Ng`wanakidiku
JF-Expert Member
- Apr 18, 2009
- 1,195
- 232
Ndugu wa JF leo nipo mwanza, na juzi nilibahatika kutemebele kisiwa kimojawapo katika ziwa victoria kiitwacho IJINGA.
Miongoni mwa mambo niliyoyaona katika kisiwa hicho ni utulivu na hari ya hewa ya kuvutia ambayo kama ingekuwa kwa Dar basi pangekuwa na Mbezi Beach nyingi.
Katika maongezi na wakazi wa kisiwa hicho amabacho kina utulivu mzuri nikaambiwa kuna kisiwa kimoja amboacho kipo ndani ya ziwa victoria kuna jamaa amejimilikisha kisiwa na huwa anaua mtu yeyote anayetofautiana naye na hajawahi kuchukuliwa hatua yoyote na wakazi wa hicho kisiwa wanahofu ya kutoa taarifa vyombo vya sheria wakihofia usalama wao.
Sasa nimelimwaga hapa JF ili kama kuna waandishi wa habari basi watafute undani wa hili suala ili lianikwe kwa jamii na vyombo vya sheria vichukue mkondo wake.
Miongoni mwa mambo niliyoyaona katika kisiwa hicho ni utulivu na hari ya hewa ya kuvutia ambayo kama ingekuwa kwa Dar basi pangekuwa na Mbezi Beach nyingi.
Katika maongezi na wakazi wa kisiwa hicho amabacho kina utulivu mzuri nikaambiwa kuna kisiwa kimoja amboacho kipo ndani ya ziwa victoria kuna jamaa amejimilikisha kisiwa na huwa anaua mtu yeyote anayetofautiana naye na hajawahi kuchukuliwa hatua yoyote na wakazi wa hicho kisiwa wanahofu ya kutoa taarifa vyombo vya sheria wakihofia usalama wao.
Sasa nimelimwaga hapa JF ili kama kuna waandishi wa habari basi watafute undani wa hili suala ili lianikwe kwa jamii na vyombo vya sheria vichukue mkondo wake.