Seif Mselem
JF-Expert Member
- Oct 16, 2023
- 257
- 441
Miaka ya 90’s nchini nigeria…
Kampuni moja la kutengeneza vyakula linalojulikana kama “Wonder Foods Nigeria Limited”
Lilitangaza kuzindua na kuingiza sokoni bidhaa yake moja ya maziwa iliyokuwa inaitwa “cow-bell milk”
Lakini wakati wanazindua bidhaa hiyo sokoni walikuwa wanaingia kwenye soko lenye ushindani mkali sana wa maziwa lililokuwa linatawaliwa na wauzaji wengine wakubwa kwa kipindi hicho na kama hufahamu tu…
Nigeria ni moja ya taifa linaloongoza kwa kuzalisha maziwa ya kusindika yaani… processed milk! Na… kwa kipindi hicho tayari kulikuwa na brand kubwa za maziwa sokoni…
Kulikuwa na…
- peak milk
- coast milk
- dano milk
- nido...
- three crowns milk
Yote haya tayari yalikuwa yameshika nafasi zake sokoni kwa muda mrefu…
Yaani… kwa wale wanangu wa mujibu wa sheria tunasema kila mmoja hapo juu alikuwa kishajikatia “kibangala” chake!
Kwahiyo… cowbell walikuwa na kazi kubwa ya kufanya na kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa historia basi utakuwa unakumbuka kwamba…
Miaka ya 90’s taifa la nigeria lilikuwa chini ya utawala wa kijeshi wa general “ibrahim babangida”
Kwahiyo, sio tu cowbells walikuwa wanaingia kwenye soko lenye ushindani mkali bali walikuwa wanaingia kipindi ambacho hali ya uchumi ya wanigeria wengi ilikuwa iko chini sana na mbaya zaidi maziwa yalichukuliwa kama ni bidhaa ya…“kishua”
Kwasababu…kwa kipindi kile familia nyingi zilikuwa hazina uwezo wa kununua makopo makubwa ya maziwa ya unga kama ya…nido!
So unaweza uka imagine ni kwa kiasi gani ilikuwa ni ngumu kutoboa kwenye soko kama hilo…
Mfano mzuri ni…kama vile mtu uiingie kwenye soko la ngano kwa hapa bongo…
Hahaa… nadhani unaelewa nini kitatokea!
Basi bhana Cowbells na wao walianza kwa kuuza kama walivyokuwa wakiuza washindani zao wengine sokoni…
Yaani… waliuza katika ujazo ule ule na ukubwa wa kufanana… tofauti ilikuwa ni rangi ya vifungashio tu…
Kwa ufupi wali… copy na ku paste walichokuwa wanafanya…
Nido, dano na coast milk!
Unajua nini kilitokea?..
Yeah… uko sahihi!
Walipata hasara kubwa mno…hadi ikawabidi wabadili mfumo mziwa wa uuzaji wao…
Wakaamua kuja kivingine tena waliamua kuanza kuuza maziwa yao kwenye mifuko mikubwa ya kilo 25 na 50 kama inavyokuwa mifuko ya simenti…
Na… walikuwa wanawauzia watu wenye maduka ya jumla na wao walikuwa wanauza kwa wa nigeria wa chini kwa kupima kwenye kilo na kufunga kwenye pakti zingine ndogo ndogo yaani walikuwa wanauza kama vile sukari na ngano zinavyouzwa kwa hapa bongo!
Hii mbinu iliwapa matumaini kidogo kwasababu… walikuwa wanafanya kitu ambacho wauzaji wengine wa maziwa walikuwa hawakifanyi sokoni
Hata hivyo bado waliendelea kupata hasara sokoni…
Cowbells na management timu yake yote wakaamua kurudi kwenye… drawing board na kuja na mbinu mpya kabisa ya kuuza maziwa ya unga…
Kumbuka…
Walikuwa wako kwenye soko lenye uchumi mbaya na ushindani mkali + walikuwa wanataka maziwa yao yamfikie hadi mnigeria wa daraja la chini kabisa…
Kwahiyo…haikuwa kazi rahisi kwa timu nzima ya cowbells kufanikiwa…
Na hapo ndipo walipoamua kuja na mbinu ingine mpya kabisa ya kuuza…
Walikuja na kufanya kitu kinaitwa…
“sachetization process”
Usihangaike kuelewa…nimekuwekea maelezo yake hapa chini
Yaani… walianza kwa kuyafunga maziwa yao kwenye vimifuko na vipakti vidogo vodogo vye uzito wa kama vile gramu 20 hivi…
Vipakti ambavyo hata mnaigeria wa chini kabisa angeweza kuvinunua na kuvitumia…
Kwahiyo… ujio wa hivo vimifuko vidogo ilikuwa ni fursa kwa kila mtu kutumia maziwa…
Kwasababu… vilikuwa vinapikana kwa bei rahisi na kila kona ya mtaa vilikuwa vinauzwa…
Kuanzia kwenye… vioski na maduka yote madogo na ilikuwa kila mtaa ukipita lazima ukutane na vi pakti vya blue vyenye nembo ya cowbell kwa juu…
Redio na tv zote zilikuwa zikitangaza cowbells… ingekuwa ni bet basi walikuwa wamepiga jackpot…
They were… everywhere! Na kuanzia hapo kilichobaki ni historia tu kwasababu… naamini hata wewe itakuwa ushatumia maziwa ya cowbells ya kwenye pakti kipindi cha utoto wako…
Maana hata mimi nakumbuka nilikuwa nayanunua kwa mangi kwa tshs 50 au 100 kama sijasahau…
Na kuanzia hapo ma kampuni mengine ya maziwa kama peak, coast, dano n.K yalianza kutumia hii mbinu ya… “sachetization”
Na kitu cha kushangaza ni kwamba…
Vipakti vidogo vina gharama zaidi kuliko zile pakti kubwa za mwanzo kwasababu…
Kama ukitaka kujaza pakti kwa kutumia vipakti vidogo basi utatumia pesa nyingi ukilinganisha na ungenunua pakti kubwa moja…
Ila kwasababu vilikuwa ni bei kitonga basi watu hawakujali!
Na hii mbinu haikuishia kutumika kwenye maziwa tu…inatumika hadi leo kwenye…
Kuuza bidhaa kama dawa za meno na hadi kwenye huduma za benki inatumika…
Ila hiyo itakuwa makala ya siku ingine...Kwahiyo kwa leo tuishie hapa I hope umejifunza kitu…
Uwe na siku njema.
Gracias…
Seif Mselem
Kampuni moja la kutengeneza vyakula linalojulikana kama “Wonder Foods Nigeria Limited”
Lilitangaza kuzindua na kuingiza sokoni bidhaa yake moja ya maziwa iliyokuwa inaitwa “cow-bell milk”
Lakini wakati wanazindua bidhaa hiyo sokoni walikuwa wanaingia kwenye soko lenye ushindani mkali sana wa maziwa lililokuwa linatawaliwa na wauzaji wengine wakubwa kwa kipindi hicho na kama hufahamu tu…
Nigeria ni moja ya taifa linaloongoza kwa kuzalisha maziwa ya kusindika yaani… processed milk! Na… kwa kipindi hicho tayari kulikuwa na brand kubwa za maziwa sokoni…
Kulikuwa na…
- peak milk
- coast milk
- dano milk
- nido...
- three crowns milk
Yote haya tayari yalikuwa yameshika nafasi zake sokoni kwa muda mrefu…
Yaani… kwa wale wanangu wa mujibu wa sheria tunasema kila mmoja hapo juu alikuwa kishajikatia “kibangala” chake!
Kwahiyo… cowbell walikuwa na kazi kubwa ya kufanya na kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa historia basi utakuwa unakumbuka kwamba…
Miaka ya 90’s taifa la nigeria lilikuwa chini ya utawala wa kijeshi wa general “ibrahim babangida”
Kwahiyo, sio tu cowbells walikuwa wanaingia kwenye soko lenye ushindani mkali bali walikuwa wanaingia kipindi ambacho hali ya uchumi ya wanigeria wengi ilikuwa iko chini sana na mbaya zaidi maziwa yalichukuliwa kama ni bidhaa ya…“kishua”
Kwasababu…kwa kipindi kile familia nyingi zilikuwa hazina uwezo wa kununua makopo makubwa ya maziwa ya unga kama ya…nido!
So unaweza uka imagine ni kwa kiasi gani ilikuwa ni ngumu kutoboa kwenye soko kama hilo…
Mfano mzuri ni…kama vile mtu uiingie kwenye soko la ngano kwa hapa bongo…
Hahaa… nadhani unaelewa nini kitatokea!
Basi bhana Cowbells na wao walianza kwa kuuza kama walivyokuwa wakiuza washindani zao wengine sokoni…
Yaani… waliuza katika ujazo ule ule na ukubwa wa kufanana… tofauti ilikuwa ni rangi ya vifungashio tu…
Kwa ufupi wali… copy na ku paste walichokuwa wanafanya…
Nido, dano na coast milk!
Unajua nini kilitokea?..
Yeah… uko sahihi!
Walipata hasara kubwa mno…hadi ikawabidi wabadili mfumo mziwa wa uuzaji wao…
Wakaamua kuja kivingine tena waliamua kuanza kuuza maziwa yao kwenye mifuko mikubwa ya kilo 25 na 50 kama inavyokuwa mifuko ya simenti…
Na… walikuwa wanawauzia watu wenye maduka ya jumla na wao walikuwa wanauza kwa wa nigeria wa chini kwa kupima kwenye kilo na kufunga kwenye pakti zingine ndogo ndogo yaani walikuwa wanauza kama vile sukari na ngano zinavyouzwa kwa hapa bongo!
Hii mbinu iliwapa matumaini kidogo kwasababu… walikuwa wanafanya kitu ambacho wauzaji wengine wa maziwa walikuwa hawakifanyi sokoni
Hata hivyo bado waliendelea kupata hasara sokoni…
Cowbells na management timu yake yote wakaamua kurudi kwenye… drawing board na kuja na mbinu mpya kabisa ya kuuza maziwa ya unga…
Kumbuka…
Walikuwa wako kwenye soko lenye uchumi mbaya na ushindani mkali + walikuwa wanataka maziwa yao yamfikie hadi mnigeria wa daraja la chini kabisa…
Kwahiyo…haikuwa kazi rahisi kwa timu nzima ya cowbells kufanikiwa…
Na hapo ndipo walipoamua kuja na mbinu ingine mpya kabisa ya kuuza…
Walikuja na kufanya kitu kinaitwa…
“sachetization process”
Usihangaike kuelewa…nimekuwekea maelezo yake hapa chini
Yaani… walianza kwa kuyafunga maziwa yao kwenye vimifuko na vipakti vidogo vodogo vye uzito wa kama vile gramu 20 hivi…
Vipakti ambavyo hata mnaigeria wa chini kabisa angeweza kuvinunua na kuvitumia…
Kwahiyo… ujio wa hivo vimifuko vidogo ilikuwa ni fursa kwa kila mtu kutumia maziwa…
Kwasababu… vilikuwa vinapikana kwa bei rahisi na kila kona ya mtaa vilikuwa vinauzwa…
Kuanzia kwenye… vioski na maduka yote madogo na ilikuwa kila mtaa ukipita lazima ukutane na vi pakti vya blue vyenye nembo ya cowbell kwa juu…
Redio na tv zote zilikuwa zikitangaza cowbells… ingekuwa ni bet basi walikuwa wamepiga jackpot…
They were… everywhere! Na kuanzia hapo kilichobaki ni historia tu kwasababu… naamini hata wewe itakuwa ushatumia maziwa ya cowbells ya kwenye pakti kipindi cha utoto wako…
Maana hata mimi nakumbuka nilikuwa nayanunua kwa mangi kwa tshs 50 au 100 kama sijasahau…
Na kuanzia hapo ma kampuni mengine ya maziwa kama peak, coast, dano n.K yalianza kutumia hii mbinu ya… “sachetization”
Na kitu cha kushangaza ni kwamba…
Vipakti vidogo vina gharama zaidi kuliko zile pakti kubwa za mwanzo kwasababu…
Kama ukitaka kujaza pakti kwa kutumia vipakti vidogo basi utatumia pesa nyingi ukilinganisha na ungenunua pakti kubwa moja…
Ila kwasababu vilikuwa ni bei kitonga basi watu hawakujali!
Na hii mbinu haikuishia kutumika kwenye maziwa tu…inatumika hadi leo kwenye…
Kuuza bidhaa kama dawa za meno na hadi kwenye huduma za benki inatumika…
Ila hiyo itakuwa makala ya siku ingine...Kwahiyo kwa leo tuishie hapa I hope umejifunza kitu…
Uwe na siku njema.
Gracias…
Seif Mselem