya kufanikiwa kupata kitu unachohitaji kutoka kwa mtu ni kumtega kimazungumzo. Kwa mfano unahitaji mtu akuazime gari yake. Endapo utamwambia moja kwa moja akuazime anaweza kukwambia gari hiyo sio mali yake. Hivyo unaweza kumtega kwa kumuuliza "...gari yako umenunua kiasi gani?" Bila shaka atakujibu "...shs milioni kadhaa" Kwa jibu hili atakuwa amejifunga kimazungumzo bila ya kujua lengo lako. Hivyo itakuwa rahisi kwako kufanikiwa kulipata endapo utamwomba akuazime ili ulitumie kwa siku hiyo. Jaribu kutumia MBINU hii uone jinsi utakavyofanikiwa.
VIMADA. ??? wewe ni kimada wa nani