Mbonea
JF-Expert Member
- Jul 14, 2009
- 640
- 20
Serikali ya Saudi Arabia imemchinja kwa kutumia jambia mwanaume raia wa Yemen ambaye alihukumiwa adhabu ya kifo baada ya kupatikana na hatia ya kuwabaka wanawake wawili.
Mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la Suleiman bin Ali alichinjwa kwa jambia jana jumapili kufuatia hukumu iliyotolewa na mahakama ya Jeddah iliyoamuru auliwe.
Suleiman alipatikana na hatia ya kumpiga na kumbaka mke wa raia mmoja wa Saudia, ilisema taarifa ya wizara ya mambo ya ndani ya Saudia.
Suleiman ambaye alitajwa kama mbakaji aliyekuwa akitafutwa kwa makosa menhi ya ubakaji, pia anatuhumiwa kumshambulia na kumbaka mwanamke mwingine wa nchini humo.
Kuuliwa kwa Suleiman kumefanya jumla ya wahalifu waliouliwa nchini Saudi Arabia kuanzia mwezi januari mwaka huu kufikia 67.
Mwaka jana watu 102 wwaliuliwa baada ya mahakama kuwahukumu adhabu ya kifo. Mwaka 2007 jumla ya watu waliohukumiwa adhabu ya kifo ilikuwa 153.
Kwa mujibu wa sharia za kiislamu zinazotumika nchini Saudi Arabia, wabakaji, wauaji, majambazi na wauzaji au wasafirishaji wa madawa ya kulevya huhukumiwa adhabu ya kifo.
Source: http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3817442&&Cat=2
Mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la Suleiman bin Ali alichinjwa kwa jambia jana jumapili kufuatia hukumu iliyotolewa na mahakama ya Jeddah iliyoamuru auliwe.
Suleiman alipatikana na hatia ya kumpiga na kumbaka mke wa raia mmoja wa Saudia, ilisema taarifa ya wizara ya mambo ya ndani ya Saudia.
Suleiman ambaye alitajwa kama mbakaji aliyekuwa akitafutwa kwa makosa menhi ya ubakaji, pia anatuhumiwa kumshambulia na kumbaka mwanamke mwingine wa nchini humo.
Kuuliwa kwa Suleiman kumefanya jumla ya wahalifu waliouliwa nchini Saudi Arabia kuanzia mwezi januari mwaka huu kufikia 67.
Mwaka jana watu 102 wwaliuliwa baada ya mahakama kuwahukumu adhabu ya kifo. Mwaka 2007 jumla ya watu waliohukumiwa adhabu ya kifo ilikuwa 153.
Kwa mujibu wa sharia za kiislamu zinazotumika nchini Saudi Arabia, wabakaji, wauaji, majambazi na wauzaji au wasafirishaji wa madawa ya kulevya huhukumiwa adhabu ya kifo.
Source: http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3817442&&Cat=2