waukae
Member
- Feb 12, 2008
- 6
- 0
vijana wa kitanzania waliopo south afrika hali zao zinasikitisha sana wana jf juzi nilipigiwa simu na mmoja wao akiwakilisha wenzie 51 alinambia kwamba maisha ya kule yamewashinda na walikuwa wako uwanja wa ndege wa johernesberg walipopelekwa na maofisa wa ubalozi wa tanzania ili kurudishwa makwao na wengine kwa maelezo yao kwamba walishachanga baadhi ya fedha zao lakini cha kushangaza baada ya kufika uwanja wa ndege wakatelekezwa na hao waliojiita mafisa wa ubalozi wa tanzania, na hivi ninavyoandika wanasema wamerudi tena mitaani kwenda kujisalimisha polisi lakini polisi nao wamewakataa sasa wana jf hebu tutafakari tuwasaidie vipi hawa watanzania wenzetu ambao wanakimbia machafuko huko south afrika? je serikali ya tanzania inashindwa nini kuwasaidia kurudi hawa watanzania mbona kenya wameweza?