Mawaziri vivuli wa CHADEMA wana uwezo mdogo!

nyumbu wapo kazini, ni nadra watu wa ccm kusimama na CDM ktk hoja HAKUNA! na ndio maana hata Bunge live wamekataa kwani hoja za wapinzani ni kali DHIDI ya zile dhaifu za CCM. na huo ndio ukweli!
Mbona nyumbu hilo ni jina mbadala la bavicha..wewe pilipili kichaa.
 
Ingekuwa kweli basi bunge lingeachwa liwe live ili wapinzani waumbuke!Hali ni tofàuti,wananchi wanawaona wapinzani ndio wenye hoja!Upinzani umepata heshima sana kwa wananchi kupitia bunge!Hilo hakuna mtu timamu anayelipinga!
 
Kwanza ungeeleza mawaziri wa serikali wanafanya kazi vipi?Serikali ni taasis ina maana pia serikali kivuli ni taasis...
 
Post zako huwa ni zisizo na mchango wowote kitaifa zaid ya umbea,mipasho,nk tumia mda wako kutafakar mambo ya msingi sio chuki dhidi ya wapinzani unalishwa maneno machafu na wewe unayabeba bila kutumia kichwa chako,maendeleo hayaji kwa kiwachukia wapinzani na kuwananga kila siku bali kwa msikamano na jitihada za ziada ili kujikwamua kama taifa

Tukirud kwenye hoja yako mbona kuna viongozi wengi sana wameteuliwa awamu hii wakiwemo wakurugenzi,makatibu tawala nk ambao hawana sifa za kutosha kushika nyadhifa hizo? Mbona hujaongelea hilo kama ndio hoja yako kuu? Acha utumwa wa fikra kuamin kuwa mpinzani ni adui yako.
Inawezekana hujui ulisemalo kufanya vibaya serekali sio kigezo upinzani kuiga wao wanatakiwa kuwa mfano na kuwashawishi watu kuwapigia kura na vipi alichoandika mbona hukujibu hoja zake.
 
Ukishakuwa mwanachadema bila kujitoa ufahamu hutadumu nao!ona jinsi huyu alivyojibu !sishangai....uweledi wako mdogo sana!hivi kwa kuwa Sugu ni mwimbaji bongo fleva basi ndo unampa uwazir kivuli habari?unaweza mchagua waziri kivuli kwa kigezo kama hiki!kifupi chama chenu kimekosa watu wenyeuweledi wa kuchambua mambo kiakili au kama wapo hawapewi nafasi ya kutosha!
Kuna Wanaojitoa ufahamu nchi hii kama vijana wa pale Lumumba. Fikirieni kabla ya kuandika humu. Tizama hoja nyepesi mnazoweka mezani sasa. Hii ni sawa na kusema kwamba Bunge lisitunge sheria kwa sababu wabunge sio wasomi wa sheria...
 
Nyie kijani vichwa vigumu sana. Mnapenda kujifagilia sana. Mnafikuri mtaendelea kuingoza hii nchi milele?
Hata KANU walisema hivyo hivyo lkn leo wako wapi?
Kitachowazika ni hiki hapa ''Fao la kujitoa'' km hamtarudisha hili mnajichimbia kaburi nyie wenyew.
Kutoajiri kwa wakati, kuwabana wa diploma mpaka uwe na GPA 3.5 ndiyo uende chuo kikuu.
Msipoangalia mtakufa kibudu km KANU. Mnawachukia bure upinzani, kitachowaondoa ni utendaji mbovu wenu hakuna kingine. Wananchi wanataka watu watakao watetea
Sasa nyie endeleeni kujiaminisha kuwa nyie ni kila kitu.
Mpaka sasa meshapunguza wapiga kura tayari. Mtu anayesubiria ajira kwa sasa halafu aje awapigie kura kijani huyo atakuwa ana mtindio wa ubongo, hivyo hivyo kwa mfanyakazi ambaye katolewa fao la kujitoa na mtu wa diploma.
Nyie endeleeni kujitakasa tu, hata KANU walikuwa km nyinyi. Nyie wenyew shahid uchaguzi uliopita mlikuwa mpaka mnapiga push up. Ujao sijui itakuwaje
 
Hayo ni mawazo yako finyu. Mbona wakija na hotuba zao bungeni mnawaambia wakafute maneno waliyoyaandika? Mnawapangia maneno mnayotaka kusikia ninyi na si wananchi?
 
Uzi wako utapendeza ukiambatanisha na hii picha
1473872395542.png
 
Ingekuwa kweli basi bunge lingeachwa liwe live ili wapinzani waumbuke!Hali ni tofàuti,wananchi wanawaona wapinzani ndio wenye hoja!Upinzani umepata heshima sana kwa wananchi kupitia bunge!Hilo hakuna mtu timamu anayelipinga!
Bunge halina siri,kuna waandishi....pia zama za akina Lamwai,Lwekama,Mutungirehi,Mrema,Slaa hakukuwa na bunge laivu na walitingisha.....kama wangekuwa na hoja wasingekimbilia kiki ya maafa.
 
Ukibishana na chiz na ww utaonekana chizi ni heri kumuacha chiz akutukane mbele za watu ili hali kila mtu anamjua yule n chizi
Sasa na ww jifanye chizi kumjibu chizi utaona watu wanavyo sema ona wale machiz wanatukanana
 
Bunge halina siri,kuna waandishi....pia zama za akina Lamwai,Lwekama,Mutungirehi,Mrema,Slaa hakukuwa na bunge laivu na walitingisha.....kama wangekuwa na hoja wasingekimbilia kiki ya maafa.
Bunge kutowekwa live ni kuifichia aibu serikali na ccm kwa ujumla!Mfano awamu iliyopita wananchi kwa wingi walijionea umahiri wa wapinzani na udhaifu wa ccm ambao walikuwa busy kulinda maslahi ya chama!Nikwambie tu,kama bunge lingekuwa linaipa ccm credit kuliko upinzani basi lingeachwa liwe live!Lakini wapinzani ndio huwa wanapata credit!Hebu angalia kipindi bunge liko gizani,ni michango ya wapinzani tu ndiyo ilikuwa inasambaa kwa wananchi kupitia social networks!Labda wa ccm ni yule wa sanamu la diamond na ukumbusho alipopiga Rais Push up!
 
Bunge kutowekwa live ni kuifichia aibu serikali na ccm kwa ujumla!Mfano awamu iliyopita wananchi kwa wingi walijionea umahiri wa wapinzani na udhaifu wa ccm ambao walikuwa busy kulinda maslahi ya chama!Nikwambie tu,kama bunge lingekuwa linaipa ccm credit kuliko upinzani basi lingeachwa liwe live!Lakini wapinzani ndio huwa wanapata credit!Hebu angalia kipindi bunge liko gizani,ni michango ya wapinzani tu ndiyo ilikuwa inasambaa kwa wananchi kupitia social networks!Labda wa ccm ni yule wa sanamu la diamond na ukumbusho alipopiga Rais Push up!
Kwa vigezo vyako...sababu hakuna siri tena siku hizi, wafuatiliaji wa bunge live ni pungufu ya 2% ya watanzania ambao wengi hujishughulishana siasa,na kwa wale wafanyabiashara,wakulima,wanafunzi hufuatilia bunge pale waziri/serikali inapowasilisha bajeti au ripoti inayowahusu...so sio kigezo. na hayo yote yapo live na ripoti hutolewa kupitia magazeti.
 
Bunge halina siri,kuna waandishi....pia zama za akina Lamwai,Lwekama,Mutungirehi,Mrema,Slaa hakukuwa na bunge laivu na walitingisha.....kama wangekuwa na hoja wasingekimbilia kiki ya maafa.


Acha uongo.
Ungewajuaje kama vyombo vya habari vingekua vinadhibitiwa kama ilivyo leo.
Tena ushukuru tu mana sheria sasa hivi inatungwa kichama. Ukiwa CCM hata utukane mtu kwenye vyombo vya habari na usiku kucha uwe unakashfu wapinzani hakuna hatua itakayochukuliwa. Tuliona vifo vya Mawazo na Dr. Mvungi.

Hata bungeni tunaona wale tunaofuatilia bunge CCM haina wabunge wenye hoja zaidi ya kupitisha miswada kama ilivyoletwa na serikali kwa kugonga meza tu.

Na nikukumbushe pia kuwa tangu wakati wa utawala wa Mwingereza bunge lilikua linatangazwa redioni na wananchi hasa wa vijijini walikua wanafuatilia sana matangazo ya Bunge.
Tusingewajua hao wakina Lamwai ,Mrema , Slaa na wengine kama sio matangazo ya bunge kupitia redio na Tv.
Dr. Slaa alipata umaarufu wakati wa bunge live likiongozwa na Samweli Sita. Kama JK na Sita wangebana bunge na vyombo vya habari tusingewajua watu kama akina Dr. Harison Mwakyembe na hata Viongozi wengi waliopo madarakani.
Kudharau uhuru wa matangazo ya bunge ni ujinga mkubwa kwani utawaumiza zaidi CCM kwani tutarejea enzi zile za kiongozi hakosei. Wale wa mitandao mtabaki mitandaoni tu na hamtaweza kuonyesha jamii uwezo na vipaji vyenu.
Leo hii mwaka mmoja sasa umepita lakini mpaka sasa hakuna mtanzania anayejua kuwa ni mbunge gani kijana wa CCM ambaye ameonyesha uwezo na kipaji cha kujenga hoja kama tulivyowaona enzi za akina January, Nchemba, Kigwangala. Serukamba, Lusinde n.k. achilia mbali wale wa upinzani.
Kwa nchi ya kidemokrasia ambapo watu wanaomba ajira ya uongozi kupitia kura za wananchi ni jambo la hatari sana endapo watu hawataachwa wakaonekana kwenye vyombo vya habari na kwenye shughuli za kisiasa. Ukibana shughuli za kisiasa unazalisha shughuli haram za kisiasa kama zile za siasa kwenye dini na mara nyingine ugaidi. Mana yule anayeonekana sana na kujulikana kwenye nyumba za ibada anaweza kugeuka na kujipigia debe kidini na akapata kura.

Tusifurahiye siasa za gizani kwani tuna shindwa kujua nani anaweza akatufaa kuongoza jamii yetu , nani anatetea maslahi yetu na nani anatoa lugha chafu na nani hana nidham.

Mfano hai upo kwa madiwani. Hawa wameharibu sana mipango ya serikali kwenye halmashauri nyingi kwa sababu wanafanya maamuzi yao gizani. Wengi hawana uwezo kabisa wa kiuongozi na kimipango lakini wanaendelea kuchaguliwa kutokana na ukweli kuwa wananchi hawajui kuwa diwani wa kata nyingine amemzidi kwa kiwango gani diwani wake.
Vikao vya madiwani vingekua vinafanyika hadharani nadhani ubadhirifu mkubwa kwenye halmashuri usingekuwepo mana tungewajua wale ambao hawatoshi kupata nafasi hizo.
Kuna madiwani wa darasa la nne na wameongoza kwa miaka zaidi ya 45 . Wananchi bado wanawachagua kwa sababu ya kutojua ushindani wa kihoja kwenye vikao vya madiwani ambavyo vinafanyika gizani.
Hata mahakamani haki inatendeka kwa sababu mahakama inakuwa huru na kwa uwazi kila mtu anaruhusiwa kuingia na kusikiliza mabishano ya pande zote. Hakuna anyezuiwa kutoa ushahidi wake kwa wazi. Na nadhani kama mahakama ingekua inafanyika kwenye jengo moja tu kama lilivyo bunge kwa nchi nzima basi mahakama ingekuwa ya kwanza kuonyeshwa live kwenye vyombo vya habari.
Pamoja na kwamba mahakimu na majaji hawaombi kuchaguliwa kwa kura lakini bado kesi zinaendeshwa kwa uwazi na kusikilizwa kwa uwazi bila kificho au kuchuja habari.
 
Kwa hiyo ushauri niliyowapa sio kitu?..hayo mengine na wewe yaongelee sina muda wa kuzungumza yote kwa wakati mmoja.Jifunze kuvumilia kukosolewa,usitoe matusi.
POST ZAKO SIKU ZOTE "unajipotezea muda na kupost utumbo"

OVA
 
Mleta mada umeshindwa zaidi kuliko hao uliowataja mana hujaleta ushahidi wowote zaidi ya hisia za kichama.

Nilitegemea uweke hapa mezani Bajeti ya serikali uonyeshe ubora wake na namna inavyotekelezeka mpaka sasa halafu utuwekee na ile ya wapinzani na uichambue ni kwa vipi ina mapungufu na pia haitekelezeki.

Mfano umemtaja Mnyika na Sugu bila kuleta bajeti ya serikali( sitaki kuwataja wahusika mana naweza kuitwa mchochezi) ya Wizara ya Michezo na wizara ya Nishati na madini ukailinganisha na ile ya hao mawaziri vivuli ili tuone kuwa hawakuandika bajeti yenye mipango mbadala zaidi ya kukosoa tuu kama ulivyodai?

Tofauti na hapo watu wanajadili hewa.
 
Back
Top Bottom