Ronal Reagan
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 5,299
- 3,055
Kesho Jumamosi tarehe 10 Iyyar 5771, yaani tarehe 14 Mei 2011, Israe inaadhimisha miaka 63 ya kuzaliwa kwake. Mnamo tarehe14 May 1948 (5 Iyyar 5708), Waziri Mkuu wa Israel David Ben Gurion alisoma Tangazo la Uhuru wa Israel lijulikanalo Israeli Declaration of Independence (Kiyahudi huitwa, Hakhrazat HaAtzma'ut). Ben Gurion alitangaza rasmi kuzaliwa kwa taifa la Israel, ikiwa ni miaka mitatu tu tangu kumalizika kwa vita kuu ya pili ya dunia mwaka 1945.
Israel ni nini na nani hasa? Israel ni nchi, na Israel ni watu. Lugha yao ni Kiyahudi (lugha ya zamani huitwa Kiebrania). Neno au jina Yahudi latokana na neon Yudah au Yehudah, ambalo ni moja ya makabili halisi 12 ya watoto wa Yakobo au Israel. Yuda ni kabila ambalo baadaye, mwanzoni mwa utawala wa mfalme Rehoboam (mtoto wa mfalme Suleman), nchi ya Israel ilipogawanyika sehemu mbili, ilikuja kuwa dola. Kaskazini waliitwa Israel (ndiko walikokaa kabila kumi) na kusini waliitwa Yuda (ndiko kabila 2 za Yuda na Benyamini walikaa). Makao makuu ya Kaskazini yalikuwa mji wa Samaria, makao makuu ya kusini yalikuwa Yerusalem. Waliendelea hivyo (kuwa falme mbili) kwa karne nyingi. Pia neno/jina Yahudi ni utambulisho wa dini yao rasmi.
Duniani humu ni nchi au jamii chache sana zenye historia iliyo hai ya kuishi mfululizo (yaani bila kuangamia au kupotea) na kuwa na utambulisho wao. Tena katika historia, hakuna nchi (watu) iliyowahi kuchukuliwa nje ya mipaka yao na kubaki na utambulisho wao na kisha baadaye kurudi katika nchi yao ya asili na kuweka tena mizizi na kuchipuka. Israel walichukuliwa utumwani Ashuru (Syria zamani), walichukuliwa utumwani Babeli (Iran/Iraq) na baadaye kwa takriban miaka 1,900 walitawanywa kila pembe ya dunia tangua mwaka 70 A.D. (kufuatia Warumi kubomoa hekalu lao) hadi 1948.
Hivyo napenda kugusia kwa uchache sana jambo moja tu wakati huu wa kusherehekea miaka 63 ya kuzaliwa Taifa la Israel. Umuhimu wa Yerusalem kwa Israel. Ijulikane hapa kuwa MUNGU alipoichagua Israel kuwa nchi yake kadhalika aliichagua Yerusalem kuwa mji wake na makao yake. Hakuna nchi makini isiyo na mji mkuu (kitovu cha nchi). Israel na Yerusalem ni kitu kimoja, havitenganishiki wala kugawanyika. Yerusalem ni mji mkuu wa Israel milele. Amen.
Israel ina historia ya ajabu, ya kushangaza, kusikitisha, ya kusisimua na ya kipekee. Nawiwa kuwake dondoo zifuatazo:-
i) Ndio nchi au watu (kama jamii) ambao MUNGU aliwachagua na kujitambulisha kwao na kufanya nao maagano. Kwamba Yeye ni MUNGU wao, na wao ni watu wake na amewapa eneo husika la ardhi kuwa milki yao.
ii) Katika vita kuu ya Pili ya dunia, takwimu zinaonyesha Wayahudi milioni sita waliauwa. Tukio hilo lilikuwa ni moja ya chachu ya kuharakisha mchakato wa uundwaji taifa la Israel, ili Wayahudi wasiendelee kuuawa, kuwa wakimbizi wasio na matumaini ya kuiona nchi ya babu na baba zao.
iii) Israel ni nchi ya kidemokrasia, na Serikali yake huongozwa na Waziri Mkuu anayetokana na chama kilichoshinda uchaguzi. Benyamini Netanyahu ni WM wa 32 wa Israel. Bunge la Israel linaitwa Knesset. Pia Israel ina rais ambaye ni kiungo kati jamii na serikali yao. Inaundwa na majimbo nane kisha mikoa, wilaya na vijiji. Tofauti na jirani zake, Israel haina hazina ya mafuta, gesi au madini.
iv) Israel imestawi sana katikati ya uadui mwingi na vita toka kwa majirani zake na hata mbali ya mipaka yao. Ndio dola la kidemokrasia ya kweli Mashariki ya Kati (MK). Ndio dola lenye uchumi imara zaidi MK, Ndio dola lililoendelea zaidi kisayansi, kielimu, kiviwanda na kilimo MK. Ndio dola lenye nguvu kijeshi MK.
v) Kuelekea Vita ya Siku Sita – 1967 nchi za Kiarabu chini ya Abdel Nasser wwa Misri zilitaka kufunga ukurasa wa "historia" na "aibu" ya kushindwa vita ya 1948, zilizopelekea kuzaliwa taifa la Israel.
vi) Vita ya Siku Sita – 1967, Kiyahudi "Mil'hement sheshet Hayamim", ilianza tar 5 Juni 1967 na kumalizika tar 10 Juni 1967. Tukio moja kubwa katika vita hiyo ni Israel kuukomboa mji wa Yerusalem na kuurudisha katika milki yake.
vii) Uhalali, msingi na utashi wa kuwepo kwa Israel na watu wake hautegemei maazimio ya UN, au America au maoni ya mataifa. Uhalali na msingi wake ni maagano MUNGU wao aliyofanya nao. Ndio maana kila tunaposherehekea kuazaliwa kwa Israel pia huadhimisha uwezo wa neno "Waache watu wangu waende", ambalo Musa alimwambia Farao wa Misri.
Tukitaka kujifunza tuna mengi tunaweza kujfunza kwa Israel kama watu na kama nchi.
MUNGU IBARIKI ISRAEL! MUNGU WALINDE WATU WAKO ISRAEL!
Israel ni nini na nani hasa? Israel ni nchi, na Israel ni watu. Lugha yao ni Kiyahudi (lugha ya zamani huitwa Kiebrania). Neno au jina Yahudi latokana na neon Yudah au Yehudah, ambalo ni moja ya makabili halisi 12 ya watoto wa Yakobo au Israel. Yuda ni kabila ambalo baadaye, mwanzoni mwa utawala wa mfalme Rehoboam (mtoto wa mfalme Suleman), nchi ya Israel ilipogawanyika sehemu mbili, ilikuja kuwa dola. Kaskazini waliitwa Israel (ndiko walikokaa kabila kumi) na kusini waliitwa Yuda (ndiko kabila 2 za Yuda na Benyamini walikaa). Makao makuu ya Kaskazini yalikuwa mji wa Samaria, makao makuu ya kusini yalikuwa Yerusalem. Waliendelea hivyo (kuwa falme mbili) kwa karne nyingi. Pia neno/jina Yahudi ni utambulisho wa dini yao rasmi.
Duniani humu ni nchi au jamii chache sana zenye historia iliyo hai ya kuishi mfululizo (yaani bila kuangamia au kupotea) na kuwa na utambulisho wao. Tena katika historia, hakuna nchi (watu) iliyowahi kuchukuliwa nje ya mipaka yao na kubaki na utambulisho wao na kisha baadaye kurudi katika nchi yao ya asili na kuweka tena mizizi na kuchipuka. Israel walichukuliwa utumwani Ashuru (Syria zamani), walichukuliwa utumwani Babeli (Iran/Iraq) na baadaye kwa takriban miaka 1,900 walitawanywa kila pembe ya dunia tangua mwaka 70 A.D. (kufuatia Warumi kubomoa hekalu lao) hadi 1948.
Hivyo napenda kugusia kwa uchache sana jambo moja tu wakati huu wa kusherehekea miaka 63 ya kuzaliwa Taifa la Israel. Umuhimu wa Yerusalem kwa Israel. Ijulikane hapa kuwa MUNGU alipoichagua Israel kuwa nchi yake kadhalika aliichagua Yerusalem kuwa mji wake na makao yake. Hakuna nchi makini isiyo na mji mkuu (kitovu cha nchi). Israel na Yerusalem ni kitu kimoja, havitenganishiki wala kugawanyika. Yerusalem ni mji mkuu wa Israel milele. Amen.
Israel ina historia ya ajabu, ya kushangaza, kusikitisha, ya kusisimua na ya kipekee. Nawiwa kuwake dondoo zifuatazo:-
i) Ndio nchi au watu (kama jamii) ambao MUNGU aliwachagua na kujitambulisha kwao na kufanya nao maagano. Kwamba Yeye ni MUNGU wao, na wao ni watu wake na amewapa eneo husika la ardhi kuwa milki yao.
ii) Katika vita kuu ya Pili ya dunia, takwimu zinaonyesha Wayahudi milioni sita waliauwa. Tukio hilo lilikuwa ni moja ya chachu ya kuharakisha mchakato wa uundwaji taifa la Israel, ili Wayahudi wasiendelee kuuawa, kuwa wakimbizi wasio na matumaini ya kuiona nchi ya babu na baba zao.
iii) Israel ni nchi ya kidemokrasia, na Serikali yake huongozwa na Waziri Mkuu anayetokana na chama kilichoshinda uchaguzi. Benyamini Netanyahu ni WM wa 32 wa Israel. Bunge la Israel linaitwa Knesset. Pia Israel ina rais ambaye ni kiungo kati jamii na serikali yao. Inaundwa na majimbo nane kisha mikoa, wilaya na vijiji. Tofauti na jirani zake, Israel haina hazina ya mafuta, gesi au madini.
iv) Israel imestawi sana katikati ya uadui mwingi na vita toka kwa majirani zake na hata mbali ya mipaka yao. Ndio dola la kidemokrasia ya kweli Mashariki ya Kati (MK). Ndio dola lenye uchumi imara zaidi MK, Ndio dola lililoendelea zaidi kisayansi, kielimu, kiviwanda na kilimo MK. Ndio dola lenye nguvu kijeshi MK.
v) Kuelekea Vita ya Siku Sita – 1967 nchi za Kiarabu chini ya Abdel Nasser wwa Misri zilitaka kufunga ukurasa wa "historia" na "aibu" ya kushindwa vita ya 1948, zilizopelekea kuzaliwa taifa la Israel.
vi) Vita ya Siku Sita – 1967, Kiyahudi "Mil'hement sheshet Hayamim", ilianza tar 5 Juni 1967 na kumalizika tar 10 Juni 1967. Tukio moja kubwa katika vita hiyo ni Israel kuukomboa mji wa Yerusalem na kuurudisha katika milki yake.
vii) Uhalali, msingi na utashi wa kuwepo kwa Israel na watu wake hautegemei maazimio ya UN, au America au maoni ya mataifa. Uhalali na msingi wake ni maagano MUNGU wao aliyofanya nao. Ndio maana kila tunaposherehekea kuazaliwa kwa Israel pia huadhimisha uwezo wa neno "Waache watu wangu waende", ambalo Musa alimwambia Farao wa Misri.
Tukitaka kujifunza tuna mengi tunaweza kujfunza kwa Israel kama watu na kama nchi.
MUNGU IBARIKI ISRAEL! MUNGU WALINDE WATU WAKO ISRAEL!