Maumivu ya magoti

Mantz

Member
Aug 6, 2009
97
30
Waungwana,

Nina tatizo la miguu (Joint Magotini). Nikitembea miguu inalia kama mifupa inagongana. Huwa nafanya mazoezi ya kucheza mpira wa miguu, hivyo nakimbia sana. Lakini sasa nashindwa kukimbia kutokana na maumivu hayo ya magoti. Msaada wenu.
 
Subiri wanakuja ila kwaupande wangu nakushauri uwe unatumia mboga zenye utelezi kama mlenda na bamia mara kwa mara zitakusaidia sana ndani ya mwezi m1 tu utakuwa vizuri!
 
Mkuu nenda kawaone wataalamu wa mifupa. Kama upo dsm nenda pale MOI weka appointment kumuona Dr.Shareef, au Dr.Mboya au nenda Hindumandal Hospt Kamuone Dr. Kaushik. Hawa ni madaktari wazuri wa mifupa.
Unaweza ukawa na aina mojawapo ya Arthritis kama vile Rhumatoid Arthritis(i just Guess ,mimi si mtaalamu)
 
Back
Top Bottom